Skip to main content

WEJISA WAJUMUIKA NA WANAWAKE WENZAO KUSHEHEREKEA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI

 




Na Mwandishi Wetu,

WAFANYAKAZI wa Kampuni ya 
Weka Jiji Safi Limited  (WEJISA ) wameungana na wanawake wenzao kusheherekea sikujui ya wanawake inayoadhimishwa Machi 8 Kila mwaka.

Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni hiyo Bi.Nuru  Hassan amesema kuwa, maadhimisho hayo yanaleta chachu ya Maendeleo kwa wanawake Kwa sababu ya Rais Samia Suluhu Hassan  kuonyesha njia ya kuwa wanawake tunaweza.

Amesema kuwa Rais Samia ameweza  kuweka mazingira mazuri ya wanawake kujituma na kufanya kazi Kwa bidii bila ya kuwa wategemezi , jambo ambalo limeongeza uchapakazi Kwa jinsia hiyo.

"Rais wetu Samia tunamuunga mkono kwa sababu nafasi aliyonayo amesaidia kuongeza mwamko kwa wanawake kufanya kazi na wale ambao walikua hawana kazi na kutafuta shughuli zozote ili waweze kujiondoa kwenye utegemezi," alisema Nuru.

Alisema kuwa, kampuni ya WEJISA  itaendelea kushirikiana na Serikali bega kwa bega na ndo maana leo tumekuja hapa kusheherekea pamoja na kujifunza mengi kwa Wafanyakazi wetu Wanawake" alisema Nuru Seif Hassan

Aidha, amesema kuwa amepata faraja kujumuika na Wanawake hao kwani wamekuwa chachu ya Maendeleo ya Kampuni hiyo.

Wanawake hao wa WEJISA wanatoka vitengo mbalimbali ikiwemo wanaosafisha maeneo ya Jiji, ikiwemo ufagiaji, ukusanyaji wa taka na usafi wa mazingira.

Lengo la tukio hilo ni kupeana moyo kama Wanawake katika kuamua mambo katika kufanikisha utendaji bora wa kazi.

Kwa upande wake Patricia Kimelemeta Mwandishi Kimara wa Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Mtoto Mkoa wa Dar es Salaam ambaye alitoa mada ya malezi na makuzi Kwa watoto katika tukio hilo la kusheherekea siku ya Wanawake, ambapo alisema kuwa, licha ya wanawake kufanya Kazi mbalimbali lakini pia tunapaswa kutimiza wajibu Kwa watoto wetu katika masuala ya Malezi na makuzi.

"Baadhi ya wanawake wanashindwa  kutimiza wajibu wao Kwa watoto Kwa kisingzio cha kufanya Kazi, jambo ambalo limesababiaha watoto kukosa mapenzi na wazazi wao badala yake kulelewa na ndugu au jamii.

" Hivyo basi wakati kunasheherekea madhimisho haya tunapaswa kujua kuwa sisi ni mama, wazazi na walezi, hata kama tunafanya kazi lakini pia tunapaswa kutimiza wajibu wetu kama wazazi na  walez", amesema Kimelemeta.

Ameongeza kuwa, watoto wenye umri kuanzia sifuri hadi miaka minane wanahitaji uangalifu wa hili ya juu na wazazi, walezi au jamii inayowazhnguka Ili waweze kukua Katika hali ya utimilifu.



Amesema kuwa, katika.maadhimisho haya wanawake wanapaswa kukumbushana na kuhimizana Ili Kila mmoja anapotoka hapa abadilikw na kujiona kuwa ana wajibu wa kumlinda, na kumtetea mtoto wake au aliyepo kwenye jamii anayoishi.

Amesema kuwa, Serikali inatekeleza mradi wa Malezi, makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto (PJT-MMMAM) ikiwa ni pamoja na kuwataka watoto wake Katika hali ya utimilifu, wasomw katika mazingira bora na jamii ihusike Katika ulinzi na usalama wa mtoto.

 Hata hivyo, baadhi ya wanawake wa Kampuni hiyo  wameushukuru uongozi wa kampuni hiyo kwani imekuwa mkombozi kwao na wamekuwa wakifanya kazi moyo.

"Mie nina familia, nikitoka nyumbani naandaa kabisa chakula kwa wanangu.

Aidha, amewataka Wanawake kuzingatia sheria za Usalama barabarani kwani wamekuwa wakishuhudia matukio mengi, ikiwemo wao kugongwa.'  Alisema Bi. Asha Salum.



Kwa upande wake. Sharifa Magombeka amesema kuwa, anafanya kazi ya kuzoa taka ilikupata kipato chake halali,

"Mwanamke ni kujitambua, nafanya kazi yangu ya kuzoa taka hii kupata kipato kihalali, tunamshuru Mhe Rais kuendelea kueka mazingira ya ufanyaji kazi,
Leo tumejumuika hapa tumepata elimu, lakini pia tumefuraia pamoja" alisema Sharifa.


 Mwisho.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch