Skip to main content

FAMILIA ZENYE WATOTO WENYE ULEMAVU PEMBA WAKUMBUSHWA JAMBO

 

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA::

WAZAZI na walezi kisiwani Pemba, wamekumbushwa kuwa, sio haki watoto wenye ulemavu kukoseshwa haki zao za msingi, kama elimu na kuchanganyika na wenzao, kwa sababu ya ulemavu walionao.

Hayo yameelezwa na Mratibu wa Idara ya watu wenye ulemavu kisiwani humo, Mashavu Juma Mabrouk, wakati akizungumza na wazazi, walezi na wanafunzi wa madrssa za Umi ya Vikunguni na ile ya Annajah ya Machomane Chake chake, kwenye ziara iliyoandaliwa na Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria Zanzibar.

Alisema, bado baadhi ya wazazi na walezi, wamekuwa wakijenga dhana kuwa, mtoto mwenye ulemavu anahiari ya kumpatia elimu, na asiyekuwa na ulemavu ndio mwenye haki kamili.

Alieleza kuwa, dhana hiyo isiwapitikie wazazi hata siku moja katika maisha yao, na badala yake wawe na haki sawa watoto wenye ulemavu na wengine, ili kutimiza matakwa ya kisheria.

Mratibu huyo alisema, suala la uwep wa changamoto kwenye sekta ya elimu kama vile uhaba wa vifaa visaidizi kwa watoto wenye ulemavu, isiwe sababu ya kuwafungia ndani na kuwakosesha haki hiyo.

Alieleza kuwa, sera ya elimu inataka watoto wote wenye umri wa kupata elimu, wawepo kwenye mfumo wa elimu, ili zinapotokea changamoto, ziwakuwate wakiwa madarasani.

‘’Ipo tabia ya baadhi ya wazazi, wakiona wamepata mtoto mwenye ulemavu, ameshapata kichaka cha kumtopeleka skuli au madrassa, akifikiria kuwa hawezi na atachekwa na wenzake, hilo sio sahihi,’’alieleza.



Hata hivyo amewataka wanafunzi waliomo kwenye mfumo wa elimu, kuendelea kuwashawishi wazazi na walezi wao, ikiwa kuna wenzao wenye ulemavu wamefungiwa ndani, nao waandamane nao kutafua elimu.

Katika hatua nyingine Mratibu huyo wa Idara ya watu wenye kisiwani Pemba Mashavu Juma Mabrouk, ameitaka jamii kuendelea kupanga mikakati madhubuti, ili kuwalinda na udhalilisha watoto wenye ulemavu.

‘’Watoto wote wanakabiliwa na hali mbaya ya kufanyiwa vitendo vya ukatili na udhalilishaji, ingawa sasa wabakaji wamekua wakikimbilia zaidi kwa watoto wenye ulemavu, wakidhani hawawezi kueleza chochote mahakamani,’’alieleza.

Hata hivyo alisema wazo la Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria Zanzibar, kuandaa ziara ya kuwapitia wanafunzi, ili kuzungumza nao juu ya namna ya kukabiliana na matendi hayo, ni nzuri.

 Kwa upande wake Mwakilishi wa Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria Zanzibar ofisi ya Pemba Mohamed Massoud Said, alisema, moja ya dalili ya mtu anaetaka kumdhalilisha mtoto, huanza kwa kumuonesha picha za ngono, kumnunulia zawadi, kumpa fedha, na kuendelea kwa maneno ya ushawishi juu ya udhalilishaji.

Hata hivyo, amewataka wanafunzi, waalimu, wazazi na walezi kuitumia Idara hiyo, kwa kutoa taarifa za matukio hayo, au uwepo wa watu wanaojaribu, kuzifanyia sulhu kesi za udhalilishaji.



Mkurugenzi wa Jumuiya wa wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba ‘CHAPO’ Nassor Bilali Ali, amesema kama jamii haikushirikiana katika ulinzi wa watoto, kusitarajiwe matendo hayo kupungua.

Akizungumza kwenye ziara hiyo, Mratibu wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ‘ZLSC’ tawi la Pemba Safia Saleh Sultan, aliwataka wanafunzi hao, kutomruhusu mtu yeyote, kuuchezea mwili wake.

‘’Sehemu zako za siri ni mali yako, usimuonesha mtu mwengine wala usikubali kuguswa kama hakuna sababu inayokubalika, maana huo ndio mwanzo, wa udhalilishaji unapoanzia,’’alieleza.

Hata hivyo amesema, lazima ulinzi kwa watu wenye ulemavu uimarishwe mara mbili, ili wawe huru na matendao ya udhalilishaji wa kijinsia.

Mwalimu mkuu wa Almadra-ssatul-Annajah Imani Ali Mohamed, alisema ziara hiyo kwao ni faraja, katika kuwakumbusha wanafunzi juu ya kujikinga na matendo hayo.

Kwa upande wake Msaidizi mwalimu mkuu wa Almadra-ssatul-Umi ya Vikunguni Zubeda Yussuf Mohamed, alisema bado wazazi hawajaona umuhimu, wa kushirikiana na waalimu, katika malezi ya watoto.

Ziara hiyo ya kutoa elimu ya kupambana na makosa ya udhalilishaji na ukatili wa kijinsia, ni muendelezo ya mikakati ya Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria, katika kuhakikisha kundi la wanawake na watoto, linaishi pasi na ukatili.






Ripoti ya Jeshi la Polisi Zanzibar, inaonesha, kwa mwaka 2021, kulikuwa na matendo 1,222 ya wanawake na watoto kudhalilishwa Unguja na Pemba.

Aidha ripoti nyingine ikaonesha kuwa, kulikuwa na matukio 610 ya aina hiyo, kwa kipindi cha miezi mitatu mitatu ya mwaka 2021 na 2022.

                     Mwisho

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch