Skip to main content

TAKWIMU ZA WAJUMBE WANAWAKE KAMATI ZA MASHEHA WANAUME WETE PEMBA ZARIDHISHA

 




 

NA HAJI NASSOR, PEMBA::

‘’Kamati yangu inawajumbe tisa, saba ni wanawake sawa na asilimia 77.77 na wawili ni wanaume wakiwa asilimia 22.22, na kazi zangu zinafanikiwa ,’’ndio maneno ya mwanzo ya sheha wa shehia ya Jadida Wete, Juma Ali Juma.

 

Awali alikuwa na kamati ya wajumbe 12, wanawake wakiwa wawili na wanaume 10, ingawa kuanzia mwaka 2020, aliivunja kamati hiyo baada ya kuona maagizo anayoyatoa, hayafanikiwi.

 

Mwaka 2019, alihudhuria mkutano wa ulioandaliwa na Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA- Zanzibar, Gombani Chake chake, na kuelezwa kua wanawake wana haki sawa ya kuongoza kama walivyo wanaume.

 

‘’Mimi dhana hiyo niliijaribu kwenye shehia yangu, na kweli sasa wanawake ndio ninaowategemea pale ninapotoa maagizo kwa ajili ya kuwafikishia wananachi,’’anasema.

 

Anasema, hawajahi kushindwa kwenye shehia yake, kwa kuwa na idadi kubwa ya wajumbe wanawake, na anafikiria kuwapunguza tena idadi ya wajumbe wanaume.

 

‘Wajumbe wanaume wazito kufika kwa muda kwenye vikao na mikutano, pili fedha wameweka kipaumbele, lakini hata unapowapa kazi, nao huwapa watu wengine wazifanye, lakini kwa wanawake ni tofauti,’’anasema.

 

Kumbe sio shehia ya Jadida pekee, ambako masheha wanaume wanawaamini wajumbe wanawake, hata shehia ya Mtemani ina wajumbe 13, wanawake ni tisa, sawa asilimia 63.23 na wanaume wanne wakiwa asilimia 30.76.

 

Sheha wa shehia hiyo Mrisho Juma Mtwana, alisema sababu ya kuongeza idadi ya wanawake, ni baada ya kuona shehia ya Jadida inafanikiwa kikazi.

 

‘’Nilimfuata sheha mwenzangu wa Jadida, nikamuuliza siri ya mafanikio, kwa mfano kupata watu wengi kwenye mikutano ya jioni, akaniambia ni kuwapunguza wajumbe wanaume,’’anasema.

 

Sasa kuanzia mwanzoni mwaka 2021, aliamua kwanza kupunguza wajumbe kutoka 15 wa zamani, na kuwa na wajumbe 13 na wanawake kuwaweka tisa (9).

Tokea afanye mabadiliko hayo, kuanzia sasa anafurahia utendaji wa kazi, na hasa anafurahishwa zaidi, anapokuwa na mikutano ya nyakati ya jioni, jinsi wajumbe wake wanawake wanavyotumia mbinu ya kukusanya wananchi.

 

‘’Kama kuna sheha anamatatizo kwenye shehia yake, aangalie uwezekano wa kuwaweka wajumbe wengi wanawake kwenye kamati, kama hana tatizo binfsi, anaweza kufanikwa kama nilivyo mimi,’’anasema.

 

WAJUMBE WA SHEHIA HIZO

Wanasema, kamati ya sheha yenye wajumbe wengi wanaume imekuwa ikikosa ufanisi, kutokana na kuwaburuza wanawake, hata kwa jambo lililo wazi.

 

Asha Mussa Idd na mwenzake Maimuna Ali Khamis wajumbe wa kamati ya shehia ya Jadida, wanasema licha ya kuwa sheha wao ni mwanamme, lakini wamefanikiwa kwa kiwango kikubwa.

 

‘’Kwa mfano suala la utoro kwa wanafunzi, tulizungumza na wanawake wenzetu kwa kutumia maneno yetu, walitifahamu na kwa mwaka 2022 pekee wanafunzi 13 walirudishwa skuli,’’wanasema.

 

Lakini hata wajumbe wa kamati ya shehia ya Mtemani Sauda Issa Haji na Asha Issa Ali, wanasema sheha amekuwa akiwaamini kutokana na kujituma kwao.

 


‘’Sisi sheha akitupa kazi huwa hailali, maana tunajiuliza, kwa nini wameachwa wanaume tena walio na elimu, nafasi hii tukapewa sisi, inabidi tufanye kazi kwa bidii,’’wanasema.

 

Lakini mjumbe wa kamati hiyo, Ali Makame Mkubwa anasema, pamoja na na kuwa idadi ya wajumbe wanawake ni kubwa, lakini inamamtiki katika utendaji wa kazi zao.

 

WANANCHI WA SHEHIA HIZO

Khadija Ussi Haji na mwenzake Asiya Sharif Hassan wa shehia ya Jadida na wenzao wa shehia za Mtemani, Nussra Mohamed Omar na Mtumwa Ilayas Kombo, walisema kamati zao sasa ziko hai.

 

‘’Inafurahisha, kwa mfano tunapokuwa na kazi ya usafi wa shehia, hawa wajumbe wa shehia zetu ambao wengi ni wanawake, huwa ndio wa mwanzo, sasa na sisi tunahamasika,’’wanasema.

 

Wanasema kama kuna tasisi mfano Chama cha Waandishi wa habari Wanawake Tanzania -TAMWA Zanzibar ndicho kilichowaelimisha masheha wao, na sasa kuwa na kamati zilizohai, baada ya kuingia wanawake kwa asilimia kubwa.

 

‘’Kumbe wanawake wanaweza, sasa lazima kuwa na sheria hasa iwalazimishe masheha kuwa wajumbe wawe sawa sawa baina ya wanawake na wanaume, maana faida inaonekana,’’wanashauri.

 

HALI HALISI YA WILAYA YA WETE KWA WAJUMBE WANAWAKE

Wilaya ya Wete, bado hali hairidhishi sana, maana baina ya wajumbe wote 359 kutoka shehia 36 wilayani humo, wajumbe wanawake 132 sawa na asilimia 36.76 na wanaume wakiwa ni 227, kwa asilimia 63.23.   

 

Hili linaweza kuchangiwa kwa karibu, na uhaba wa masheha wanawake wilayan humo, kwani wapo 10 tu sawa na asilimia 27.77 na wanaume wakiwa 26 sawa na asilimia 72.22.

 

MASHEHA WANAWAKE WILAYA YA WETE

Sheha wa shehia ya Mtambwe Kaskazini, Shufaa Asaa Muombwa, alisema anao wajumbe 11, lakini wote ni wanaume.

 

‘’Mara tatu nimeshateua wajumbe saba wanawake, lakini wanazuiliwa na waume wao, na wengine hutishwa na wananchi,’’alisema.

 


Na ndio maana kuanzia mwaka 2021 mwishoni, aliamua kuwa na wajumbe 11, sawa na asilimia 100, kuwa wote ni wanaume, ingawa anasema anangalia namna na kuwa na wanawake hapo baadae.

 

‘’Napata shida ninapo wapa maagizo hawa wajumbe wangu, huwa wazito wazito kuyatekeleza, inabidi wakati mwengine niingie na mimi, lakini kama wanawake wakiondolewa vikwazo, ntafanikiwa,’’anasema.

 

Sheha wa shehia Bopwe Ramia Said Rashid, alisema kamati yake imeshirikisha wajumbe tisa (9), wanawake wakiwa watano sawa na asilimia 55.55 na wanaume ni wanne sawa na asilimia 44.44.

 

‘’Mimi nna nia ya kupunguza idadi ya wajumbe wanaume na kuongeza ufanisi, maana zipo shehia kama za Mtemani na Jadida zinakwenda vizuri,’’alisema sheha.

 

WANAHARAKATI WALISEMAJE?

Mwanaharakati wa haki za wanawake na watoto Tatu Abdalla Mselleh, alisema idadi kuwa ndogo ya wajumbe wanawake kwenye kamati za masheha, hakun uhusiano na uchache wa masheha wanawake.

 

‘’Wivu wa kupindukia, masheha kutowaamini wanawake, au mfumo wa utamaduni unaweza kuwa kichocheo kikubwa kwa wanawake kutopewa nafasi hizo au kuzikataa,’’alisema.

 

Mratibu wa TAMWA Pemba Fat-hya Mussa Said, alisema wapo wanawake hupewa nafasi ya ujumbe wa sheha, lakini kutokana na vikwazo wanavyowekewa, huzikataa nafasi hizo.

 

‘’Kwa mfano mwanzoni mwa mwaka 2022 yupo mwanamke alipewa nafasi ya usheha, lakini kwa vikwazo vya muume aliusamehe, sasa mfano kama huu, huwakumba hata wajumbe wanawake wa kamati,’’alisema .

 

Sifuni Ali Haji kutoka Jumuiya mwevuli ya asasi za kiraia Pemba ‘PACSO’ alisema bado wapo baadhi ya wanaume, wamekuwa wakitumia vitisho, kwa wanawake na kuogopa kupewa uongozi.

 

‘’Hata ukija kwenye vyama, ukiweka nia ya kugombea kama ubunge au uwakilishi, umeanza kujitengenezea adui, hivyo hata huko kwenye wajumbe wa shehia, wanawake wanasumbuliwa,’’anasema.

 


Mohamed Hassan Ali, Mwenyekiti wa jumuiya za asasi za kiraia mkoa wa kaskazini Pemba, alisema bado baadhi ya viongozi wanaume, hawajawaamini wanawake.

 

‘’Kwa mfano wilaya ya Wete ina shehia 36, lakini masheha wanawake ni 10, kwanini hapa isiwe idadi sawa,  na Mkuu wa mkoa na katibu tawala wilaya wote wanawake,’’alihoji.

 

VIONGOZI WA SERIKALI

Mkuu wa wilaya ya Wete Dk. Hamad Omar Bakari, alisema masheha hawafungiki na idadi ya wajumbe wa shehia, kutokana na ukubwa wa shehia zao.

 

‘’Sisi hataka kama watawachagua wanawake wote, hakuna tatizo muhimu mambo yaende, kama ambayo maagizo yanakuja kila siku, maana wananchi wanachotaka ni kutekelezewa shida zao,’’anasema.

 

Mkuu wa mkoa wa kaskazini Pemba, Salama Mbarouk Khatib, anasema kubwa ni kuhakikisha wanawake wanapewa nafasi na kisha kuzitendea haki.

 


Akizungumza kwenye kongamano la kutimiza miaka miwili lililofanyika ukumbi wa zamani wa baraza la wawakilishi Wete, Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi, alisema mawaziri wanawake wameongoza kwa kufanya vizuri.

 

‘’Na kwa siku sijazo nitaongeza idadi yao, katika nafasi mbali mbali za uongozi iwe mawaziri, makatibu wakuu, wakuu wa wilaya na mkoa,’’anasema.

 

Dk. Mwinyi kwa sasa, alimteuwa Katibu mkuu kiongozi mwanake kwa mara ya kwanza, tokea Zanzibar ilipofanya Mapinduzi miaka 59 iliyopita.

 

KATIBA

Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 ndani ya kifungu cha 21 (1) kimeeleza wazi wazi kwamba, kila mzanzibari anayohaki ya kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi.

 

Kifugu hicho kikazidi kufafanua kuwa iwe ni moja kwa moja au kupitia wawakilishi waliochaguliwa kwa hiari, sasa je mbona wanawake wamekua wakikoseshwa haki hii.

 

Maana leo hii wanawake wamkuwa waimbaji vigelele gele wakubwa na kuimba nyimbo mwanana kwenye vyama vyao vya siasa,  mbona wamekuwa wakikwazwa wanapotaka kuchukua fomu na kugombea nafasi za majimboni.

 

Ndani ya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, kwenye Ibara ya 21, nayo imeeleza haki ya kila mtanzania kushiriki kwenye shughuli za utawala, na pia suala la kuchagua na kuchaguliwa.

 

Hapa utaona kwamba, wanachama wa vyama vya siasa wamekuwa wakiwang’ng’ania wanaume kama vile kuna kifungu ndani ya katiba za vyama vyao au ya nchi inayowalazimisha hivyo.

 




ATHARI YAKE

Mwanaharakati wa haki za wanaweke, Dina Juma Makota kutoka Jumuiya ya PEGAO wanaotekeza mradi wa miaka minne wa kuwajengea uwezo wanawake kuadai haki, zao anasema ni kukosa kujiwakilisha.

 

Ali Khamis Juma mwenye ulemavu wa viungo, anasema kama wanawake hawamo kwenye kamati za shehia, shughuli za kimaendeleo, zinaweza kuzorota kwa kiwango kikubwa.

 

Sheha wa shehia ya Pembeni Saumu Ali Hamad, anasema wao hushindwa kuyatekeleza maagizo ya wilayani, kwani baadhi ya maeneo, wanaume hawafiki kutoa taarifa.

 

Mjumbe wa kamati ya shehia ya Gando, Hamisa Iddi Kassim anasema, na masheha wanaweza kushindwa kazi, maana suati yao inaumuhimu wake kwenye vikao.

 

Mwanafunzi Hassan Khatib Nassor wa Utaani, anasema kama shehia inataka iporomoke kiutendaji, isiwashirikishe wanawake kwenye kamati za shehia.

 

NINI KIFANYIKE  

Masheha wanasema, ili idadi ya wajumbe wanawake iongezeke kutoka ya sasa 132, kati ya wajumbe 359, elimu inahitajika kwa wenye mamlaka.

 

Masheha wanawake, wamesema kama wanaume watawafungulia minyororo wanawake na kuwaamini, idadi ya wajumbe wakamati za masheha itaongezeka.

 

Wajumbe wa shehia wanasema kama shehia nyingine zitajenga utamaduni wa kuzitembelea shehia zilizofanikiwa, idadi ya wajumbe wanawake itakua.

 

Mratibu wa TAMWA anasema wanawake waliojengewa uwezo na kupata nafasi, wazitumie kwa moyo mmoja thabiti nafasi zao, ili kuwatia moyo na ari, wenye mamlaka ya kuteua.

 

Mkuu wa wilaya ya Micheweni Mgeni Katib Yahya, anasema masheha waamue kuwatea wajumbe wanawake, wale wenye uwezo, ili wengine waige.

 

                    mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch