Skip to main content

ALIYEKATWA MIGUU KWA TUHUMA ZA WIZI PUJINI SASA ATUMIA YA BANDIA

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA:::

KIJANA Gizahibu Ali Amour miaka 38 aliyekatwa miguu yote miwili, miaka mitatu iliyopita kwa tuhma za wizi, shehia ya Pujini wilaya ya Chake chake, amepona na kupata ulemavu wa kudumu.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa njia simu, Januari 8, 2023 alisema licha ya kuwa bado yuko hai, lakini amepata ulemavu wa kudumu na kulazimika kutembelea miguu ya bandia.

Alisema, mguu mmoja wa bandia aliununua kwa shilingi 400,000 ambapo kwa hatua za awali alichangia na ndugu na jamaa, marafiki na madaktari katika hospitali aliyokuwa amelazwa.

Alieleza kuwa, sasa ni mwaka mmoja, tokea atoke hospitali na kutumia miguu ya bandia, na imeanza kumbana na kuanza kuisaidia kwa mgongo mawili.

Kijana huyo alieleza kuwa, kama hakupata usaidizi tena, anachokiona mbele yake, ama ni kubakia nyumbani muda wote au kutembelea magongo, kwenye safari zake ndogo ndogo.

‘’Kwani nipo nyumbani na ilikuwa natembelea vyema miguu yangu ya bandia, lakini sasa imeshaanza kuchakaa na kama sikupata ufadhili, itabidi nitembelee magongo,’’alieleza.

Akizungumzia kuhusu maisha yake, alisema kwa sasa anaowatoto watano wanaomtegemea, ingawa hana mke anayemsaidia kimaisha.

‘’Hali yangu ya maisha kwa sasa, ni ya kubahatisha, siku zote ili nipate chakula kazi kubwa ni kuomba msaada kwa wahisani, wapita njia na kisha ndio niwapelekee na watoto wangu,’’alieleza.

Hata hivyo alisema, tuhuma za yeye kuwa ni mwizi na kupelekea kukatwa miguu miwili, hazikuwa za kweli, na ndio maana hadi leo hakuna aliyemlalamikia.

Kwa upande mwengine, wapo watu 25 waliwahi kuhojiwa na Jeshi la Polisi mkoa wa kusini Pemba, kwa tuhma za kumshambulia kijana huyo.



Ingawa hakukua na yeyote alipandishwa mahakamani, na baada ya kuhojiwa watu hao wote, waliachiwa huru, huku kijana huyo kwa wakti huo akiendelea kuuguaza majereha.

Mmoja kati ya wanafamilia wa kijana huyo, ambae hakupenda jina lake lichapishwe, alisema kijana huyo baada ya kumuuguza kwa mwaka mmoja na nusu, sasa anatembea kwa kutumia miguu ya bandia.

Alieleza kuwa, kijana huyo alionewa kwa kudhaniwa kuwa aliiba, ingawa hadi leo, hakuna yeyote aliyeripoti kwa jeshi la Polisi kuibiwa jambo lolote.

Alieleza kuwa, ni vyema kwa sasa, kwa wale watuhumiwa zaidi ya 25 waliokamatwa na kuhojiwa na kisha kuachiwa, kuona haki inatendeka, kwa vile kijana wao amepata ulemavu.

‘’Kijana Gizahibu Ali Amour miaka 38, alikutikana pembezoni mwa barabara, akilalamikia maumivu makali, baada ya watu wasiojulikana, kutumia kitu chenye ncha kali, kumkata miguu  yote,’’alieleza.

Baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo walisema, mtu huyo baada ya kukatwa viungo hivyo na kuachwa karibu na alipotupwa na kuanza kuugua kwa maumivu, alitoa sauti, iliosababisha wapita njia kumuona.

Baadae, mpatwa na jali huyo, alifikishwa hospitali ya Chakechake kwa matibabu, ingawa ilishindikana na kupelekwa hospitali ya Mkoa ya Abdalla mzee, Mkoani Pemba.

Aliyekuwa Katibu wa hospital hiyo, Ali Omar Mbarawa, alithibitisha kumpokea majeruhiwa huyo, na kusema imeshindikana, kuvirejesha viungo hivyo vya miguu yake.

 “Ni kweli tulimpokea mjeruhiwa akitokea hospitali ya Chakechake kwa rufaa, akiwa hali mbaya, maana viungo vyake vya miguu viko mbali na yeye, na sio rahisi kuvirejesha tena,’’alieleza.

Aliyekuwa Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa kusini Pemba Said Omar Dadi, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo, lilitokea August 4, mwaka 2018 majira ya saa 2:00 usiku.

 Hata hivyo Kaimu Kamanda huyo amekemea vikali tabia ya wananchi kujichukulia sheria mikononi, wanapoona kuna mtu ametenda au anania ya kufanya uhalifu katika sehemu zao.

Miezi miwili iliopita kijana mwengine wa Pujini Abdalla Mohamed Amour ‘babu dii’ alipigwa ndani mwake na watu wasiofahamika na kusababisha kupata ulemavu wa mguu na mkono.



Kwa mujibu wa taarifa za uhalifu zilizochapishwa na Jeshi la Polisi Tanzania mwaka 2017, imeonesha kuwa matukio ya kujichukulia sheria mikononi, yamezidi kuongezeka nchini, ambapo katika kipindi cha Januari hadi Disemba, 2017 watu 917 waliuawa.

Aidha taarifa hiyo ya Jeshi la Polisi Tanzania, ilieleza kuwa, idadi hiyo iliongezeka kidogo, ikilinganishwa na watu 912 waliouawa katika kipindi kama hicho kwa mwaka 2016, ambapo hilo ni ongezeko la watu 5 ambao ni sawa na asilimia 0.5.

Kwa Zanzibar pekee katika kipindi hicho cha miaka miwili, Jeshi hilo la Polisi liliripoti idadi ya watu 47 waliouwawa, huku mkoa wa mjini Magharibi ukiwa na watu 34, kusini Unguja saba.

Mkoa wa kusini Pemba, wakiripotiwa wanne, wakati Mkoa wa kaskazini Pemba na Mkoa wa kaskazini Unguja wakiwa na idadi sawa ya mtu mmoja mmoja, ingawa kwa mikoa ya kipolisi Konondoni iliongoza kwa watu 189, ikifuatiwa na Temeke 128.

                       Mwisho

 

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch