Skip to main content

WIZARA YA ELIMU: ''WANAFUNZI WARIPOTINI WAALIMU WANAOWANYEMELEA KIMAPENZI''

 

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WIZARA ya Elimu na Mafunzo ya Amali wilaya ya Chake chake, imewataka wanafunzi kuwaripoti mara moja, waalimu watakaoonesha dalili za kuchupa mipaka yao ya ualimu, na kuelekea katika vitendo vya udhalilishaji dhidi yao.

Kaimu Afisa Elimu na Mafunzo ya Amali wilayani humo, Khamis Juma Yahya, alitoa agizo hilo leo Machi 8, 2023 wakati akizungumza na wanafunzi wa skuli ya sekondari ya Dk. Omar Ali Juma, kwenye kampeni maalum, ya kuongeza uwelewa, kwa wanafunzi wa skuli, madrassa, vyuo vikuu na klabu za sanaa, iliyoandaliwa na TAMWA-Zanzibar.

Alisema waalimu nao ni binaadamu, kama walivyowengine, wanaweza kujisahau na kuanza kuvunja maadili yao, hivyo ikijitokeza hayo, wanafunzi wasisite kutoa taarifa za haraka.

Alieleza kuwa, udhalilishaji hauna kabila, mtu maalum, umri, cheo wala wakati, hivyo wanafunzi hawanabudi kuwa makini na waalimu, ambao watawataka kimapenzi.

‘’Niwakumbushe jambo wanafunzi wangu, hata waalimu kwa vile ni binaadamu wanaweza kutaka kuvunja maadili, sasa mkihisi kuna viashiria hivyo, toweni ripoti japo kwa wazazi,’’alieleza.





Hata hivyo, amewakuwambusha kuwa, kwa sasa kazi iliyoko mbele yao ni kusoma kwa bidii, ili wajijengee misingi imara ya maisha yao ya leo na baadae.

Nae Mratibu wa Chama cha waandishi wa habari Wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar ofisi ya Pemba Fat-hya Mussa Said, aliwaonya wanafunzi hao, kutokubali kuchezewa wala kuchezeana sehemu zao za siri.

Aliweleza kuwa, sehemu hizo ni mali ya mwanafunzi mwenyewe, na kusiwe na mtu mwengine yeyote, atakaepata ruhusa ya kumchezea.

‘’Jitambue, jielewe, jiheshimu na ujue kuwa, sehemu zako zote za siri ni mali yako, na jitahidi mno kuhakikisha, hakuna mwengine anaezichezea,’’alifafanua.

Akizungumza miongoni mwa dalili za mtu aliyedhalilishwa ni pamoja na kutopenda kujichanga na wenzake, kukosa uchangamfu, kukosa hamu ya kusoma pamoja na kupata msongo wa mawazo.

Kuhusu kampeni hiyo, alisema lengo ni kuwafikia wanafunzi wa skuli, walioko vyuo vikuu, madrassa na vikundi vya sanaa, ambapo mwisho, hutakiwa kuvibua na kuviripoti vitendo vya udhalilishaji.

Kwa upande wake Mwalimu mkuu skuli ya sekondari ya Dk. Omar, Said Ali Makame, alisema elimu kama hiyo, huwapa uwelewa wanafunzi na waalimu kwa ujumla.





‘’Niwaombe TAMWA, wasisite kuja mara kwa mara, maana sisi waalimu tukisema na wageni kama hivi wakisema, inasaidia elimu hii, kufika kuwafikia,’’alieleza.

Mapema Msaidizi wa sheria, Said Rashid Hassan, alisema kwa vile dini zote zinapinga ukatili na udhalilishaji, ni wajibu wa jamii kulikataa kwa vitendo jambo hilo.

Alifafanua kuwa, msingi imara wa kila mmoja hapa dunia na siku ya malipo, ni kupata elimu na kuitumia kwa vitendo, hivyo ikiwa wanafunzi watapuuza masomo yao, watakuwa wamejikosesha haki yao.

‘’Wazazi wanawajengea wamazingira imara, ikiwemo ya huduma za kila siku, mavazi, chakula ili muhakikishe mnapata elimu, sasa sio wakati wa kujihusisha na mapenzi,’’alieleza.

Wakili wa watoto wanaokinzana na sheria, kutoka Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ‘ZLSC’ tawi la Pemba Siti Habib Mohamed, alisema sheria ya Mtoto nambari 6 ya mwaka 2011 ya Zanzibar, bado haijaweka adhabu kwa mtoto, anayefanya kosa la jinai.

‘’Kwa mfano mtoto ndiye anayefanya kosa, na anapelekwa mahakamani, lakini mahakama inapomtia hatiani kama ni fidia au faini, anayelipa ni mzazi,’’alifafanua.




Hata hivyo alieleza kuwa, ikiwa mzazi amekosa uwezo huo, mtoto huyo hutakiwa afikishwe kwenye nyumba ya kurekebisha tabia, ambazo hadi sasa serikali haijazijenga.

Katika hatua nyingine, amewaonya wanafunzi wa kike kuendelea kushughulikia masomo yao, na kuacha tabia ya kujihusisha na vitendo vya ngono.

Baadhi ya wanafunzi wa skuli hiyo, waliouliza maswali na kutoa maichango yao, walipendekeza kwa sasa wanawake watakaochangia wenyewe kudhalilishwa, nao waapate adhabu mahakamani.

Aidha wanafunzi hao, walitaka kujua, ikitokezea mtoto wa kike amemfuata mwanamme masafa marefu, adhabu yake ikoje kwa mujibu wa sheria.

TAMWA-Zanzibar kwa sasa inaendelea na kampeni ya kusaidia wadau katika mapamabano ya udhalilishaji wa wanawake na watoto, kupitia skuli, madrassa, vyuo vikuu na vikundi vya sanaa na kisha kuchukua hatua, kupitia mradi tumia jukwaa la habari kumaliza udhalilishaji.

                             Mwisho

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch