Skip to main content

'MABARAZA YA MILA, DESTURI KEMEENI UNYANYASAJI KWA WATOTO' DK. OSWALD




Joyce Joliga,Tunduru

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Makumbusho ya Taifa Tanzania Dkt. Oswald Masebo alitoa ushauri mzito wa kuyataka Mabaraza ya Mila na Desturi  kutumia matamasha ya kumbukizi yatumike kukemea vitendo  vya unyanyasaji  Watoto, wenye umri  wa siku 0 hadi miaka 8  


Watoto hao wanekuwa  wajikutana na vitendo vya ukatili  ikiwemo ubakaji ,ulawiti  ambavyo  vimekithiri kwenye jamii ili kujenga jamii bora ambayo inaenzi mila na Desturi za kitanzania.

 

Kadhalika ameyataka Mabaraza ya Mila na Desturi kukemea  vitendo vya ushoga  ambavyo vimekithiri nchini vikiwemo na vitendo   viovu vinavyokwenda kinyume na mila na desturi ya  mtanzania.


 Ikumbukwe kuwa Ushauri huu wa Dkt.Masebo ametoa ushauri huo kwenye kongamano la kumbukizi ya mashujaa wa vita ya Majimaji lililofanyika kwenye ukumbi wa Crasta mjini Tunduru.


Kongamano hilo ni sehemu ya kumbukizi ya miaka 118 ya mashujaa wavita ya Majimaji waliuawa na wajerumani Februari 27,1906 kwa kunyongwa mashujaa 67 na wajeruamni katika eneo la Songea Klabu na kuzikwandani ya makumbusho yaTaifa ya Majimaji Mahenge Songea.


Taifa lipo katika vita ya kupambana na watu wanaoharibu mila nadesturi za mtanzania ambapo kumekuwa na mmomonyoko wa maadili kwa Watoto na vijana.


“Hivi sasa vitendo vya ukatili kwa watoto wadogo hasa wenyeumri  chini ya miaka 8 ,ubakaji,ulawiti vinatishia  maishaya watoto wetu ni jukumu  la Wazee  kutumia matamasha haya kuelimisha jamii kuacha vitendo hiyo ,pia vitendo vya  kishoga ambavyo ni kinyume na mila na desturi zetu vimekuwa tishio kubwa kwa vijana wetu,hivyo tunapofanya kumbukizi kama
hii ya mashujaa wa vita ya Majimaji inatakiwa sote kukemea kwa nguvu
zote ili kulinusuru Taifa kuingia kwenye janga kubwa la mmomonyoko wa
maadili’’,alisisitiza Dkt.Masebo.


Siyo siri kumekuwa na vitendo vingi vya matukio ya unyanyasaji watoto ambavyo vinakiuka haki za watoti na haki za Binadamu,Kesi zinaendelea .


Akizungumza wakati wa ufungaji kongamano hilo ambalo lilishirikisha wadau mbalimbali kutoka mkoa wa Ruvuma ,Wizara ya Maliasili na Utalii na watoa mada kutoka Chuo Kikuu cha Dar es salaam,mgeni rasmi Kaimu  Mkuu wa Wilaya ya Tunduru .Ngollo Malenya ameipongeza Wizara  kwa kufanya kongamano hilo kwa mara ya kwanza katika wilaya ya Tunduru.


Licha ya kauli hii vitendo vya ukatili wa watoto wadogo vimekuwa vikiripotiwa mara kwa mara ambapo vimeacha kumbu kumbu mbaya kwa jamii hasa yenye watoto waliofanyiwa ukatili.




Katika kongamano hilo mapendekezo mbalimbali yalitolewa ikiwemo  mapendezo ya kurejeshwa hapa nchini malikale zote za Mkoa wa Ruvuma  zilizopo nje ya nchi na wanafunzi katika shule za sekondari na vyuo kila
mwaka kuhakikisha wanashiriki kikamilifu kwenye matamasha ya mila  na  utamaduni ili kurithisha historia ya Tanzania.



Ni zairi kuwa kuna umuhimu mkubwa wa kuenzi  mila na  Desturi za Mababu zetu kwani  zimesaidia kuwa na taifa lenye amani,upendo na mshikamano nalimesaidia kuwana wananchi wenye umoja,ambapo kwenye matamasha hayo kumesaidia pia  kujenga  urafiki       inakuweza kujifunza  mambo mbalimbali ya kale, pamoja nakuelekezana vyanzo vya maendeleo kiuchumi


katika kongamano hilo Mada mbalimbali ziliwasilishwa zikiwemo kutoka kwa wahadhari wa chuo kikuu cha Dar es salaam na Wataalam wa Makumbusho ya Taifa zikiwemonafasi ya ndumba katika vita,urithi na utamaduni wa wangoni na utamu wa historia ya Mkoa wa Ruvuma.


Kilele cha miaka 117 ya kumbukizi ya mashujaa 67 wa vita ya Majimajikinatarajiwa kufanyika Februari 27,2023 katika Makumbusho ya Taifa ya Majimaji mjini Songea ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri wa
Maliasili na Utalii.


Hivyo Basi kuna haja ya Wazazi walezi,pamoja na Jamii kwa ujumla kuenzi kwa vitendo matamasha  haya kwa kufata mila na desturi za mababu zetu ili tuwe na jamii salama na kuweza kuwalinda na manyanya,Ukatili wa kingono watoto wetu kwa ajili ya urithi wa taifa la kesho.


                        mwisho.





Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch