Skip to main content

WANANCHI PEMBA WADAI KULAZIMISHWA CHANJO YA CORONA, WIZARA YATOA TAMKO

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA:::

WIZARA ya Afya Zanzibar, imepiga marufuku kwa daktari yeyote, kumlazimisha mwananchi kuchoma chanjo ya kinga ya Corona, na badala yake, chanjo hiyo itaendelea kuwa ya hiari ya mtu binafsi.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa njia ya simu Januari 13, 2023, Waziri wa wizara hiyo Zanzibar, Nassor Ahmed Mazurui, alisema hakuna mtu yeyote, mwenye mamlaka ya kumlazimisha mwengine, kuchanja chanjo hiyo.

Alisema, bado kila mtu yuko huru ama kuamua kuchanja au kukataa kufanya hivyo, kwani suala la kinga ni la hiari ya mtu binafsi, na sio kumlazimisha kama ilivyozuka kwa baadhi ya madaktari kulalamikiwa.

Alisema bado msimamo wa wizara ya Afya, ni kuona chanjo hiyo inakuwa ya hiari, na wala hukuna daktari yeyote wala mfanyakazi wa wizara, mwenye nguvu na mamlaka ya kumlazimisha mtu kuchanja.

‘’Kama kuna daktari anawalazimisha watu kuchanja chanjo ya Corona, hilo ni kosa kisheria, maana bado msimamo wa serikali kuwa chanjo hiyo, ni hiari,’’alisema.

Hata hivyo Waziri huyo wa Afya wa Zanzibar Nassor Ahmed Mazurui, alisema atafuatilia kwa karibu katika hospitali zote za Unguja na Pemba, ili kujua kuna madaktari wamekuwa wakiwalazimisha wananchi kuchanja.

Katika hatua nyingine, Waziri huyo alisema, wanachopaswa kufanya madaktari na wahudumu wengine wa afya, ni kuwaelimisha wananchi, juu ya faida za chanjo hiyo.

‘’Lakini pia wanaweza kuwaeleza wananchi athari za mtu asiyechanja, aina za chanjo zilizokubaliwa, ipi unachoma mara moja na ipi mara mbili, lakini sio kuwalazimisha,’’alisema.

Hayo yamekuja hivi karibuni, baada ya baadhi ya wananchi kisiwani Pemba, kulalamikia tabia iliyozushwa, na baadhi ya madaktari, kuwalazimisha kuchoma chanjo ya Corona.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa masharti ya kutochapishwa majina yao walisema, kwa wanaokataa wamekuwa wakielezwa kuwa, wanaweza kukosa matibabu pindi watakapokwenda hospitalini.

Walisema wamekuwa, wakilalamika, kutokana na amri ya madaktari hao, ambao baadhi yao wamekuwa wakipita majumbani na kuwalazimisha kwenda kuchanja.



Wananchi wa shehia za Mwambe, Kengeja, Msingini Chake chake, Kwale, Ole, Micheweni, Wawi, Kiuyu Mbuyuni na Mtambwe wamesema, wamelazimishwa kuchanjwa, chanjo ya corona.

Vijana Omar Haji Khamis na mwenzake Nadia Issa Ali wa Kengeja, waliotaka majina yao yachapishwe, walisema juzi waliporudi kwenye safari zao, walikuta ujumbe unaowataka kufika hospitali kupata chanjo.

‘’Niliposema kuwa mimi siendi, tuliambiwa na waliotupa salamu, kuwa hata matatibabu mengine huwenda nayo tukayakosa,’’alisema Omar.

Kadika Mkubwa Mashiri na mwenzake Assa Khamis Mohamed wa Mtambwe walisema, wao waliwashuhudia madaktari wakipita nyumba hadi nyumba, sio tu kuwashawishi bali ni kuwalazimisha.

Akizungumza hivi karibuni, Afisa Mdhamini wizara ya Afya Pemba Khamis Bilali Ali, amerejea kauli yake, ya kuwaomba wananchi kupata chanjo hiyo, ili kujikinga na corona.

‘’Corona bado ipo, na zipo njia kadhaa za kujikinga na ugonjwa huo, ikiwa ni pamoja na chanjo, kunawa mikono kwa sabuni na maji tiririka kila baada ya muda na kuacha mikusanyiko isiyo ya msingi,’’alieleza.



Katika hatua nyingine Afisa Mdhamini huyo, alisema ambao hawastahiki kupata chanjo hiyo ni watoto waliochini ya miaka umri wa 18 na wale ambao sindano zinawadhuru pekee.

Mwezi Machi 11, 2020 Shirika la Afya Ulimwengini ‘WHO’ itangaaza kuwa ugonjwa Corona kuwa ni janga, la taifa hii ilitokana na kasi yake ya kuua na kusambaa.

Kisha WHO ikiwashauri wananchi kujiinga kwa kupata chanjo ambayo ni dawa ya kibaologia iliyokubaliwa na wataalamu wa afya, kwa lengo la kukinga, kujenga, ulinzi wa mwili na ugonjwa fulani husika kwa mujibu wa aina chanjo.

Hivi karibuni kituo cha Ulaya cha kudhibiti na kuzuwia magonjwa (ECDC) na ‘WHO’ wanakadiria kuwa watu 470,000 wenye umri wa zaidi ya miaka 60, wamenusurika kifo katika nchi 33 kote barani Ulaya, tangu chanjo hiyo ilipoanza kutolewa.

                      Mwisho

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch