Skip to main content

MWARUBAINI HUU HAPA WA KUMALIZA TABIA YA KUWAUWA WATUHUMIWA ZANZIBAR

 


 

I

NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

‘’ATAKAYE muua mwenzake, basi naye anyongwe, na kinga kuwa alikuwa na hasira isifanye kazi, yakifanyika hayo, kujichukulia sheria mikononi itakoma,’’wanasema wahanga wa matukio hayo.

WAHANGA WANATOA RAI GANI?

Mke ambaye muume wake aliuawa mwaka 2020 eneo la Micheweni kwa wananchi waliodaiwa kuwa na hasira, anasema njia pekee ya kuondoa utamaduni wa wananchi kujichukulia sheria mikononi, naye ni kuuliwa.

Kijana Issa Haji Othman wa Mwanakwerekwe, anasema njia nyingine ya kukomesha wananchi kujichukulia sheria mikononi, ni kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria.

Mayasa Haji Mzee wa Chake chake, anasema ili kukomesha wananchi kujichukulia sheria mikononi, ni wananchi kuelezwa mifumo ilivyo ya haki jinai.

‘’Wananchi hawaelewi kwa undani, mifumo ya haki jinai, kuanzia kesi inapokuwa Polisi, Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka hadi Mahkamani pamoja na haki ya dhamana au rufaa,’’anasema.

VYOMBO VYA KUSIMAMIA HAKI JINAI VINASEMAJE?

Kamanda wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba Juma Saad Khamis, anashauri, elimu zaidi itolewa ya athari ya kujichukulia sheria mikononi.

‘’Nadhani wananchi hawajui madhara ya kujichukulia sheria mikononi, sasa kama wataelewa, inaweza kuwa njia moja ya kupunguza utamaduni huo,’’anashauri.

Afisa Sheria kutoka Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria Zanzibar ofisi ya Pemba Bakar Omar Ali, anasema wananchi waelimishwe, ni maana na sheria na mifumo yake katika mahakama.

‘’Wananchi wanadhani kama vile mtuhumiwa hana haki zake, ikiwemo dhamana au kukata rufaa, sasa yanapofanyika haya pasi na uwelewa, hujichukulia sheria mikononi,’’anaeleza.

Mratibu wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Pemba Suleiman Salim, anasema ili kupunguza wimbi la wananchi kujichukulia sheria mikononi, ni kuenezwa kwa elimu ya sheria.

Sheha wa shehia ya Wawi, Sharifa Waziri Abdalla, anasema vyombo vya ulinzi na usalama, viharakishe upelelezi wa makosa mbali mbali, ili kupunguza hasira kwa wananchi.

Kamishna wa Polisi Zanzibar Hamad Khamis Hamad, anasema njia rahisi ya kupunguza wananchi kujichukulia sheria mikononi, ni kuwa na kasi ya uendeshaji wa kesi za jinai.



‘’Ile tabia ya wananchi kukataa kutoa ushahidi isiwepo, majaji na mahakimu wapungze dharura, ili kesi hizo ziende kwa haraka na haki ipatikane,’’anashauri.

Jaji Mkuu wa Zanzibar Khamis Ramadhan Abdalla, anashauri kuwa, kama mifumo ya uendeshaji wa kesi itafumuliwa na kuwa rahisi zaidi, wananchi watakoma kujichukulia sheria mikononi.

‘’Inawezekana mifumo yetu ya kuanza upelelezi, utoaji wa ushahidi, kujitetea, kukata rufaa, dhamana na kutia wakili, pengine wananchi wanaiona ina mizunguruko, yengefumuliwa kidogo,’’anashauri.



Aliyekuwa Mratibu wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ‘ZLSC’ Zanzibar ofisi ya Pemba Safia Saleh Sultan, anashauri kuwa, kila mmoja awe mlinzi kwa mwenzake, ili kuondoa wananchi kujichukulia sheria mikononi,’’anashauri.

Mwanasheria wa serikali kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka Ali Amour Makame, anasema wananchi kufika mahakamani kutoa ushahidi, itasaidia kuondoa changamoto hiyo.

VIONGOZI WA DINI WANASHAURI NINI?

Mratibu wa Ofisi ya Mufti Pemba, sheikh Said Ahmad Mohamed, anasema, kama waumini watashibisha elimu ya kiroho, inaweza kusaidia, kuondoa tabia ya kujichukulia sheria mikononi.

‘’Maana uislamu umekataza moja kwa moja kumwaga damu, sasa kama waumini wa dini ya kiislamu watapewa elimu hii, inaweza kusaidia jambo hilo,’’anashauri.

 Mchungaji Samuel Eliyas Maganga kutoka Kanisa la Tanzania Assembles of God ‘TAG’, anasema njia ya kuondoa tabia ya kujichukulia sheria mikononi, ni waumini, kufungwa kimoyo na kiroho.

‘’Sisi viongozi wa dini, tuwafunge kiimani waumini wetu, tukiwaeleza athari ya kumwaga damu na madhara ya kuua, ambayo ni kazi halali ya Muumba,’’anashauri.

Mchungaji Benjaman Kissanga, anasema kama viongozi wa dini watatoa hutuba zenye kukemea tabia hiyo, kila wanapokutana na waumini wao, inaweza kusaidia.

Sheikh Mohamed Issa Kombo, anasema waumini wa dini ya kiislamu, kama watapewa elimu ya kumjua Muumba na kazi zake, kuna uwezekano wa kupungua matendo hayo.

WANAHARAKATI WENGINE WANAONAJE?

 Mkurugenzi wa Jumuiaya ya Wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba ‘CHAPO’ Nassor Bilali Ali anasema, ni wananchi kujenga utamaduni wa kuhudhuria vikao na mikutano wanayowekewa, ili wapate njia za kushughulikia kesi na malalamiko.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wasioona Pemba ‘ZANAB’ Suleiman Manssour anasema, njia rahisi ya kuondoa tabia ya wananchi kujichukulia sheria mikononi, ni vyombo vya haki jinai kutenda haki.

‘’Inatokea familia imeshauliwa ndugu yao, kisha Hakimu anayeshughulikia kesi hiyo kwa tamaa zake anachukua rushwa, na mtuhumiwa anaachiwa, hapo ndipo hasira za kujichukulia sheria mikononi inapotokezea,’’anasema.



Mwakilishi wa Jimbo la Konde Zawadi Amour Nassor, anasema njia pekee ya kumaliza tabia hiyo, ni wananchi kujengwa kiuzalendo katika jamii.

Mratibu wa Jumuiya wa ajili ya watu wenye ulemavu Zanzibar ZAPDD tawi la Pemba Khalfan Amour Mohamed, anasema mifumo ya haki jinai isipowazingati wananchi wenye kipato cha chini, matendo hayo yanaweza kuongezeka.

WATAALAMU WA AFYA AKILI WANASHAURI NINI?

Dokta Ali Yussuf, mtaalam wa saikolojia ya binaadamu, anasema cha kufanya ni vyombo vilivyopewa mamlaka, kushirikiana na jamii, kwenye utungaji wa sheria.

Jengine anaona ni kwa vyombo vya kusimamia haki, wasizipindishe sheria, wakifanya hivyo jamii itawaamini na kutoa taarifa zaidi kwenye matukio hayo.

Daktari mwengine wa saikolojia Mtumwa Hija Mzale anasema, uwezo wa akili ya mwanadamu, ni kuvumilia kosa la mwanzo, hivyo la pili, likitokezea hupenda kujichukulia sheria mwenyewe, na sio vyombo kuzuia makosa.

‘’Saiokolojia ya mwanadamu haipendi kuona kuna adhabu kali, lakini hakuna mikakati ya kuzuia makosa ya jinai yasiotokee, hivyo wajibu huo bado upo,’’anashauri.

NINI KIFANYIKE?

Haroub Shein Hassan, anasema uhuru wa kufanya kila mmoja apendavyo bila ya kuchukuliwa hatua, usiwepo kwani unaweza kuzaa madhara kwa jamii.

Mayasa Himid Mjaka, wanasema vyombo vya ulinzi na usalama, viweke mazingira ambayo ni laini na mwafaka kwa watu wa madaraja yote katika jamii.

Kamisha wa Polisi Zanzibar Hamad Khamis Hamad, anasema ni wananchi kupewa elimu ya sheria, na hasa ya namna ya uendeshaji wa kesi za jinai mahakamani.

Jaji Mkuu wa Zanzibar Khamis Ramadhan Abdalla, anasema wananchi waekelezwe juu ya haki za mtuhumiwa, mara tu baada ya kushikiliwa, ikiwemo dhamana na rufaa.

Mratibu wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Tanzania ofisi ya Pemba Suleiman Salim, anasema wananchi wakifundishwa manufaa ya kutoa ushahidi mahakamani, matendo hayo yataondoka.

RIPOTI YA UHALIFU TANZANIA KWA UPANDE WA ZANZIBAR

Ripoti ya uhalifu na makosa ya usalama barabara ya Jeshi la Polisi Tanzania ya mwaka 2020, inaonesha kuwa wapo wananchi 124 wameshauawa, kutokana na watu kujichukulia sheria mikononi visiwani Zanzibar.

Uchunguzi umebainika, hao ni wa kipindi cha miaka 10, kati ya mwaka 2011 hadi mwaka 2020, kwa mikao mitano pekee ya Zanzibar.

Kwa idadi ya wananchi hao waliouawa, kwa tuhma za kufanya uhalifu, ni sawa na kila mwaka, wastani wa watu 13 kuuawa visiwani humo katika kipindi hicho.

Kwa idadi hiyo, ilisababisha punguzo la watu kutoka milioni 1,303,569 waliohesabiwa kwenye sensa ya mwaka 2012, hadi kufikia watu milioni 1,303,445.

Watu wao waliouawa kwa Zanzibar, Mkoa wa mjini Mgharibi Unguja, ulioongozwa kwa miaka yote hiyo, na takwimu hizo haijwahi kushuka.

Imebainika kuwa, mwaka 2011, Zanzibar kuliripotiwa matukio manne (4), mkoa wa Mjini mgharibi pekee, uliripoti matukio matatu (3).

Hali hiyo, iliripotiwa kutisha zaidi katika mwaka 2017, kulikoripotiwa wananchi 26 waliouawa, ambapo kati yao, 18 walikuwa wa mkoa wa Mjini magharibi.

Kwa mwaka huo mikoa mingine ya iliyoripoti matukio mengi zaidi, ni mkoa wa kusini Unguja, matano (5), kusini Pemba matatu (3), na mikoa mengine kukiwa hakuna vifo vilivyoripotiwa.

Mwaka 2019, ulibeba matukio 17, uchunguzi ukaonesha matukio 12 yalikuwa mkoa wa Mjini magharibi pekee, kusini Pemba matukio mawili (2) na mikoa mengine kukiwa na idadi sawa na tukio moja moja.

Hata mwaka 2020, mkoa wa Mjini magharibi, ulikusanya matukio 10, ya mauwaji kwa wananchi kujichukulia sheria mikononi, kati ya matukio yote 15 yaliyoripotiwa. 

NINI CHANZO?

Hafsa Issa Khamis Ali wa Mwanakwerekwe mkoa wa Mjini magharibi Unguja, anasema, chanzo ni jamii kukosa maadili, huruma na kukosa utu.

Khadija Mansour Haji wa Kiwajuni wilaya ya Mjini Unguja, ambae mwaka 2019 muume wake alipoteza uhai, kwa kushambuliwa na wananchi wakati wa usiku, anasema chanzo ni sheria kuwa lege lege za wanaoua.

Mohamed Kassim Othman wa Gulioni wilaya ya mjini Unguja, anasema chanzo ni jamii kukosa uwelewa, juu ya kumfikisha katika vyombo vya sheria mtuhumiwa wa aina yoyote.

Kheir Makame Haji wa Chake chake Pemba, anasema bado jamii haijapata elimu ya athari ya kujichukulia sheria mikononi, na ndio maana visa hivyo mkaoni humo viko juu.

Mwanakhamis Muhidin Juma wa Mzingani Mkoani Pemba, anasema mifumo ya haki jinai, kuanzia siku ya kwanza ya kuripotiwa kwa tukio hadi siku ya hukumu ni shida.

NYARAKA

Katiba ya Zanzibar yam waka 1984, kifungu cha 13 kimebainisha kuwa ‘kila mtu anayo haki ya kuwa na hifadhi ya maisha yake kwa mujibu wa sheria’.

Kifungu hicho kifafanua kuwa, ‘kila mtu anayo haki ya kuishi na kupata hifadhi, na ni marufuku kuteswa, kuadhibiwa kinyama au adhabu zinazomdhalilisha’.

Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 Ibara ya 15 ikafafanua kuwa, ‘kila mtu anayo haki ya kuwa huru na kuishi kama mtu huru’.

Mkataba wa haki za binadamu wa mwaka 1948 kuanzia ibara yake ya 3 hadi ya 8, imekataza kwa mtu kuteswa, kuadhibiwa, kwani yuko huru kulindiwa.

Mkataba wa kimataifa wa haki za kiraia na kisiasa wa mwaka 1966, ambao Tanzania uliuridhia mwaka 1976, Ibara ya 1, umeanisha haki ya kuishi, ukamilifu na usalama wa mtu.

 

                         Mwisho

 

 

 

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch