Skip to main content

JUKWAA LA PILI LA MSAADA WA KISHERIA ZANZIBAR LAZAA MAAZIMIO 16 KUELEKEA 2023

 



 JUKWAA LA PILI LA MSAADA WA KISHERIA ZANZIBAR 2022

Laibua maazimio 16 yenye shabaha ya uimarishaji utoaji msaada wa kisheria

LSF yaahidi makubwa, Mkurugenzi Hanifa aupiga mwingi

NA HAJI NASSOR, PEMBA::


DISEMBA 13 na 14 mwaka 2022, ilikuwa ni siku adhimu na adimu, zilizofanyika jukwaa la pili la msaada wa kisheria Zanzibar.

NINI MAANA YA JUKWAA?

Ni mkutano, mjadala, kongamano la wazi linalowakutanisha wadau wa haki jinai, kujadili, kubadilishana uwezo na kukosoana, kwa njia amani.

Maana kupitia jukwaa hilo, linalowakutanisha wadau zaidi ya 200 kutoka Unguja na Pemba, huandaliwa na wizara ya Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora, chini ya Idara ya Katiba na Msaada wa kisheria.

Jukwaa hilo, liliwakutanisha watoa msaada wa kisheria, wasaidizi wa sheria, mahakimu, waendesha mashtaka, wanufaika wa msaada wa kisheria, Polisi, masheha na wanaasasi za kiraia.

Kwa jicho la kawaida utaona kuwa, jukwaa hilo linamtiki kwa wadau hao kukutana, na kujadili changamoto, mafanikio, mwelekeo na dira ya baadae, ya utaoji wa msaada wa kisheria.

LSF

Tasisi hii, imekuwa ndio mdau mkuu wa Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria sio tu, kufanikisha majukwaa kama hayo, lakini hata, kuiwezesha Idara, kufikia malengo yake.

Ijapokuwa Idara hiyo ni ya serikali, lakini kupitia sheria yake nambari 13 ya mwaka 2018 ya Msaada wa Kisheria na hata sera yake ya mwaka 2017, hazijakataa kushirikiana na wadau.

Ndio maana, katika jukwaa la mwaka huu, ambalo lilifanyika tena Chuo cha Utalii Maruhubi mjini Unguja, na kufunguliwa na Makamu wa Pili wa rais Hemed Suleiman Abdulla, mwakilishi wa LSF alitoa neno.



‘’Niiombe sana serikli kuhakikisha, sheria ya Msaada wa Kisheria Zanzibar, nambari 13 ya mwaka 2018, ifanyiwe marekebisho,’’anasema Lulu Mwanakilala.

Mwanakilala hapa, kumbe hakulala alichoona ni kufuatia ushauri huo kwa serikali, kutaka kuwepo kifungu kipya, kinachoruhusu uanzishwaji kwa Mfuko wa Msaada wa Kisheria Zanzibar ‘MMSAKIZA’  

Hapa akisema, mfuko huo sasa unaweza kuchangiwa na serikali na watu wa asasi za kiraia, au mtu mmoja mmoja, ili sasa kuwasaidia watoa msaada wa kisheria Zanzibar.



Jengine alilolishauri kwenye jukwaa hilo, Lulu anasema wakati umefika kwa wasaidizi wa sheria, ambao hawana mishahara kupewa ofisi chini Idara ya serikali za Mitaa, ili wapunguze gharama za kukodi ofisi.

IDARA YA KATIBA, MSAADA WA KISHERIA ZANZIBAR

Ambapo Mkurugenzi wa Idara hii, Hanifa Ramadhan Said wakati akisoma yataokanayo na jukwaa la mwaka 2021, anasema yapo mengi yaliotekelezwa, baada ya kupendekezwa.

‘’Kwa sasa wasaidizi wa sheria wetu, wanavitumia vyombo vya habari wanapokuwa na shughuli zao za kutoa elimu kwa wananchi,’’anasema.



Hata suala la ushirikiano, kati ya wasaidizi wa sheria na watendaji wa serikali, unatia moyo, jambo ambalo limerahisisha utendaji wa kazi zao.

Mkurugenzi Hanifa hakuacha kuipongeza tasisi ya LSF, kwa kuendelea kuwaunga mkono, katika utekelezaji wa shughili zao hasa za kujengeana uwezo.

Kisha kwenye siku ya pili, kabla ya jukwaa hilo kufunguwa akasoma maazimioa 16 yalioibuliwa na kupitishwa na washiriki wa jukwaa hilo.

Yote ni mazuri na moja wapo ni kwa LSF kuendelea kusadiana kuwajengea uwezo watendaji wa Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria, pamoja na kufunguliwa kwa ofisi za wasaidizi wa sheria katika ofisi ya wilaya.

‘’Kuhakikisha kuandika ripoti za utendaji kazi, kwa kugusia malengo 17 endelevu ya dunia, ili kuonesha muitikio wa jamii pamoja na kuimarisha mifumo, itayohakikisha taifa linakuwa na raia wema,’’alifafanua.

Azimio jengine ni kwa Idara hiyo, kuhakikisha inachukua juhudi za kuratibu na kufanya marekesbisho ya sheria ya Msaada wa Kisheria, ili kuweka mfuko wa taifa wa Msaada wa kisheria.

Mkurugenzi huyo akasema azimio jingine ni kuongeza kasi ya mafunzo ya usuluhishi na utatuzi wa migogoro kwa wasaidizi wa sheria.



Afisa sheria wa Idara hiyo Unguja Ali Haji Hassan, anasema lazima wasaidizi wa sheria, wazidishe kasi ya kuwafikia wananchi kuwapa elimu, ushauri na msaada wa kisheria.

SERIKALI KUU                                  

Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar Hemed Suleiman Abdullah, yeye ndie aliyekuwa mgeni rasmi, katika jukwaa hilo, na kuelezea namna wasaidizi wa sheria, wanavyofanya kazi zao.

Licha ya kuvutiwa huko, amewakumbusha wasaidizi wa sheria na watoa msaada wa kisheria, kuendelea kufanya kazi zao kwa uweledi.

Hapa, akasema hasa nguvu zaidi kwao ni mapambano ya udhalilishaji, rushwa na dawa za kulevya, ambazo zinaendelea kugharimu maisha ya vijana.

Maana anaona kuwa, bado jamii inakabiliwa na changamoto hizo, hivyo ni wajibu wao kuendelea kutumia weledi wao, ili wananchi waishi kwa salama, bila ya kuwa na changamoto hizo.



Lakini hata waziri wa Nchi Afisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora Zanzibar, Haroun Ali Suleiman, yeye akasema, serikali, inajua kazi inayofanywa na wasaidizi wa sheria.

Hapa nae akawasisitiza wasaidizi wa sheria wazidishe kasi na juhudi za kuhakikisha, wanaifikisha elimu husika kwa jamii.

Mwalimu Haroun, kama wengi wanavyomuita, akaendelea kutoa darssa kwa wasaidizi hao wa sheria kuwa, serikali itaendelea kuwa karibu mno, na Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria.

Lengo anasema kwanza kuwatia moyo watendaji hao wanaoongozwa na Mkurugenzi Hanifa, ili kuona wanafanikisha malengo yao, ya kuifikia jamii.



‘’Muelewe kuwa, kazi hii ya utoaji wa masaada wa kisheria ni kazi ya kujitolea zaidi, na malipo yenu ni kwa Muumba zaidi, hivyo endeleeni kuwasaidia wananchi, ili wapate haki zao kisheria,’’alieleza.

Lakini Makamu wa Pili, alikumbushia ahadi yake kuwa, yuko tayari kuusaidia mfuko wa msaada wa kisheria, mara utakapoanzishwa, ili kuhakikisha unasaidia kusukuma mbele dhana ya utoaji wa msaada wa kisheria.



Jambo hili lilizua shangwe, vifijo, furaha na kushangiliwa na kupigiwa makofi na wasaidizi wa sheria, waliojazana kwenye jukwaa hilo la mwaka 2022.

‘’Mheshimiwa Waziri, mimi naunga mkono uanzishwaji wa mfuko huo, na niko tayari hata mshahara wangu mmoja kuuweka, na naamini na wengine watasaidia,’’aliweka bayana.

Zamu ikafika ya Naibu Katibu Mkuu wizara ya Nchi Afisi ya Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora Zanzibar Omar Haji Gora, amefurahishwa na uamuzi wa waziri Haroun, pale alipoiagiza Tume ya Kurekebisha sheria Zanzibar, ili kuifanyia marekebisho sheria ya msaada wa kisheria, Zanzibar no 13 ya mwaka 2018.

‘’Ushauri wa wenzetu wa tasisi ya LSF, kuwa sasa sheria yetu tuifanyie marekebisho, ili itambuwe uwepo wa mfuko wa maalum wa msaada wa kisheria, kama ilivyo kwa wenzetu wa Tanzani bara,’’anafafanua.

Akafafanua kuwa, jukwaa hilo ni utekelezaji wa sera ya mwaka 2017 na sheria ya msaada wa kisheria no 13 ya mwaka 2018.

Akafurahishwa na tasisi ya LSF kuwa, imekuwa karibu mno na Idara ya Katiba, Msaada wa Kisheria, katika kufanikisha majukumu yake, hasa ya kuhakikisha, wananchi wanapata haki zao na ufumbuzi wa mambo ya kisheria.

WADAU WA SHERIA

Kwenye jukwaa hilo, wapo waliopata nafasi ya kusema jambo, akiwemo mwakilishi kutoka Umoja wa watu wenye Ulemavu Zanzibar ‘UWZ’ Shaibu Abdalla Mohamed, akasema kuna ahuweni kwa watu wenye ulemavu, juu upatikanaji wa msaada wa kisheria.

‘’Jukwaa hili la pili na sisi kushirikishwa kikamilifu hadi kutoa mada ni hatua moja, maana kwa jukwaa la kwanza hatukushirikishwa kikamilifu,’’anasema.

Kwenye hili, mwakilishi kutoka LSF Said Chitung, akasema kundi la watu wenye ulemavu, lazima liangaliwe kwa macho manne, katika kuwafikia kielimu.

Akichangia kwenye jukwa hilo, Said Rashid Hassan wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ‘ZLSC’ tawi la Pemba, akasema lazima suala la utoaji wa msaada wa kisheria, liendelee kwa kasi.

Akitoa mada ya saikolojia ya jamii na upatikanaji wa msaada wa kisheria kwa wahanga na waathirika wa udhalilishaji katika mfumo wa haki jinai, wakili wa serikali Ali Rajab, anasema ni jambo la kuzingatiwa mno.

‘’Hata matumizi ya maneno wakati wa kumuuliza, kumtaka akuelezea nini alichofanyiwa, usipokuwa makini unaweza kumzidishia maumivu,’’anafafanua.

Anasema saikolojia kwa jamii wakati mwengine, mfano mdhalilishaji haonekani kama ni mtenda kosa kubwa kama kisheria, hivyo lazima kwa watoa msaada wa kisheria walijue hilo.

‘’Ndio maana wapo wanaodhalilishwa, wamekuwa wakikataa kutoa ushahidi makahamani, kwani saikolojia yao kwao hilo sio kosa kubwa,’’alifafanua.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ‘ZLSC’ Harusi Miraji Mpatani, yeye akavishauri vyama vya wanasheria, lazima viongeze nguvu, ili jamii ipate msaada wa kisheria.

Hoja yake ni kuwa, msaada wa kisheria umewalenga wale watu maskini zaidi, hivyo lazima viongozi wa vyama na wale wanasheria, wawasaidie wananchi.

‘’Hapa mawakili wa kujitegemea, lazima sasa tujitolee kuzisimamia kesi bila ya kujali malipo ‘probono cases’ na huo ndio mchango wetu kwa jamii,’’alishauri.

WASAIDIZI/WADAU SHERIA WANASEMAJE

Mkurugenzi wa Jumuia ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake ‘CHAPO’ Nassor Bilali Ali, anasema kazi inayofanywa na Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria ni nzuri.

‘’Hata sisi jumuia za wasaidizi wa sheria, inafaa kwa kila aliyepata mafunzo kuwapa wenzake, maana wakati mwengine inakuwa ngumu wasaidizi wote kufikiwa,’’anasema.

Mkuugezi wa Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Kaskazini ‘A’ Asiya Fadhil Makame, anasema moja ya changamoto wanayokumbana nayoni kukosa elimu ya saikolojia.

‘’Elimu ya mapambano dhidi ya ukatili na udhalilishaji, tunayo ingawa sasa elimu ya saikolojia ndio shida, na wakati mwengine tunawakosa kuongozana na waathirika kwenye mahojiano,’’alisema.

Lakini hata Mkurugenzi wa wasaidizi wa sheria wa sheria wilaya ya Mkoani Nassor Hakim, anasema kupitia jukwaa hilo, linawapa mwanga kwa kule kubadilishana uzoefu na wengine.

Kumbe hili la uwepo wa jukwaa, hata profesa Mohamed Makame kutoka Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ anasema, suala la usaidizi wa sheria, linafaa kuungwa mkono na jamii.

‘’Chimbuko la msaada wa kisheria ni la kujitolea zaidi, kwa ajili ya kuwafikishia huduma za msaada wa kisheria, tena bila ya malipo,’’anasema.



Jukwaa hilo lilifungwa Disemba 14, 2022 na Waziri Haroun, ambae aliwataka wasaidizi wa sheria, kuyafanyiakazi, yale waliyoyapata kwenye jukwaa hilo.

 Ambapo ujumbe wa mwaka huu ni ’Uimarishaji wa Huduma Bora na endelevu za utoaji wa msaada wa kisheria Zanzibar ‘’.

                              Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch