Skip to main content

INTERNEWS: LAWAKUMBUSHA WAANDISHI KUANDIKA HABARI ZA UCHUNGUUZI

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WAANDISHI wa habari nchini, wamesisitizwa kujikita katika kuandika habari za uchunguuzi, ambazo kwa kwaida huisaidia jamii, katika kupata haki na kukuza uhuru wao wa kujieleza.

Akifungua mafunzo ya siku moja leo Machi 14, 2023 kwa njia ya kielektroniki ya zoom, wakati akifungua mafunzo ya siku moja kwa waandishi wa habari, Msimamizi wa vyombo vya habari kutoka Internews Alakok Mayombo kupitia mpango maalum chini mradi wa Boresha habari, unaotekelezwa na Intrernews Tanzania.

Alisema, njia ya waandishi wa habari kujikita katika kuandika habari za uchunguuzi, ndio ambazo huibua changamoto kwa jamii na kuimarisha uhuru wa kujieleza.

Alieleza kuwa, katika eneo la utawala bora, haki za binaadamu, jinsi na afya hasa eneo la Covid 19, ambalo linahitaji kuangaliwa kwa kina, ili jamii itambua haki zao.

Alifahamisha kuwa, bado jamii inavitegemea vyombo vya habari, kuandika habari kwa kina na zenye tija, ili kujua wajibu wao, haki zao pamoja na changamoto zilizopo.

‘’Waandishi wahabari nyinyi ambao meingia katika mafunzo haya maalum, Internews imewaamini na bila shaka, na nyinyi mtaifanya kazi hii kwa kina,’’alieleza.

Katika eneo jingine, Msimamizi huyo wa vyombo vya habari kutoka Internews Alalok Mayombo, alisema vyombo vya habari, bado vitaendelea kuwa tegemeo kwa jamii husika.

Mkufunzi wa mafunzo hayo, mwandishi mkongwe Erick Kabendera, alisema habari za kina ‘uchunguuzi’ zinahitajika kufanywa kwa utulivu na tahadhari kubwa.

‘’Mara zote unapoandika habari za ukweli, huweza kukuletea madhara ikiwe kifo, kuwekwa chini ya ulinzi, kwani wanaoandikiwa huwa hawapendi, aibu zao zinatoka nje,’’elieleza.



Hata hivyo amewataka waandishi hao wa habari, kuwashirikisha wengine ili kupata jicho la pili, kwani habari inajengwa makundi mbali mbali.

Katika hatua nyingine alisema, kinga pekee kwenye habari za uchunguuzi ni kuandika habari za ukweli na zenye ushahidi, ambapo kufanya hivyo wengine watawajibishwa.

Aidha amewahimiza waandishi kujisomea kwa kina, kwani jukumu lao ni kuandika na kusoma zaidi ili kuandika habari zenye tija.

Wakitoa maoni yao, waandishi hao wa habari, wameahidi kuyafanyia kazi mafunzo, na kwa kuandika habari za kina, ili kuimarisha utawala bora na uhuru wa maoni.

Mwandishi Denis Nyali, alisema sasa ameelewa kuwa, sio kila tukio linaweza kuwa habari ya uchunguuzi, kama halikutimia vigezo husika.

 Nae Chelu Matuzya, alisema kweli kuna umuhimu mkubwa wa mwandishi wa habari kusoma zaidi, ili kuwa mweledi wa kuandika habari za uchunguuzi.

Faraja Masinde, alisisitiza kuwa, bado kuna umuhimu wa kwa waandishi w ahabari kuendelea kufuatilia kwa karibu ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi wa hsabu za serikali, ili kupata vyanzo vyengine vya kuandika. 

                 Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch