Skip to main content

SOKO LA ASALI LAJA ZANZIBAR

 



WAZIRI  wa Ardhi na Maendeleo ya Makaazi  Rahma Kassim Ali amesema kuwepo kwa kituo cha usarifu wa asali  nchini kutaimarisha upatikanaji wa bidhaa hiyo na kuondokana kwa tatizo la                     kukosekana kwa soko la zao hilo hapa Zanzibar.

Akizungumza katika uzinduzi wa kituo cha kusarifu asali huko Kizimbani Unguja Wilaya ya Magharibi "A"ikiwa ni shamrashamra za kuelekea miaka 59 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar. Alisema ujenzi wa kituo hicho utawasaidia wajasiriamali wadogo wadogo kukuza kipato  pamoja na ajira kwa  makundi mbali mbali wakiwemo  vijana na wanawake.

 Alisema kua ujenzi wa vituo hivyo ni muhimu kwa upande wa Unguja na Pemba ambapo ni miongoni mwa jitihada za Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) katika kuimarisha rasmi Sekta ya Uwekezaji  kiuchumi ili kuleta tija kwa wananchi kwa ujumla.

"Vituo hivyo vitasaidia sana kuwawezesha wananchi hasa wanawake kujikwamua kiuchumi na kuondokana kua tegemezi kwani watakua wamejiajiri na kuondokana na ugumu wa  maisha”Alisema  Waziri Rahma.

Aidha alisisitiza umuhimu wa kuyatunza majengo hayo kwa watendaji katika kuimarisha usafi ili kuweza kufikia lengo lililokusudiwa, kwani SMZ inamalengo makubwa katika kuwainua wananchi kupitia Sekta ya Uwekezaji Kiuchumi hivyo haitapendeza baada ya muda mfupi majengo hayo kuonekana hayaridhishi kimazingira pamoja utendaji kazi.



Mapema Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Kazi Uchumi na Uwekezaji Mudrik Ramadhani Suraga  aliwataka wajasiriamali hao kuzalisha asali iliyo bora ili kuweza kuingia katika ushindani wa kibiashara wa ndani na nje ya nchi kwani SMZ  itaendelea kuwawezesha wananchi kiuchumi kupitia miradi mbali mbali.

“Mkizalisha asali bora itaweza kuingia katika soko la ushindani wa kibiashara na Serikali ya awamu ya nane inayoongozwa na Mhe. Rais wa Zanzibar na Mwenyeki wa baraza la Mapinduzi Dkt Hussein Ali Mwinyi inamipango mizuri kwa wananchi wake kupitia  sekta hii” Alisema Suraga.

Kwa upande wake Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Kazi Uchumi na Uwezeshaji wananchi kiuchumi  Maryam Abdalla Juma alisema ujenzi wa kituo hicho ulianza mwaka jana mwezi Machi,2022 na umegharimu jumla zaidi ya shilingi  Milioni mia mbili (236,325,000/= ).

Alifahamisha kwamba katika juhudi ya kuwawezesha wananchi kiuchumi jumla ya wajasiriamali 753 kutoka Uguja na Pemba wakiwemo wanaume 280 na wanawake 473 walipatiwa mafunzo ya ufugaji wa nyuki kwa nadharia na vitendo ikiwa ni hatua ya kuwajengea uwezo katika utaalam wa kufuga nyuki.

Aidha Katibu Mkuu huyo  alisema kua ununuzi wa vifaa vya ufugaji wa nyuki kwa wajasiriamali umegharimu jumla ya shilingi milioni mia sita nukta 2.5 (625,000,000/=) ambapo vifaa hivyo tayari vimeshagaaiwa kwa wajasiriamali wote waliopatiwa mafunzo Unguja na Pemba kupitia Ofisi za Mikoa.

Naye mjasiriamali wa ufugaji wa asali faraja Ali Hassan ameishukuru Serikali ya Mapinduzi Zanzibar pamoja na Wizara ya Kazi, Uchumi na Uwekezaji  kwa kuwapatia mafunzo hayo pamoja na kuwajengea kituo cha kusarifu asali hatua itakayowasaidia katika kujikwamua na hali ngumu ya maisha hivyo aliahidi kuyaafanyia kazi mafunzo waliyopatiwa kwa vitendo.

 Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch