Skip to main content

WANANCHI MTEGA WAWI WAKARABATI BARABARA YAO KWA MATOFALI

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA @@@@

WANANCHI wa kijiji cha Mtega, shehia ya Wawi wilaya ya Chake chake Pemba, wameamua kuikarabati barabara yao yenye urefu wa kilomita 2.5, kwa kutumia matofali ya fuuwe na mawe, baada ya kuharibika kwa mvua, inayoendelea kunyesha.

Mwandishi wa habari hizi, aliwashuhudia wananchi hao, wakiwa kwenye eneo la barabara hiyo, wakiikarabati barabara hiyo, kwa kutumia vipande vya matofali na mawe, ili iweze kupitika.

Wananchi hao walisema, uamuzi huo umekuja kufuatia kukosa misaada kutoka mamla husika, hali iliyopekea mvua kuathiri barabara yao.

Mwenyekiti wa kamati ya maendeleo ya kijiji hicho, Khamis Haji, alisema barabara hiyo imeharibika mno, kufuatia mvua zinazoendelea kunyesha nchini kote.

Alieleza kuwa, juzi Mei 4, kamati iliikagua barabara hiyo, na kufikia uamuzi wa kutafuta matofali na mawe, ili kuikarabati katika maeneo, yalioathiriwa zaidi na mvua.

‘’Hivi sasa, kama atatokezea mgonjwa ama mzazi anataka kwenda hospitali, inabidi tutumie gari za Ng’ombe au tutumie magunia hadi njia kuu,’’alieleza.

Mwenyekiti huyo alieleza kuwa, kwa sasa kwenye kijiji chao cha Mtega hakufika, gari wala chombo chochote cha maringi mawili, kutokana na kukatika na kuchimbika kwa barabara yao.

Wakati huo huo, Mwenyekiti huyo amepiga marufuku tabia ya baadhi ya wananchi kuchota mchanga kwenye barabara hiyo, na kusema, atakaepatikana atafikishwa mbele ya vyombo vya sheria.



‘’Wapo baadhi ya wananchi wenzetu, kwa maksudi huchimba mchanga kwenye barabara hii, hivyo tunawataka kila mmoja awe mlinzi kwa mwenzake,’’alifafanua.

Katika hatua nyingine, amemtaka Mbunge na Mwakilishi wa Jimbo la Wawi, kuzitekeleza ahadi walizoziweka za kuwapatia kifusi kwenye bara bara hiyo.

Mshika fedha wa Kamati hiyo, Mwalimu Juma Yahya, alisema kusita kwa mchango wa shilingi 50,000 kwa kila nyumba, ambazo ilikuwa ni kwa ajili ya ununuzi wa kifusi, kumesababisha uchakavu wa barabara hiyo.

‘’Kama lile zoezi la uchangiaji wa fedha, kwa ajili ya ununuzi wa kifusi twengelikamilisha kabla ya mvua, leo barabara yetu isingeharibika sana,’’alieleza.

Hata hivyo, amewakumbusha wananchi wa kijiji cha Mtega na wengine, kuendelea kutoa michango yao, ili kufanikisha ununuzi wa kifusi, mara mvua zitakapomalizika.

Mjumbe wa kamati hiyo Rashid Ali Mussa, alisema lazima katika kipindi hichi cha mvua, mkazo wa kuifanyia ukarabati barabara hiyo uwekwe, na wananchi wenyewe bila ya kutegemea ufadhili.

Nao Ibrahim Mohamed Ali, Hassan Abdalla na Khamis Khatib walisema, lazima kila mmoja, awe mlinzi kwa mwenzake, juu ya suala la uchimbaji wa mchanga kwenye barabara yao.




Bara bara ya kijiji cha Mtega, shehia ya Wawi wilaya ya Chake chake, iliyoanzia Wawi kwa Gerei, yenye urefu wa kilomita 2.5 kupitia mtega uwanja wa mpira, hadi mwanzo wa kambi za Jeshi la wananchi, iliasisiwa mwaka 2016 na wananchi wenyewe.

                        Mwisho                                                                 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch