Skip to main content

USHIRIKA ENEO LILILOPUNGUZA FOLENI YA AJIRA SERIKALINI WANAWAKE, VIJANA WAVAMIA SEKTA HIYO

 



NA MARYAM SALUM, PEMBA:::

WALIOSEMA ‘umoja ni nguvu utengano ni udhaifu’ wala hawakukosea.

 

Waliaamini kuwa, watu wanapofanyakazi kwa pamoja, maendeleo na ushindi kwa kweli hupatikana.

Sheria namba 15 ya mwaka 2018 iliundwa kwa ajili ya kuipa nguvu  sekta ya ushirika, ili iweze kuimarika zaidi  kwa nia ya kuwafanya wananchi wapate ajira na kipato.

     HISTORIA YA VYAMA VYA USHIRIKA

Sekta ya ushirika iliasisiwa hapa Zanzibar tokea miaka ya 1923 hadi mwaka 1925, ingawaje haikupewa kipaumbele kikubwa kwa wakati huo, kutokana na ukosefu wa sera makini.

Ambapo kwa wakati huo, jamii haikuwa ikiona manufaa kwa kuwepo kwa sekta hiyo, hali iliyotajwa kupana foleni ya ajira kubwa serikalini.

 

                      HALI YA SASA

Miaka ya hivi karibuni sekta hiyo, imepewa mkazo mkubwa na kujengewa mazingira na kuundiwa sera madhubuti baada ya kuonekana ni fursa mzuri kwa wananchi kuweza kupata pahala pa kujiajiri bila ya kusubiri ajira kutoka serikalini.

Sera hiyo ilikusudia kuviimarisha vyama hivyo, ili viweze kuwa na uwezo wa kuhimili ushindani wa kibiashara, kuongeza akiba na uwekezaji na kuinuwa hali za maisha ya wanaushirika kiuchumi na kijamii.

Malengo ya sera ya ushirika mi kujenga vyama vya ushirika vilivyohuru, imara, endelevu, vinavyoendeshwa kwa uwazi, vinavyoendana na mahitaji yaliopo.

Ikitajwa vyama hivyo kuwa, vinaweza kuchangia katika kutoa fursa za ajira, kupunguza umaskini na maendeleo endelevu ya kiuchumi kwa ujumla.

Sekta ya ushirika Zanzibar inaendelea kuimarika kwa viongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, kuipa msukumo mkubwa ikiwemo nyenzo na vitendea kazi kwa wanachama ili kuona wanakuza vipato vyao kupitia sekta hiyo.

Kutokana na umuhimu huo Serikali iliandaa sera ya maendeleo ya Ushirika ya mwaka 2014, ambayo imeweka dira, dhamira pamoja na mikakati ya kutekeleza ili kuweza kuimarika zaidi sekta hiyo ya ushirika.

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar inaendelea kusimamia misingi ya kanuni za kimataifa zinazoongoza masuala ya ushirika, kwa kuhakikisha inafuata fuata misingi na kanuni za ushirika zilizotolewa na Shirika la kimataifa la vyama vya Ushirika (ICA-1937) na mapendekezo ya ‘ILO’ namba 193 ya mwaka 2002.

Kwa kuonekana kuwa sekta ya ushirika ni muhimu kwa maendeleo ya taifa na hata kuinuwa kipato ilani ya Chama cha Mapinduzi ya uchaguzi uliopita wa 2015/2020 ibara ya 85 hadi 87 iliagiza kumarishwa kwa vyama vya ushirika kama ni taasisi muhimu .

Kutokana na hilo hadi sasa vyama vya ushirika vimekuwa ni tegemeo kubwa kwa wananchi waliojiunga katika umoja huo na vimekuwa vikiongezeka siku hadi siku.

Akizungumza na makala hii Msaidizi wa Idara ya vyama vya ushirika Pemba Yussuf Saleh, anasema vyama 4,418 vimeanzishwa na kusajiliwa ambavyo vina wanachama wa mchanganyiko wakiwemo wanawake na wanaume ingawaje karibu asilimia 90 ni wanawake.



Vyama hivyo vinamtaji wa shilingi milioni 269.602 na vimefanyiwa ukaguzi na mamlaka husika vinaaminika kwamba vinafanya kazi zake kwa mujibu wa sheria za vyama hivyo.

Anasema vile sekta hiyo imekuwa ni moja ya kitu kinachotoa ajira kwa wananchi, ambao ni wanachama wa vikundi hivyo vimetowa ajira kwa wananchi 10,423wakiwemo wanawake 5,442 na wanaume 4,981.

Yussuf anaeleza kuwa kuimarika kwa vyama vya ushirika kunategemea sana, kiwango cha huduma za kitaalamu zinazotolewa kwenye vyama husika ikiwemo.

Moja ya eneo hilo ni usajili, kuvipatia ushauri wa kitaalamu, kuvisaidia katika utatuzi wa migogoro pamoja na kusimamia masuala ya utawala bora na ubadhirifu wa mali na fedha za vyama vya husika.

“Hili kama la ubadhirifu wa mali na fedha za vyama vya ushirika kama halikusimamiwa vyema, kunapeplekea kufa na tumekuwa tukiwasikia wenzetu kukumbwa na kashfa kama hizi”, alisema.

 

VYAMA VYA USHIRIKA

Katibu wa kikundi cha ushirika cha ufugaji wa samaki cha Maambani Chambani wilaya ya Mkoani, Maalim Nassor ‘Buda’ anasema kwanza kujiunga katika kikundi cha ushirika kunatoa fursa ya kujenga umoja wa ndani na nje.

Anaeleza kuwa kuanzishwa vikundi vya ushirika kunakuwa na mafanikio mbali mbali ikiwemo kupata mikopo, mafunzo ya kibiashara, kuongeza udugu na uzalishaji mkubwa wa bidhaa.

“Nawaomba wale ambao hadi sasa hawajaamua kujiunga na vikundi kama hivi, basi waanzishe na wajiunge kwa wingi kwani sasa kunafursa nyingi ambazo Serikali imeziweka kwa wale ambao wamejiunga na vikundi vya ushirika,’’anasema.

Nae Katibu wa kikundi cha ushirika wa ‘Kichakaa sishangi’ unaojihusisha na utengenezaji wa Chumvi na ufugaji wa Samaki, Shehe Bakar anasema uwepo wa ushashirika umekuwa mkombozi mkubwa kwao.

‘’Kwa hakika hata kama ni kiasi kidogo, lakini ushirika wetu umezaa ajira kwa wanachama, na hman hamna, lakini rizki inapatikana ya kuendeshea maisha,’’anasema.

Anasema kama mwanachama anakuwa mjanja wa kutafuta, kupitia vyama vya ushirika anaweza kujiendeleza na kuanzisha shughuli nyingine mbadala ambayo atajiingiza kipato.

Hata ndani ya ushirika wao, wapo wanachama toa wamefanikiwa kusomesha watoto hadi vyuo vikuu, kutibu wanafamilia na kujenga nyumba za thamani, jambo ambalo halipo kwa wale ambao hadi sasa hawajaamuwa kujiunga.

“Hii fursa ambayo ipo kwa wanaushirika, tuitumieni kwani inafaida kubwa kwetu, sasa hivi tunapatiwa mikopo mbali mbali kwa wale ambao tumejiunga,’’anaeleza.



Kwa upande wake Mwanakhamis Ali Haji mwanaushirika wa kikundi cha ‘Tumpendane’ Wingwi anasema vikundi vya ushirika, vimefanikiwa kuwatoa katika utegemezi kutoka kwa watu wengine, kwani wanakuwa wakipata fedha za mahitaji yao mengi.

“Ilikuwa ninapokumbana na changamoto za kifamilia au zangu binafisi, nilikuwa na hofu wapi nitapata pesa ya kujikwamuwa, lakini sasa namshinda mfanyakazi serikalini, wakati wowote napiga hodi kikundini nakopa,’’anaeleza.

Anawawashauri wengine kuacha kukaa bila ya kazi ni vyema wakajitokeza kujiunga na vikundi vya ushirika, ili waweze kuwa na shughuli ambazo zitawapatia kipato cha halali.

Mwanachama wa ushirika wa ‘Tuaminiane’ wa Pembeni wilaya ya Wete, Omar Ali anaona vyama vya ushirika ni moja ya hatuwa muhimu katika kujinasua na umaskini wa kipato.

Anasema  kwake fursa kubwa ambayo inampa uhakika wa maisha asasa ni kuwa na sehemu ya uhakika ya kukopa fedha hasa pale anapotokezea na shida.

 “Nimeshawahi kukopa hadi shilingi 500,000 kwangu ni fedha kubwa, maana kabla ya kujiunga na ushirika huu na kuanzisha kikundi cha kuweka na kukopa, sikuwa na uhakika,’’anasema.

Anaeleza kuwa vikundi hivyo vya kuweka na kukopa  hutumika kama ni fursa ya haraka kupata fedha za kujinasua na matatizo ya ghafla, katika kumuwezesha mwanachama kuondowa changamoto zao.

Kwa upande wake mwanaushirika wa ufugaji kuku Juma Omar wa Njuguni , anaieleza makala hii kuwa Sekta ya ushirika ni moja ya jambo ambalo limewakombowa kutokana na umaskini ingawaje sio kwa haraka sana ila Waswahili walisema kidogo kidogo ndio mwendo.

Anasema wao wanafuga kuku wa kisasa ambapo kuku mmoja ana uzito wa baina ya kilo tano hadi saba na wanauza kwa kilo moja kwa shilingi 10,000, na kupata faida ya kiasia.

“Iwapo tutawezeshwa kwa kupatiwa mikopo yenye masharti nafuu, tutapiga hatuwa kubwa, kwani hivi sasa soko lipo, ingawaje sio kubwa“, anasema.

 Akizungumza na wanachama wa vikundi vya ushirika na Saccos, ukumbi wa Samael Gombani Pemba, katika shamra shamra za siku ya Washirika Duniani , aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Wete Abeid Juma Ali, alisema Serikali imekuwa ikisaidiana na vyama hivyo katika kuwafanya Wanachama wake waweze kufikia ndoto zao.

Anaeleza kuwa, Saccos nyingi huwa zinaonekana kupata mafanikio makubwa, baada ya kuanzishwa, lakini hufa kidogo kidogo kutokana na baadhi ya viongozi kutokuwa waaminifu .

Wakati hayo yakifanyika, moja ya eneo ambalo serikali imeshaanza kuweka mazingira, kwa kuwepo kwa vituo vinne kwa ajili ya masoko ya uhakika.

Ni kujenga kituo kimoja kutoka kila wilaya kisiwani Pemba Tumbe kwa wilaya ya Micheweni, Kifumbikai wilaya ya Wete, Michakaini wilaya ya Chake chake na Kipitacho kwa wilaya ya Mkoani, kwa sasa kazi ya ujenzi imeshaanza.


Mkuu wa mkoa wa kusini Pemba, Mattar Zahoro Massoud, anasema wastani wa wajasiriamali 500 watanufaika kwa wakati mmoja kwa vituo viwili vya Chake chake na Mkoani.

“Kumalizika kwa vituo hivyo itakuwa ni fursa kwa wajasiriamali wetu, ambao wamekuw wakihangaika kupata eneo la uhakika la kuuza bidhaa zao,’’anasema.

Aisha Rashid Mohamed kutoka Mkoani anaeleza kuwa ushirika umeweza kuwasaidia na kuwakombowa wananchi wakiwemo wanawake na Vijana na kuwa kwenye hali mzuri kimaendeleo.

Nae Hadia Hamad Makame mkaazi wa Piki anasema kuwa Ushirika kama utakuwa na watu wanaoelewana na waaminifu ni moja ya chanzo kikubwa cha ajira.

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imekuwa ikiwahamasisha wananchi kila mara kuanzisha vikundi vya ushirika, ili waweze kujinasua na umaskini na kuondosha wimbi la watu wanaosubiri ajira serikalini.

                          MWISHO. 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

WATU WA KAWAIDA

 

Omar Haji Omar wa …………..anasem

 

Khadija Haji Mlekwa wa ………..anasema

 

Hasina Issa Juma wa ………………….

 

 

 

 

 

 

 

 

 

                                 MWISHO.

 

 

 

 

 

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch