Skip to main content

IPA: 'WATUMISHI WA UMMA TUMIENI LUGHA MWANANA KWA WANANCHI'

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA:::

WATUMISHI wa umma kisiwani Pemba, wametakiwa kutumia lugha laini, zenye mvuto, shirikishi na zenye heshima wakati wanapowahudumia wananchi wanaofika kwenye tasisi hizo kudai huduma.

Hayo yameelezwa na Mkuu wa Chuo cha Utawala wa Umma ‘IPA’ tawi la Pemba Juma Haji Juma, wakati akizungumza na watumishi wa baraza la mji Chake chake, wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo pamoja na wa wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi, kwenye mafunzo ya sehemu ya uthibitisho wa kazini, yaliofanyika ukumbi wa Baraza la mji Chake chake.

Alisema, moja ya msingi mkuu kwa watumishi wa umma, wakati wanapowahudumia wananchi, ni matumizi ya lugha sahihi na zenye ushawishi wa kupokea na kutoa huduma.



Alisema, wapokea huduma huwa wanahitaji kusikilizwa, kushauriwa, kufafanuliwa na wakati mwengine kuelezwa jambo lilipofikia, ambapo mchakato wote huo, matumizi ya lugha nzuri ni jambo la kuzingatia.

‘’Niwakumbushe watumishi wenzangu wa umma kuwa, suala la kutumia lugha isiyorafiki kwenye maeneo yetu ya kazi, haijengi bali inabomoa, lazima tutumie lugha za mvuto, zenye heshima na nidhamu, na hayo ndio maadili mema,’’alieleza.

Katika hatua nyingine, Mkuu huyo wa IPA tawi la Pemba, aliwasisitiza watumishi hao, kuwa makini kwenye mafunzo, ambayo ni sehemu ya uthibitisho wa kazi, baada ya ajira.

Akifungua mafunzo hayo, Afisa Utumishi wa Baraza la mji wa Chake chake Abdalla Salim Abdalla, aliwaeleze watumishi hao kuwa, wanawajibu wa kuzisoma na kuzijua sheria na kanuni za utumishi wa umma.



Alisema, mara mtumishi anapoajiriwa haraka sana, anatakiwa kuzitafuta na kuzisoma sheria zinazomuongoza, ili kujua haki na wajibu wake kazini.

‘’Kama wenzetu wa IPA wakishirikiana na wizara zetu, imeamua kuwakusanya na kuwapa elimu hii, ni jambo jema, na sasa ni wajibu wenu muwe makini wakati wakufunzi wanawafundisha,’’alieleza.

Katika hatua nyinge, Afisa huyo Utumishi wa Baraza la mji wa Chake chake Abdalla Salim Abdalla, alisema mtumishi wa umma lazima aelewe kuwa, anaiwakilisha serikali kuu kwenye utendaji wake.



Hata hivyo amesema, mtumishi asipoweka mbele maslahi ya tasisi yake na kuangalia zaidi mashali binafsi, anaweza kuzalisha changamoto zisizo za lazima.

Akiwasilisha mada ya utekelezaji wa program ya utumishi wa umma, mkufunzi kutoka ‘IPA’ Abubakar Nuhu, alisema ina lengo la kuleta ufanisi, sehemu za kazi.



Alisema program hiyo, ipo kwa mujibu wa sheria na kanuni za utumishi wa umma, hivyo ni wajibu kwa kila mtumisha na kwa nafasi yake, kufanya juhudi za kuhakikisha inaleta ufanisi.

Hata hivyo mkufunzi huyo, amewataka watumishia hao, kuzilinda nyaraka za ofisi zao, kwani ndio roho ya kila tasisi na kinyume chake, ni kutoa siri za serikali.

Kwa upande wake mkufunzi Khamis Nassor Salim, akiwasilisha mada ya uzalendo na umuhimu wake kwa taifa, alisema ni jambo ambalo, linatakiwa kuwa ndani ya moyo wa mtumishi mwenyewe.



‘’Hili suala la uzalendo, linakwenda sambamba na imani na huruma zaidi, sasa hapa tunasomeshana lakini kila mmoja atajipima mwenyewe, kama yuko chini kiuzalendo azidishe, kwani ni chachu ya kufikia maendeleo ya kweli.



Katika mafunzo hayo ya siku tatu, mada 10 zitawasilishwa ikiwa ni pamoja na rushwa na athari zake, huduma za ZSSF, uzalendo, sheria na kanuni za utumishi wa umma, afya na usalama kazini na maadili ya utumishi wa umma.

                    Mwisho        

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch