Skip to main content

JAJI MKUU ZANZIBAR AWAPIGA MARUFUKU MAKARANI 'VISHOKA'

 


 

NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

JAJI Mkuu wa Zanzibar Khamis Ramadhan Abdalla, amepiga marufuku kwa makarani wa mahakama, kuandika hati za madai kwa wananchi, kwani kufanya hivyo, ni kinyume na sheria za utumishi.

Jaji Mkuu huyo aliyasema hayo leo Machi 16, 2023 ukumbi wa mahakama kuu Pemba, wakati akizungumza na mawakili wa kujitegemea na wale wa serikali, kwenye kikao kazi, cha kupokea ushauri kuelekea mwaka mpya wa mahakama.

Alisema, tayari Mahakama kuu imeshapiga marufuku kwa muda mrefu kwa makarani wa mahakama, kuchukua kazi za kuandika hati za madai, kwani wanakuwa wanazitumia vibaya rasilimali za serikali.

‘’Kuhusu baadhi ya watendaji wa mahakama, na hasa makarani kuandika hati za madai ‘plaint’ tumeshapiga marufuku kwa muda mrefu, na natarajia sasa watendaji wawe wameshalisikia hili,’’alieleza.

Katika hatua nyingine, Jaji Mkuu huyo wa Zanzibar Khamis Ramadhan Abdalla, alisema serikali iko katika hatua za mwisho za kuandaa mpango, wa utozaji kodi itokanayo na malipo ya mawaikili wa kujitegemea.

Alifafanua kuwa, Mawakili wamekuwa wakidai kuwa wanatoa huduma kwa wananchi, ingawa nao wamekuwa wakiwatoza fedha nyingi, bila kutozwa kodi.

‘’Mjiandae sasa kutoa kodi kwenye malipo mnayowatoza wananchi wanaotaka huduma, za uwakili kwenye mahakama zetu mbali mbali, ili nayo serikali ipata mapato yake,’’alieleza.

Aidha Jaji mkuu huyo wa Zanzibar, aliwataka mawakili hao, kuendelea kulinda maadili na nidhamu za kazi zao, ili waendelee kuwa kimbilio kwa wananchi.



‘’Katika siku za hivi karibuni, kumeibuka wimbi la baadhi ya Mawakili kuchupa maadili yao, ikiwemo kutoleana lugha chafu na mahakimu, jambo ambalo halijengi taswira nzuri,’’alieleza.

Kuhusu ucheleweshaji wa mwenendo wa kesi, ‘proceeding’ alisema kwa sasa jambo hilo, halitarajii kutokea, baada ya kuongeza vitendea kazi.

‘’Hivi karibuni tumeshanunua kompyuta 10 na kuongeza idadi ya watendaji, lengo ni kuona tunafanikisha utendaji wetu wa kazi, ikiwemo uandishi wa mwenendo wa kasi,’’alieleza.

Mapema Mrajisi wa mahakama kuu Pemba, Faraji Shomari Juma, alisema mkutano huo umesadia kuwaamsha Mawakili hao, katika utendaji wao wa kazi.

Alieleza kuwa, vikao kama hivyo, husababisha watendaji hao kuelezea mafanikio na changamoto zao, katika kufanikisha kazi za kutoa huduma kwa jamii.




Akitoa neno la shukran, Wakili wa kujitegemea Zahran Mohamed Yussuf, alimuahidi Jaji Mkuu huyo kuyafanyia kazi maagizo aliyoyatoa kwenye mkutano huo.




Nae Mwanasheria dhamana wa Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka Pemba, Ali Haidar Mohamed alisema ushirikiano uliopo baina ya mahakimu na mawakili wa kujitegemea, unajenga ari kubwa ya kazi.

Jaji Mkuu wa Zanzibar Khamis Ramadhan Abdalla, yupo kisiwani Pemba, kwa ziara ya maalum ya kukutana na watendaji wake, ambapo pia alizungumza na mawakili wa serikali na wale binafsi.

                                      Mwisho  

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch