Skip to main content

Posts

'MABARAZA YA MILA, DESTURI KEMEENI UNYANYASAJI KWA WATOTO' DK. OSWALD

J oyce Joliga,Tunduru Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Makumbusho ya Taifa Tanzania  Dkt. Oswald Masebo alitoa ushauri mzito wa kuyataka Mabaraza ya Mila na Desturi  kutumia matamasha ya kumbukizi yatumike   kukemea vitendo  vya unyanyasaji  Watoto, wenye umri  wa siku 0 hadi miaka 8   Watoto hao wanekuwa  wajikutana na vitendo vya ukatili  ikiwemo ubakaji ,ulawiti  ambavyo  vimekithiri kwenye jamii ili kujenga jamii bora ambayo inaenzi mila na Desturi za kitanzania.   Kadhalika ameyataka Mabaraza ya Mila na Desturi kukemea  vitendo vya ushoga  ambavyo vimekithiri nchini vikiwemo na vitendo   viovu vinavyokwenda kinyume na mila na desturi ya    mtanzania.  Ikumbukwe kuwa Ushauri huu wa D kt.Masebo ametoa ushauri huo kwenye kongamano la kumbukizi ya  mashujaa wa vita ya Majimaji lililofanyika kwenye ukumbi wa Crasta mjini  Tunduru. Kongamano hilo...

ULINZI SHIRIKISHI NG'AMBWA CHAKE CHAKE WAPUNGUZA WIZI KIDOGO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANANCHI wa kijiji cha Vikunguni shehia ya Ng’ambwa wilaya ya Chake chake Pemba, wamekiri kupungua kidogo kwa vitendo vya wizi wa mifungu na mazao, baada ya ulinzi shirikishi kuimarika shehiani humo. Walisema, ijapokuwa bado wapo baadhi ya wananchi wamekuwa wakiidharau na kukebehi uwepo wa ulinzi shirikishi, lakini vitendo vya wizi wa Ng’ombe na mazao umeanza kupungua kwa kasi. Wakizungumza na waandishi wa habari waliofika kijijini hapo kusikiliza kero zao, walisema sasa mifugo imekuwa salama kwa kiasi fulani. Walisema, kwa sasa wanalala kwa amani na wanaweza kukaa hadi miezi mitatu bila ya kusikia uwepo wa wizi wa mifugo na mazao kama ilivyokuwa miaka iliyopita. Mwananchi Khamis Ali Khamis, anasema kabla ya ulinzi shirikishi kuimarishwa, kila mwezi kulikuwa wizi wa Ng’ombe kati ya watano hadai saba. ‘’Kwa sasa unaweza kukaa miezi mitatu, ukasikia tukio moja la wizi wa Ng’ombe kwetu sisi hali hiyo, tunasema afadhali mno tofauti na zamani,’’al...

JAJI MKUU ZANZIBAR AWAPIGA MARUFUKU MAKARANI 'VISHOKA'

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ JAJI Mkuu wa Zanzibar Khamis Ramadhan Abdalla, amepiga marufuku kwa makarani wa mahakama, kuandika hati za madai kwa wananchi, kwani kufanya hivyo, ni kinyume na sheria za utumishi. Jaji Mkuu huyo aliyasema hayo leo Machi 16, 2023 ukumbi wa mahakama kuu Pemba, wakati akizungumza na mawakili wa kujitegemea na wale wa serikali, kwenye kikao kazi, cha kupokea ushauri kuelekea mwaka mpya wa mahakama. Alisema, tayari Mahakama kuu imeshapiga marufuku kwa muda mrefu kwa makarani wa mahakama, kuchukua kazi za kuandika hati za madai, kwani wanakuwa wanazitumia vibaya rasilimali za serikali. ‘’Kuhusu baadhi ya watendaji wa mahakama, na hasa makarani kuandika hati za madai ‘plaint’ tumeshapiga marufuku kwa muda mrefu, na natarajia sasa watendaji wawe wameshalisikia hili,’’alieleza. Katika hatua nyingine, Jaji Mkuu huyo wa Zanzibar Khamis Ramadhan Abdalla, alisema serikali iko katika hatua za mwisho za kuandaa mpango, wa utozaji kodi itokanayo na...

MIAKA 10 BAADA YA UJENZI WA BARABARA ZA ‘MCC’ PEMBA, WANAWAKE WAZIFIKIA HUDUMA ZA KIJAMII 'UBWETE'

  NA HAJI NASSOR, PEMBA SASA ni majira ya saa 8:00 jioni, jua limeshateguka, vivuli vya miti mikubwa ndio mwemvuli wangu, nipo hapa kituo cha afya cha Uwondwe shehia ya Mtambwe kaskazini, wilaya ya Wete Pemba. Mbele yangu, namuoma mjamzito, akitokea chumba cha muuguzi wa afya ya mama na mtoto, huku mkononi akiwa na gamba la kliniki, akionekana na tabasamu. Nilipomkaribia aliniambia, sasa huduma za mama na mtoto, wanazipata ndani ya kituo hicho, na hasa baada ya kumalizika kwa ujenzi wa barabara yao ya Bahanasa- Mtambwe. Barara hiyo, ni kati ya zile tano (5), ziilizojengwa kwa ufadhili wa Mfuko wa Changamoto za Millenia na watu wa Marekeani ‘MCC’ ikiwa ni ile ya Kipangani- Kangani, Chwale- Likoni, Mzambarau takao pamoja na Pandani hadi Finya zenye urefu wa kilomita 35 kwa ujumla. Kwa uwepo wa barabara hiyo, wananawake wa Mtambwe, wanasema moja ya huduma zilizoimarika ni upande wa afya ya mama na mtoto, na sasa ni miaka tisa (9), wamesahau machungu, dhiki na shida. HU...

INTERNEWS: LAWAKUMBUSHA WAANDISHI KUANDIKA HABARI ZA UCHUNGUUZI

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WAANDISHI wa habari nchini, wamesisitizwa kujikita katika kuandika habari za uchunguuzi, ambazo kwa kwaida huisaidia jamii, katika kupata haki na kukuza uhuru wao wa kujieleza. Akifungua mafunzo ya siku moja leo Machi 14, 2023 kwa njia ya kielektroniki ya zoom, wakati akifungua mafunzo ya siku moja kwa waandishi wa habari, Msimamizi wa vyombo vya habari kutoka Internews Alakok Mayombo kupitia mpango maalum chini mradi wa Boresha habari, unaotekelezwa na Intrernews Tanzania. Alisema, njia ya waandishi wa habari kujikita katika kuandika habari za uchunguuzi, ndio ambazo huibua changamoto kwa jamii na kuimarisha uhuru wa kujieleza. Alieleza kuwa, katika eneo la utawala bora, haki za binaadamu, jinsi na afya hasa eneo la Covid 19, ambalo linahitaji kuangaliwa kwa kina, ili jamii itambua haki zao. Alifahamisha kuwa, bado jamii inavitegemea vyombo vya habari, kuandika habari kwa kina na zenye tija, ili kujua wajibu wao, haki zao pamoja na changamoto ...

WEJISA WAJUMUIKA NA WANAWAKE WENZAO KUSHEHEREKEA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI

  Na Mwandishi Wetu, WAFANYAKAZI wa Kampuni ya  Weka Jiji Safi Limited  (WEJISA ) wameungana na wanawake wenzao kusheherekea sikujui ya wanawake inayoadhimishwa Machi 8 Kila mwaka. Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni hiyo Bi.Nuru  Hassan amesema kuwa, maadhimisho hayo yanaleta chachu ya Maendeleo kwa wanawake Kwa sababu ya Rais Samia Suluhu Hassan  kuonyesha njia ya kuwa wanawake tunaweza. Amesema kuwa Rais Samia ameweza  kuweka mazingira mazuri ya wanawake kujituma na kufanya kazi Kwa bidii bila ya kuwa wategemezi , jambo ambalo limeongeza uchapakazi Kwa jinsia hiyo. "Rais wetu Samia tunamuunga mkono kwa sababu nafasi aliyonayo amesaidia kuongeza mwamko kwa wanawake kufanya kazi na wale ambao walikua hawana kazi na kutafuta shughuli zozote ili waweze kujiondoa kwenye utegemezi," alisema Nuru. Alisema kuwa, kampuni ya WEJISA  itaendelea kushirikiana na Serikali bega kwa bega na ndo maana leo tumekuja hapa kusheherekea pamoja na kujifunza mengi kwa Wafanyakazi w...

UWT YATOA ONYO KWA WANAWAKE UNYANYASAJI WATOTO

  NA MARYAM SALUM, PEMBA MWENYEKITI wa UWT Taifa Mary Pius Chatanda amewataka wanawake wenzake kuacha tabia ya kuwanyanyasa   na kuwatelekeza watoto kwani hilo sio jambo la busara kwa jamii na hata mbele ya Mungu. Wito huo ulitolewa Machi 8, 2023 na Mwenyekiti huyo katika Kiwanja chakufurahishia watoto kilichopo Tibirinzi Chake Chake kwenye wiki ya siku ya mwanamke Duniani ambapo huadhimishwa kila ifikapo machi 8 ya mwaka. Alisema kuwa suala la malezi kwa   watoto sio la mzazi mmoja ni jukumu la kila mmoja ndani ya jamii ili kuondosha changamoto mbali mbali zinazoweza kujitokeza. Alieleza kuwa sio jambo la busara kwa mzazi kutupa mtoto ama kutelekeza mtoto kwa sababu tu yakukosa huduma ama mahitaji kutoka kwa mwenza wake. “Tusitupe watoto kwani hatujui hapo mbeleni mtoto huyo unaemtupa atakuja kuwa nani katika jamii, hivyo tulee watoto wetu kwa kila hali ili kuwaepusha na vitendo vya ukatili wa Kijinsia ambao umeshamiri ndani ya jamii zetu,” alisema Mwenyekiti h...

WIZARA YA ELIMU: ''WANAFUNZI WARIPOTINI WAALIMU WANAOWANYEMELEA KIMAPENZI''

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WIZARA ya Elimu na Mafunzo ya Amali wilaya ya Chake chake, imewataka wanafunzi kuwaripoti mara moja, waalimu watakaoonesha dalili za kuchupa mipaka yao ya ualimu, na kuelekea katika vitendo vya udhalilishaji dhidi yao. Kaimu Afisa Elimu na Mafunzo ya Amali wilayani humo, Khamis Juma Yahya, alitoa agizo hilo leo Machi 8, 2023 wakati akizungumza na wanafunzi wa skuli ya sekondari ya Dk. Omar Ali Juma, kwenye kampeni maalum, ya kuongeza uwelewa, kwa wanafunzi wa skuli, madrassa, vyuo vikuu na klabu za sanaa, iliyoandaliwa na TAMWA-Zanzibar. Alisema waalimu nao ni binaadamu, kama walivyowengine, wanaweza kujisahau na kuanza kuvunja maadili yao, hivyo ikijitokeza hayo, wanafunzi wasisite kutoa taarifa za haraka. Alieleza kuwa, udhalilishaji hauna kabila, mtu maalum, umri, cheo wala wakati, hivyo wanafunzi hawanabudi kuwa makini na waalimu, ambao watawataka kimapenzi. ‘’Niwakumbushe jambo wanafunzi wangu, hata waalimu kwa vile ni binaadamu ...