Skip to main content

DK. MWINYI AIPA TANO MCT KIKAZI




NA MWANDISHI  MAALUM, MCT::

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema kuwa kazi zinazofanywa na Baraza la Habari Tanzania (MCT) hususan za kutatua migogoro inayojitokeza katika sekta ya habari ni muhimu.

Akizungumza na ujumbe wa bodi pamoja na watendaji wa MCT  Ikulu ya Zanzibar, Dk Mwinyi,  Desemba 22, 2022 amesema kuwa suala la maadili na weledi katika tasnia ya habari ni muhimu kusimamiwa na wanataaluma wenyewe ikiwa ni sehemu muhimu ya kukuza  na kuimarisha tasnia ya habari kwa ujumla.

Amesema  kuwa kuimarisha na kuendeleza  uhuru wa habari ni muhimu kwa wadau kushirikiana kwa pamoja na kalamu za wanahabari zina  nguvu  kubwa kuliko silaha.

“Kulinda uhuru wa habari ni suala la muhimu kwetu sote hivyo tushirikiane katika kulinda na kuimarisha uhuru wa habari”, alisisitiza.

Akizungumzia masuala ya utafiti na majarida mbali mbali yanayochapishwa na Baraza la Habari kwa  madhumuni ya kuyatumia kukuza taaluma ya habari  alisema kuwa hiyo ni  sehemu muhimu ya kuimarisha taaluma hiyo adhimu na muhimu.

Jinsia na vyombo vya habari nalo ni suala muhimu ambalo linahitajika kuendelezwa na kuimarishwa na hivyo kutoa wito maalum kwa baraza la habari kufuatilia kwa karibu masuala ya jinsia katika vyombo vya habari.

Rais wa Zanzibar alikiri kuwa sheria za habari hapa nchini ni za muda mrefu na hivyo serikali kwa mashirikiano na wadau wa habari itaendelea kusimamia hili ili tuweze kuwa na sheria nzuri za habari hapa nchini.

 Akiwasilisha waraka maalum kutoka kwa mwenyekti wa baraza la habari, katibu mtendaji wa baraza la habari Tanzania Kajubi Mukajanga amesema kuwa moja ya majukumu ya Baraza ni kusimamia maadili na weledi ikiwa ni sehemu muhimu ya kuimarisha na kuendeleza kada ya habari hapa nchini

“Majukumu ya kikatiba ya MCT ni pamoja na kusimamia maadili na kukuza weledi katika vyombo vya habari, kutetea na kushajiisha uhuru wa habari, kuhakikisha uwajibikaji wa vyombo vya habari kwa umma ikiwa ni pamoja na kushughulikia malalamiko ya wananchi dhidi ya vyombo hivyo, utafiti wa masuala ya habari, na kukuza usawa wa kijinsia katika vyombo vya habari”.

Katibu Mtendaji aliongeza kuwa ili kuifanya kada ya habari iweze kuimarika kuna umuhimu wa kuwa na sheria nzuri na rafiki kwa waandishi wa habari.

Sheria za habari za Zanzibar ni za muda mrefu na kuna vipengele kadhaa katika sheria hizo ambavyo vinarejesha nyuma uhuru wa habari na sekta habari kwa ujumla.

Alisema “tumefurahishwa na jinsi Serikali inavyowajumuisha wadau wa habari na wengine katika marejeo ya sheria hiyo ambayo imeonekana kupitwa na wakati na kukwaza uhuru wa wanahabari na vyombo vya habari katika kutekeleza majukumu yao na kuwapa taarifa  umma wa Wazanzibari”.

Katika mkutano huo pia Baraza la habari limepata fursa ya kumkabidhi Rais wa Zanzibar baadhi ya machapisho ya Baraza ikiwemo Kitabu cha Historia ya Vyombo vya Habari Zanzibar, Muongozo wa Kuandika Habari za Watoto, Azimio la Dar es Salaam la Uhuru wa Uhariri  na Uwajibikaji pamoja na Katiba ya Baraza la Habari Tanzania.

Waliohudhuria mkutano huo ni pamoja na Makamo Rais  MCT,   Yussuf Khamis, wajumbe wa Bodi ya Baraza la habari Edda Sanga na Bakari machumu , Katibu Mtendaji wa Baraza la habari Tanzania Kajubi Mukajanga, afisa mdhamini wa baraza la habari ofisi ya Zanzibar Shifaa Hassan pamoja na wanachama wa MCT kutoka Chuo Kikuu cha SUZA Iman Duwe na katibu wa Klabu ya Waandishi wa Habari Zanzibar Mwinyimvua Nzukwi.

                       MWISHO



Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch