Skip to main content

VIJANA WALIVYOPIGA HATUA KIMAENDELEO, SERIKALI YAWAPIGA MBELEKO

 




NA HANIFA SALIM, PEMBA::

’KIJANA ni mtu yeyote mwenye umri wa miaka 15 hadi miaka 35,’’ndivyo sera na sheria ya vijana Zanzibar inavyofafanua.

Lakini kwa upande mwengine kijana ametafsiriwa kuwa ni mwanamke au mwanamme yeyote mwenye miaka katia ya 15 hadi 24, kama sera ya taifa ya Maendeleo na vijana ya mwaka 1996, na kama ilivyorekebishwa mwaka 2007.

 Kijana ni mtu muhimu kwa taifa lolote ulimwenguni, kwani ndio nguvu kazi ya taifa, ndio taifa la kesho kama wasemavyo baadhi yao.

Lakini kijana ndio tumaini la taifa na ndio mtu anayetazamiwa kwa mapana ya nchi, katika kuongoza, kukuza uchumi na kuzima majaribio ya kihalifu.

Vijana wanakumbana na changamoto mbali mbali katika maisha yao, na mwisho wa siku taifa linamchukulia kama mtu aliyeshindwa na asiye na msaada wowote kwa taifa lake.

Lakini katika umri huo wa ujana, inampasa kijana kujitambua ili aweze kuwa na muonekano halisi, sio kwa umri tu bali matendo zaidi.

Ni lazima awe na ushawishi katika masuala muhimu na kwa manufaa ya jamii kwa ujumla, hasa kwa vijana wenzake, katika kushawishi ndio tunaona nguvu ya kijana na kuanza kutengeneza taifa imara.

Hata serikalini, vijana wengi wameaminiwa na kuonesha ushawishi mkubwa, kuwa wana uwezo wa kufanya kazi kwa kuaminiwa na pale wanapopewa nafasi za uongozi.

Serikali imeahidi kuendelea kuweka mazingira bora ya kuwawezesha vijana, kuzitumia fursa zinazopatikana katika sekta ya uchumi wa buluu, kuibua fursa za ajira na kuwainua kiuchumi.

 

Serikali ya awamu ya nane, inathamini juhudi mbali mbali zinazofanywa na vijana, hivyo ipo tayari kuendelea kuwashirikisha katika kuzitumia fursa zitakazosaidia kuwainua kiuchumi.

 

IDARA YA MAENDELEO YA VIJANA

Idara ya maendeleo ya vijana, ni miongoni mwa taasisi za serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, iliyoanzishwa mwaka 1992 kwa lengo la kuratibu na kusimamia maendeleo ya vijana Zanzibar.

Idara hii inatekeleza kazi zake kwa mujibu wa sera ya maendeleo ya vijana Zanzibar, mipango na miongozo ya Serikali.

Dhamira yake ni kukuza ustawi na maendeleo ya vijana, kuwajengea mazingira mazuri na endelevu yatakayowawezesha kushiriki kikamilifu katika sekta za kiuchumi, kijamii na kisiasa.

Mkurugenzi wa Idara hiyo Zanzibar Shaibu Ibrahim Mohamed anasema, juhudi mbali mbali zinachukuliwa na serikali kuhakikisha shughuli za vijana vinatekelezwa.

 


Kupitia Idara yao, imekua ikifanya vikao vya pamoja na wadau wa maendeleo ya vijana, kwa kila robo ya tatu kuwasilisha taarifa na mpango wa utekelezaji juu ya masuala yanayowahusu vijana.

 

"Vikao hivyo pia tunapata kujua changamoto na tunapashana habari mpya, zilizopo katika sekta ya vijana, kwani kuna miradi mingi ambayo inaibuka siku hadi siku,’’anasema.

 

 Akitaja malengo ya Idara hiyo moja wapo ni kuandaa, kusimamia na kuratibu utekelezaji wa sera, mipango ya maendeleo nchini.

 

Jengine ni kuimarisha ushiriki na ushirikishwaji wa vijana katika nyanja za kiuchumi na kijamii, ili wawe mfano bora wa taifa lao.

 

Kuratibu taasisi na asasi za maendeleo ya vijana Zanzibar, kusimamia mipango ya malezi na makuzi ya vijana na kuimarisha ushirikiano, baina ya taasisi za vijana ndani na nje ya nchi.

‘’Jengine ni kuhakikisha masuala ya vijana yanazingatiwa na kuingizwa katika sera, mipango, miradi ya kitaifa, na kusimamia mipango ya uwezeshaji wa vijana kiuchumi,’’anafafanua.

OFISI YA RAIS KAZI, UCHUMI NA UWEKEZAJI

Mratibu wa Idara ya Ajira Pemba Said Salum Othman anasema, idara yao, inatekeleza mipango maalumu ya kuhakikisha vijana wanawapatia mafunzo ya ujuzi.

 

“Mafunzo haya ni ya miezi sita kwa vijana wa rika tofauti kuanzia miaka 15 hadi 24 kwa wenye elimu ya msingi, sekondari na ambao hawana elimu kabisa, ili kuhakikisha vijana wanapatiwa fursa na kuweza kujiajiri na kuajirika,” anasema.

 

Mafunzo hayo ya ujuzi yanatolewa, na mwaka jana wilaya ya Wete walichukuliwa vijana wawili, Chake watatu, Mkoani wawili na Micheweni wawili kupelekwa Unguja kwa ajili ya kusoma utalii.

 

“Mwezi Novemba mwaka 2021, tulichukua vijana wa wilaya ya Wete, tunawaangalia ambao wanafaa kwa mchujo maalumu badala yake, tunawapeleka katika vyuo maalumu vya mafunzo ya ujuzi wa kujiajiri au kuajirika,” anasema.

 

Mwaka huu mwezi Machi walichukuliwa vijana wengine kwa ajili ya kupatiwa mafunzo ya kutengeneza mafriji, viyoyozi, ushoni pamoja na uchongaji.

 


Ambapo walichukuw avijana 28 sawa na kila wilaya vijana saba kati ya Wilaya nne zilizopo Pemba, wenye jinsia tofauti na uwezo usiolingana.

 

Hivyo sasa inafahamika kuwa, vijana 339 wa wilaya ya Chake chake, wamenufaika wakiwemo wanawake 14 na wanaume 325 na ajira kupitia kampuni za ujenzi wa miradi saba ya ahuweni wa COVID 19.

 

Mkoani jumla ya vijana 117 wakiwemo wanaume 72 na wanawake 45, huku Wete ikiwa na vijana 158 wanaume 141 na wanawake 17 na Micheweni vijana 772 wanaume 688 na wanawake 84 kupitia miradi hiyo.

 

Afisa TEHAMA kutoka mfuko wa uwezeshaji wananchi kiuchumi Pemba, Farid Hamuni Juma, anasema serikali ya awamu ya nane, imetenga zaidi ya shilingi bilioni 80 kwa ajili ya kuwawezesha wajasiriamali.

 

Ambapo tayari kwa kisiwa cha Pemba pekee, zimeshatolewa zaidi ya bilioni 2 kwa vikundi 228.

 


“Kati ya bilioni 2 hizo, wilaya ya Chake kuna vikundi 58 vimepatiwa zaidi ya shilingi milioni 500 na wilaya ya Mkoani vikundi 94, vyenyewe vimepatiwa zaidi ya shilingi milioni 700,’’anaeleza.

 

Lakini hata wilaya ya Wete nako kuna vikundi 38, vimeshapatiwa zaidi ya shilingi milioni 300 na wilaya ya Micheweni ina vikundi 38 vilivopatiwa zaidi ya shilingi milioni 400.

 

Anasema, kati ya bilioni hizo 80 kuna mgawanyiko ambao umewekwa asilimia 45 ni vijana, asilimia 35 ni wanawake, asilimia 12 watu wenye mahitaji maalumu, huku asilimu 5 wakiwa ni wastaafu na asilimia 3 watu ambao wameachana na dawa ya kulevya.

 

WIZARA YA UCHUMI WA BULUU NA UVUVI

 

Ali Rashid Hamad, kutoka ziara hiyo Pemba anasema, jamii bado uwelewa wa jamii kuhusu masuala ya uchumi wa buluu  uko chini, hivyo wameona kuna haja ya kutoa elimu ili wafahamu.

 

“Tumetoa elimu hii ya uchumi wa buluu katika shehia 25 za Pemba na ndani yake asilimia 48 ya tuliowafikia ni vijana, tumetoa mafunzo ya kusarifu wa mwani kati ya hao vijana walikua 26 na kutoa vifaa vya uvuvi ambapo wanufaika walikua 16 kati ya hao asilimia 60 ni vijana,” anaeleza.

 

Wizara ilitoa mafunzo ya ufugaji wa majongoo bahari, ambapo waliwafikia watu 80 asilimia 50 kati ya hao walikua ni vijana na baada ya kuwapa mafunzo waliwajengea vizimba vitano vya kufugia.

 

“Lazima tuwajengee mabanda maalumu kwa kushirikiana na watu wa ‘FIO’ tayari wameshatenga zaidi ya shilingi milioni 120 kwa ajili ya banda la kukaushia mwani kwa wakulima wetu wakiwemo vijana,” anasema.

 

Anasema, sasa hivi kuna zaidi ya shilingi bilioni 49 ambazo zimepangwa kutolewa kwa kukopeshwa wanufaika wakiwemo wavuvi, wafugaji wa mazao ya baharini, wakulima wa mwani wakiwemo vijana.

 

IDARA YA KILIMO

 

Afisa Kilimo Wilaya ya Chake chake Rashid Mohamed Wema, anasema idara hiyo inafanya kazi kwa kushirikiana na shirika la kilimo ulimwenguni ‘FAO’.

 

Ambalo limewawezesha vijana 23 wa vikundi viwili vya ushika kwa wilaya ya Wete na Mkoani.

 

“Katika mradi wa ‘CFP’ ambao mabwana shamba wetu wameshirikiana kwenye kilimo cha mboga mboga na matunda kwa Wete vijana 184 wamewezeshwa kupitia vikundi 12.

 

Wilaya ya Chake vijana 195 wamewezeshwa kupitia mradi huo kwa kupatiwa taaluma pembejeo, mbegu na mbolea, Mkoani vijana 133 wamewezeshwa kupitia vikundi 13 na Micheweni vijana 21.

 

WIZARA YA UTALII NA MAMBO YA KALE

 

Afisa Utalii na Mambo ya Kale Pemba, Hafidh Omar Masoud anasema, wizara yao inapitia hatua mbali mbali katika kuwawezesha vijana.

 

Kwa mwaka huu wa fedha, wizara imekua ikitoa elimu bure kwa vijana ambayo inahusisha madarasa ya vijana yanayohusiana na utalii na lugha za kigeni.

 

“Tunatoa elimu hii kupitia mikoa yote miwili ya Pemba kwa upande wa kusini tuna wanafunzi 35 wakiwemo wanawake 10 na wanaume 20 na kaskazini ni wanafunzi zaidi ya 50 wa darasa la elimu ya kigeni,” anasema.

 


Anasema, katika fursa zilizopo nyingi kwa vijana ni za kiutalii ndani ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar za kuajiriwa na kujiajiri wenyewe ikiwemo kuongoza wageni  au kuwa mwalimu wa lugha.

 

MAMLAKA YA MAFUNZO YA AMALI

 

Mwalimu Mkuu wa chuo cha mafunzo ya amali Vitongoji Juma Mussa Ali anasema kwa mwaka 2020, jumla ya wanafunzi 580 walipatiwa mafunzo ya ufundi, kupitia fani za uchongaji, ushoni na uchomaji wa mageti ‘uashi’.

 

Mwaka 2021/2022 walipata vijana 400 wa kike, ambao walijiunga na masuala ya upandaji na usarifu wa mwani, ambao walijitolea kuitumia fursa ya kilimo hicho.

 

 Anasema, katika lengo la kuwaendeleza vijana mamlaka imeandaa mpango wa kutoa mafunzo kwa vijana watakaotoa huduma za kiufundi kwenye hoteli na sehemu nyengine za nje ya nchi kupitia fani ya umeme, mafriji, viyoyozi na mafundi bomba.

 

BARAZA LA VIJANA

Fahim Abdalla ni Mwenyekiti wa Baraza la Vijana wilaya ya Chake chake, amepongeza kwa jitihada zake za kuwaunga mkono vijana, kupitia nyanja mbali mbali.

 

Anaona kazi iliyoko mbele yao sasa kwa vijana ni kukaza buti, ili fedha na miradi iliyopo kwa ajili yao ifikie lengo la kujiongezea kipato.

 

                                            MWISHO.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch