Skip to main content

ULINZI SHIRIKISHI NG'AMBWA CHAKE CHAKE WAPUNGUZA WIZI KIDOGO

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WANANCHI wa kijiji cha Vikunguni shehia ya Ng’ambwa wilaya ya Chake chake Pemba, wamekiri kupungua kidogo kwa vitendo vya wizi wa mifungu na mazao, baada ya ulinzi shirikishi kuimarika shehiani humo.

Walisema, ijapokuwa bado wapo baadhi ya wananchi wamekuwa wakiidharau na kukebehi uwepo wa ulinzi shirikishi, lakini vitendo vya wizi wa Ng’ombe na mazao umeanza kupungua kwa kasi.

Wakizungumza na waandishi wa habari waliofika kijijini hapo kusikiliza kero zao, walisema sasa mifugo imekuwa salama kwa kiasi fulani.

Walisema, kwa sasa wanalala kwa amani na wanaweza kukaa hadi miezi mitatu bila ya kusikia uwepo wa wizi wa mifugo na mazao kama ilivyokuwa miaka iliyopita.

Mwananchi Khamis Ali Khamis, anasema kabla ya ulinzi shirikishi kuimarishwa, kila mwezi kulikuwa wizi wa Ng’ombe kati ya watano hadai saba.

‘’Kwa sasa unaweza kukaa miezi mitatu, ukasikia tukio moja la wizi wa Ng’ombe kwetu sisi hali hiyo, tunasema afadhali mno tofauti na zamani,’’alisema.



Kwa upande wake mfugaji Mohamed Mkubwa Mohamed, alieleza kuwa walifikia wakati wanapolala wao ndio walipokuwa wakiilaza mifugo yao.

‘’Ilikuwa lazima Ng’ombe au Mbuzi umlaze chini ya dirisha la nyumba yako, maana ukimuacha malishoni siku ya pili ukienda ameshaibiwa,’’anafafanua.

Wakulima Leluu Suleiman Said, Saada Suleiman Omar na Mtumwa Ali Omar, walisema ijapokuwa wizi haujaondoka moja kwa moja, lakini wanalima na kuvuna mazao mapevu.

Walisema, katika kijiji chao cha Vikunguni ndizi, muhogo, mananasi ilikuwa sio rahisi kuvunwa mapevu, maana vijana wao walikuwa wakiyaiba.



‘’Kwa mfano kama wizi wa Ng’ombe na mazao mara nyingi hufanyika nyakati za usiku au siku ya Ijumaa wakati waumini na dini ya kiislamu wakiwa kwenye ibada,’’wanasema.

Vijana Issa Khamis Issa, Kombo Juma Hassan na Mundhiri Ilyasa Hilali wanasema, moja ya eneo ambalo linapaswa kudhibitiwa ni matumizi ya dawa za kulevya.

‘’Ingawa jambo hili vijana wa shehia moja na nyingine huchanganyika, lakini kama hawa wa Ng’ambwa watadhibitiwa inaweza kuwa mwarubaini kwa vitendo vya wizi,’’wanasema.

Sheha wa shehia Ng’ambwa Issa Rihani Abass, amesema alimua kuelekeza nguvu katika ulinzi shirikishi, ili kupunguza vitendo vya jinai shehiani humo.


‘’Ni kweli baada ya kuteuliwa kushika nafasi hii, moja ya changamoto niliyoiona ilikuwa ni wizi wa macho macho, sasa tukajipanga na wananchi na ndio maana kuna afadhali,’’anafafanua.

Hata hivyo alisema, bado dhamira yake hasa ya hapo baadae ni kuona shehia ya Ng’ambwa wananchi wanalala bila ya hofu, pamoja na wakulima na wafugaji kuendesha shughuli zao kwa amani.





Mkuu wa wilaya ya Chake chake Abdalla Rashid Ali, amekuwa akirejea kuali yake kwa wananchi, kuwa njia moja nzuri ya kuzuia uhalifu kwenye maeneo yao ni kuiunga mkono Polisi Jamii.

Shehia ya Ng’ambwa wilaya ya Chake chake inao wakaazi 2500, inazo huduma za kijamii kama afya, elimu, mawasiliano ya simu na huduma za barabara kwa kiwango cha kifusi.

                                  Mwisho

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch