Skip to main content

MAHAKIMU, WAENDESHA MASHTAKA: 'MSITULAUMU KESI ZINAPOFUTWA'

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA::

MAHAKIMU, waendesha mashtaka katika mahakama maalum ya kupmabana na ukatili na udhalilishaji kisiwani Pemba, wameiomba jamii kuacha kuwalaumu, pale kesi za aina hiyo, zinapofutwa au mtuhumiwa kuachiwa huru.

Walisema, wao yapofanyika matendo hayo huwa hawapo eneo la tukio, hivyo hawajui kinachoendelea, na ndio maana wanategemeo wao kuwaeleza, lakini kama hawafiki mahakamani kutoa ushahidi, na kesi kufutwa, wasiangushiwe lawama.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi kuelekea mwaka mpya wa mahakama 2023, walisema jamii ndio ambayo inategemewa mno, na mahakimu na waendesha mashataka, katika kufikia haki ya kweli.

Walieleza kuwa, wao wapo kuwasubiri wananchi kufika mahakamani kuto ushahidi, hivyo kama wanakataa wito wa mahakama, kitakachofuata ni mtuhumiwa kuachiwa huru.

Hakimu wa mahakama maalum ya kupambana na udhalilishaji mkoa wa kusini Pemba, Muumini Ali Juma, alisema kama jamii inajua namna wao wanavyokabiliana na wakati mgumu, ni kuwaonea huruma.

Alieleza kuwa, wao wanasubiri kuelezwa jinsi ubakaji au ulawiti ulivyotokea na kisha kuupima ushahidi, kabla ya mahakama, kufikia uamuzi wa kutoa hukumu.

‘’Wananchi wanatolewa wito wa mahakama ili waje mahakamani tushirikiane, katika kufikia haki, lakini chakushangaaza hawaji, sasa tuendelee kumshikilia mtuhumiwa hadi lini,’’alihoji.

Katika hatua nyingine, Hakimu huyo alisema, ili kila kesi ili ifikiwe kutolewa uamuzi wenye tija, ni kuhakikisha suala la kufika mahakamani kutoa ushahidi, lifanyike.



 Kwa upande wake Mwanasheria wa serikali Ali Amour Makame, alisema wazazi na walezi wamekuwa na hamu ya kukutana na vyombo vya sheria, mara watoto wao wanapodhalilishwa, ingawa baadae huvikimbia.

Alisema wanazo kesi kadhaa wazazi wamekuwa wakipokea wito wa mahakama, lakini bila ya sababu za msingi huamua, kutodhuhuria mahakamani.

‘’Ni kweli, hata sisi waendesha mashataka wakati mwengine ndio tunaongoza katika kuiharakisha mahakama kuziondoa au kuwaachia huru watuhumiwa, kwa vile mashahidi muhimu hawafiki mahakamani,’’alieleza.

Alieleza kuwa, wengine wanaofika mahakamani kwa makusudi huwakana watuhumiwa, ambao awali waliwataja wakati wanahojiwa vituo vya Polisi, kuwa ndio waliodhalilisha.

‘’Zipo sababu nyingi, moja wapo ni rushwa muhali, wengine hasa kwa kesi za watoto wa miaka 16 hadi 17 ni kuzifanyia sulhu, ili kukimbia adhabu,’’alieleza.

Aidha wakili huyo alisema, hata mwishoni mwa mwaka jana, mahakama maalum ya kupambana na makosa ya udhalilishaji ya mkoa kusini Pemba, ilimuachia huru daktari Hassan Said Mohamed miaka (38) wa hospitali ya Chake chake, baada ya mtoto wa aliyedai kubakwa mara tatu, kumkana daktari huyo mahakamani.

Aidha wakili wa utetezi, Massoud Mohamd Said, katika shauri la kuingilia kinyume na maumbile, aliiomba mahakama maalum ya kupambana na makosa ya udhalilishaji, kuliondosha shtaka hilo, kutokana na upande wa mashataka, kushindwa kuwasilisha mashahidi.



 Hata hivyo mahakama hiyo pia, mwezi August mwaka jana ilimuachia huru mtuhumiwa mwengine wa kosa ka ubakaji, baada ya shahidi nambari moja (mtoto wa miaka 13), aliyedai kubakwa, kushindwa kufika mahakamani kutoa ushahidi, licha kuitwa na mahkama mara saba.

Kwa upande wake Naibu Mrajisi mahakama kuu kanda ya Pemba Faraji Shomari Juma, amesema mahakama itahakikisha sasa, inawapatia nauli zao mashahidi wanaofika mahakamani, ili kusiwe na mkwamo wa kesi, hasa za udhalilishaji..

                     Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch