Skip to main content

MAABARA YA AFYA YA JAMII PEMBA YAONGEZEWA UWEZO KUGUNDUA MAGONJWA

 



NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@

WAZIRI wa Afya Zanzibar Nassor Ahmed Mazrui amesema, Maabara ya Afya ya Jamii Pemba sasa ina uwezo wa kuchunguza maambukizi mapya na kufanya ufuatiliaji wa magonjwa yenye umuhimu wa afya ya jamii kwa kutumia njia ya kisasa ya kugundua maradhi 'Next General Sequencing (NGS).

Akizungumza mara ya kufungua maabara ya kisasa Wawi Chake Chake Pemba Waziri huyo alisema kuwa, kuwepo maabara hiyo itasaidia kuchunguza maradhi mbali mbali ndani ya kisiwa cha Pemba, jambo ambalo ni faraja kubwa.

Alisema kuwa, awali Wizara ya Afya ilikuwa ikisafirisha sampuli za maradhi nje ya kisiwa cha Pemba jambo ambalo ilikuwa likiwapa usumbufu kwani majibu yalikuwa yanachelewa na kushindwa kugundua kwa haraka maradhi anayougua mgonjwa.

‘’Kwa kweli tupepata faraja kubwa sana kwa sababu sasa maradhi kama Uviko 19, Ebola na magonjwa mengine yatachunguzwa katika mabara hii ya Wawi Chake Chake Pemba, hivyo wataalamu na watendaji wazilinde na kuzitunza mashine kwa kuweka mazingira safi na salama’’, alisema.



Alisema ni lazima Serikali ihakikishe nchi ni salama, ambapo maabara ndizo ambazo zitawahakikishia, hivyo kwa sasa watafanya uchunguzi na ugunduzi wa magonjwa kisiwani Pemba, jambo ambalo ni faraja kwani wameondokana na usumbufu waliokuwa wakiupata.

Alisema kuwa ushirikiano kati ya Serikali na shirika la shirika la kitanzania linaloboresha masuala ya Afya (MDH) kwa kuonesha mafanikio makubwa katika kuimarisha mfumo wa huduma za maabara na afya kwa ujumla, hivyo wataendelea kufanya kazi ili kuhakikisha ushirikiano kati yao na wadau mbali mbali unaendelea kwa ufanisi ili kuboresha ustawi wa jamii yetu.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Wizara ya Afya Zanzibar Dk. Amour Suleiman Mohamed alisema kuwa, wamepata furaha kwa sababu mwanzo kulikuwa na changamoto lakini anaamini kwa sasa imetatuka.

‘’Tulikuwa tunalazimika kusafirisha sampuli kwa zaidi ya siku tano hatujapata majibu, jambo hili lilikuwa linatupa shida lakini kwa sasa tutachunguza ndani ya masaa 24 tutapata majibu, hivyo nawaomba wataalamu waitumie maabara ipasavyo ili kupata majibu sahihi’’, alisema Mkurugenzi huyo.



Nae Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Matar Zahor Massoud alieleza, hatua iliyofikiwa ni kubwa ya kuwepo maabara ya kisasa Pemba kwani inaenda na azma ya Dk. Hussein Ali Mwinyi katika kuimarisha huduma za Afya nchini.

‘’Tumefarajika sana, kwani huduma zitaimarika na uchunguzi wa maradhi utakuwa wa haraka sana na kupata majibu ndani ya muda mfupi’’, alieleza.



Mapema Afisa Uendeshaji Mkuu Maabara Pemba Dk. Said Mohamed Ali alieleza kuwa, maabara hiyo ya kisasa itaisaidia Serikali katika kuboresha huduma za utambuzi na ufuatiliaji wa maradhi mbali mbali.

Aliwashukuru wafadhili wao ambao ni Serikali ya Marekani (CDC) kupitia shirika la kitanzania linaloboresha masuala ya Afya (MDH) wakishirikiana na UNICEF pamoja na Serikali kwani imewarahisishia huduma za uchunguzi na ugunduzi wa maradhi.

Meneja kutoka shirika la MDH David Sando alisema, mategemeo yao ni kuwa uwepo wa maabara hiyo italeta matokeo chanya, hivyo watendaji wa maabara hiyo wafanye kazi kwa ufanisi kwa maslahi ya jamii na Taifa kwa ujumla.

‘’Tulipata msaada wa fedha za Uvico 19 kutoka CDC ambazo ndizo zilizotusaidia kuweka maabara ya kisasa hapa kisiwani Pemba ambayo itaweza kuchunguza magonjwa yote’’, alifahamisha Sando.



Maabara hiyo iliyojengwa kwa ufadhili wa CDC umegharimu kiasi cha shilingi bilioni 3.5.

                                                   MWISHO.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch