Skip to main content

MDHAMINI ELIMU PEMBA, AWAONESHA NJIA WAALIMU KUFIKA MBALI

 







NA HAJI NASSOR, PEMBA

WAALIMU wa skuli za msingi na sekondari kisiwani Pemba, wametakiwa kuongeza uadilifu, uaminifu, heshima na uzalendo wanapokuwa kazini, ili ufanisi na tija ipatikane.

 

Kauli hiyo imetolewa leo Disemba 19, 2022 na Afisa Mdhamini wizara ya elimu na mafunzo ya amali kisiwani humo Mohamed Nassor Salim, wakati alipokuwa akiyafungua mafunzo ya siku mbili, kwa waalimu hao, yenye lengo la kuthibitishwa kazi.

 

Alisema, kazi wanayofanya ni kubwa, na inakuwa na tija kwa taifa, na hasa ikiwa wataongeza kasi ya ufundishaji, uadilifu na kuweka mbele uzalendo kwa taifa.

 

Alieleza kuwa, kila jambo mtu analolifanya lazima afikirie namna ya kuweka uzalendo mbele, na akitia na uadilifu anaweza kufanikisha malengo yake.

 

‘’Leo (jana) mafunzo haya ni ishara kua, nyinyi ndio chaguo la jamii, kuwatumia katika fani ya ualimu, sasa lazima muongeza uaminifu, ujasiri, uadilifu na uzalendo, ili wanafunzi wakifie lengo husika,’’alieleza.

 


Katika hatua nyingine Afisa Mdhamini huyo, aliwataka waalimu hao kuongeza elimu na kundoka walipo, ili wewe na uweledi wa kulitumikia taifa lao.

 

‘’Taifa linahitaji waalimu wenye weledi, ili wafundishe wanafunzi kwa ufanisi zaidi, sasa ili kufikia hilo, lazima kila mmoja, aongeze elimu na kufikia ya juu zaidi,’’alieleza.

 

Hata hivyo, alisema mpango huo wa mafunzo ya uthibitishaji kazini, utakuwa endelevu kwa wafanyakazi wote wa wizara ya elimu na mafunzo ya amali.

 

Akiwasilisha mada ya uzalendo, muwezeshaji kutoka Chuo cha Utawala wa Umma ‘IPA’ kisiwani Pemba Khamis Nassor, alisema uzalendo, ni vyema ukaanzia ngazi ya familia.

 

Alisema, kisha upande kwenye ngazi ya kijiji, wilaya, mkoa na taifa kwa ujumla, kufanya shuhguli mbali mbali za kitaifa, kwa lengo la kuendeleza mbele taifa.

 

Alifahamisha kuwa, sifa moja ya mzalendo ni kutii sheria za nchi bila ya shuruti, kuogopa rushwa, kuwa na lugha nzuri kwa viongozi, heshima na nidhamu kwa kila mmoja.

 

Muwezeshaji huyo alieleza kuwa, eneo jengine la kuendeleza uzalendo, ni jamii kutekeleza maagizo ya viongozi, mfano suala la kudai risiti za kielektroniki, baada ya kununua.

 


‘’Waalimu, uzalendo hata mnapokuwa kwenye shughuli zenu za ufundishaji upo, mfano unapotumia vifaa vya skuli vibaya mfano chaki au mabuku utakuwa hamna uzalendo,’’alifafanua.

 

Katika hatua nyingine, muwezeshaji huyo, aliwataka waalimu hao, elimu waliyoipata kuhakikisha wanawafikishia na wengine, ili wajae uzalendo.

 


Nae Kaimu Mratibu wa Idara ya Uendeshaji na Utumishi ‘MIUU’ wa wizara ya elimu na mafunzo ya amali Pemba, Harith Bakar Waziri, alisema katika zoezi hilo watumushi 1,417 watafikiwa na elimu hiyo.

 

‘’Mafunzo haya yenye lengo la uthibitishaji wa kazini kwa watumishi wa wizara wakiwemo waalimu, tutahakikisha hakuna atakayebakia,’’alisema.

 

Wakati huo huo, Mkuu wa Idara ya Mafunzo kutoka ‘IPA’ Pemba Abubakar Nuhu, alisema utekelezaji wa program ya mageuzi ya utumishi wa umma, yanawalenga watumishi wote.

 

Alieleza kuwa, program hiyo, inakusudia kuona kila mtumishi anatekeleza wajibu wake kwa ufanisi, ili wananchi wanapofuata huduma iwe rahisi kwao.

 



‘’Mpango huu unataka kuona mambo kadhaa ikiwa ni pamoja na mabadiliko ya utoaji huduma kwa watumishi mkiwemo nyinyi waalimu, pamoja na kufikiria uimarishaji wa miundo ya kazi,’’alifafanua.

 

Katika mafunzo hayo, ya siku mbili mada saba zitajadiliwa ikiwa ni pamoja na sheria ya utumishi wa umma nambari 2 ya mwaka 2011, kanuni ya utumishi wa umma ya mwaa 2014, mafunzo ya afya na usalama kazini pamoja na mamlaka ya kuzuia rusha na uhujumu wa uchumi.

 

                          Mwisho   

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch