Skip to main content

SIKU YA URITHI AFRIKA YAADHIMISHWA PEMBA , RC KUSINI ASEMA JAMBO

 



NA MARYAM SALUM, PEMBA@@@@

WANANCHI Kisiwani Pemba wametakiwa kuonesha ushirikiano kwa Serikali,  juu ya  jitihada zinazofanywa na viongozi wa nchi katika kusaidiana  kuenzi urithi, ili kizazi kilichopo na kijacho kiweze kufaidika.

Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Mattar Zahor Massoud wakati akizungumza na wanachama wa jumuia ya Urithi Pemba  pamoja na wafanyakazi mbali mbali katika kilele cha maadhimisho ya siku ya Urithi duniani Afrika,ambapo kitaifa kwa pemba kilele kimefanyika tenis Chake Chake.

Alisema kuwa Serikali ya Tanzania Bara na ya Zanzibar kupitia Viongozi wake ilifanya jitihada za makusudi kwa kuandaa kipindi maalum cha kutangaza utalii duniani kama urithi wa afrika.

Alisema kuwa kutokana na jitihada zinazonywa na viongozi hao wananchi ipo haja kwa  kuunga mkono jitida hizo ili lego liweze kufikiwa.

 “Viongozi wetu wakuu akiwemo Rais wa Jamuhuri ya Tanzania Dk. Samia na Dk. Huseein Mwinyi kwa kushirikiana wameandaa mpango maalum wa kutangaza utalii kama urithi wa Tanzania,”alisema Mkuu huyo wa mkoa.

Mkuu huyo alieleza kuwa katika kutekeleza kazi hiyo walifika kwenye maeneo mbali mbali ya vivutio vya utalii kwa Tanzania bara na Zanzibar, kwa lengo la kuonesha wengine duniani.

Alisema kuwa kazi iliyofanywa na viongzoi  nchini katika kutangaza utalii imeweza kuleta matunda makubwa, kwani kumekuwa na ongezeko la idadi ya watalii kutoka nchi mbali mbali kuja Tanzania na Zanzibar.



“Idadi ya watalii waliokuja Zanzibar  kwa mwaka 2022 ni kubwa na kufikia 27,826 kuliko wakati wote katika historia ya nchi hii,” alieleza Mkuu huyo wa mkoa.

Alifahamsha kuwa wakati duania inapoadhimisha siku ya urithi duniani Afrika ni wakati wa kutafakari kwa kina juu ya maendeleo na changamoto ya ya Urithi katika taifa hili.

Alisema kuwa kuna haja kwa wananchi wapate nafasi yakuweza kutafakari kuhusiana na kazi na juhudi ya mipango ya maendeleo inayotekelezwa na viongozi knchini katika kutunza kuhifadhi na kuimarisha urithi walioachiwa na vizazi vilivyotangulia.

“Niwakati nzuri kwa Jumuia ya urithi Pemba na Wizara husika kuhakikisha wanaangalia penye changamoto kutatua, na namna bora pale walipofanya  vizuri kuendeleza,” alieleza.

Alieleza kuwa Wizara ya Utalii inaendelea kuimarishwa na kutunza maeneo mengi  kama vile ya Urithi,maeneo ya kihistoria  na mambo ya kale, ili kuimarisha utalii kisiwani Pemba.  

Hivyo wananchi wahakikishe wanalinda tamaduni zao, kulinda urithi ambao wameachiwa ili kurithisha vizazi vyao.



Kwa upande wake Afisa Mdhamini Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale Pemba, Zuhura Mgeni Othman alisema kuwa lengo la kuadhimishwa kwa siku ya urithi duniani afrika ni kuenzi urithi huo.

“Kila ifikapo Mei 5 ya kila mwaka duniani kote afrika huadhimisha siku hii kwa matamasha na tamaduni zote za asili ya Afrika,” alisema mdhamini.

Alisema kuwa Wizara inaendelea kuimarisha na kuenzi maeneo mbali mbali ya kihistoria kwa kuyafanyia ukarabati likiwemo eneo la kihistoria la Mkumbuu, Chwaka tumbe na pango la watoro na Mkamandume.

Aidha kuipongeza Serikali ya Mapinduzi kutoa fedha nyingi kwa ajili ya kufanyiwa marekebisho maneo mbali mbali ya historia, lengo likiwa ni kuimarisha zaidi kiutalii.




Mapema akisoma risala ya siku ya Urithi duniani Afrika Mwenyekiti wa Jumuia ya Uhifadhi Urithi Pemba Haji Seif Yussuf, alifahamisha kuwa   imeweza kufanikiwa kwenye mambo mbali ikiwemo, kusaidiana na Serikali kuhakikisha urithi wa Pemba unakua hai na endelevu kwa vizazi vya sasa na baadae.

“Kutafuta wadau wa mambo ya kale na urithi kwa ajili ya kufanya tafiti mbali mbali Kisiwani humu, pamoja na kutoa elimu ya uhifadhi wa Urithi na mazingira kwa jamii kwa miaka miwili sasa,” alieleza Mwenyekiti.



Siku ya Urithi duniani huadhimishwa kila ifikapo Mei 5 ya mwaka duniani Afrika, ambapo kauli mbiu ya mwaka huu kwa upande wa Pemba, Uhifadhi wa urithi ndio mafanikio ya hazina yetu.

                                        MWISHO.

 

 

 

 

 

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch