Skip to main content

UWT YATOA ONYO KWA WANAWAKE UNYANYASAJI WATOTO


 


NA MARYAM SALUM, PEMBA

MWENYEKITI wa UWT Taifa Mary Pius Chatanda amewataka wanawake wenzake kuacha tabia ya kuwanyanyasa  na kuwatelekeza watoto kwani hilo sio jambo la busara kwa jamii na hata mbele ya Mungu.

Wito huo ulitolewa Machi 8, 2023 na Mwenyekiti huyo katika Kiwanja chakufurahishia watoto kilichopo Tibirinzi Chake Chake kwenye wiki ya siku ya mwanamke Duniani ambapo huadhimishwa kila ifikapo machi 8 ya mwaka.

Alisema kuwa suala la malezi kwa  watoto sio la mzazi mmoja ni jukumu la kila mmoja ndani ya jamii ili kuondosha changamoto mbali mbali zinazoweza kujitokeza.

Alieleza kuwa sio jambo la busara kwa mzazi kutupa mtoto ama kutelekeza mtoto kwa sababu tu yakukosa huduma ama mahitaji kutoka kwa mwenza wake.

“Tusitupe watoto kwani hatujui hapo mbeleni mtoto huyo unaemtupa atakuja kuwa nani katika jamii, hivyo tulee watoto wetu kwa kila hali ili kuwaepusha na vitendo vya ukatili wa Kijinsia ambao umeshamiri ndani ya jamii zetu,” alisema Mwenyekiti huyo.

Alifahamisha kuwa siku ya wanawake Duniani yalianza kutimiza miaka  112 tangu kuasisiwa kwake, ambapo kwa Tanzania ilianza mwaka 1911, kufuatia maandamano ya wanawake wafanyakazi wa sekta viwandani nchini Marekani ambapo waliandamana na kupinga mazingira duni ya kazi kama vile ukosefu wa huduma za kijamiina vitendo vya unyanyasaji.

Alisema kuwa suala la Ukatili wa Kijinsia ni suala la kupambana nalo kwa kushirikiana pamoja ili kuhakikisha halipati nafasi.



“Wapo akinamama wengi hupigwa na waume zao, na pia wapo watoto wadogo hutelekezwa na wazazi wao ama familia zao kutokana na sababu mbali mbali ambazo hazina msingi,” alieleza mwenyekiti huyo

Alifahamisha kuwa kufuatia hali hiyo mnamo mwaka 1977 Umoja wa mataifa ulithibitisha azimio lililozitaka nchi wanachama kuadhimisha siku ya wanawake ifikapo machi 8 ya kila mwaka nakuenzi mchango wa wa wanawake katika ujenzi wa Taifa husika.

“Hapa Tanzania siku ya mwanamke Duniani ilianza kudhimishwa mwaka 1997, hivyo tunaendelea kudhimisha kila mwaka katika Mikoa na kitaifa ambapo sherehe hizi huadhimishwa kila baada ya miaka mitano, alifahamisha.

Alisema  kuwa sherehe hizi ni  tathmini niutekelezaji wa sera mpango wa mikakati na miongozo mbali mbali  itakayo faa iliyoandaliwa na kwa ajili yakuleta usawa wa kijinsia na uwezeshaji wa wanawake, mfano ilani ya CCM ya mwaka 2020 – 2025 sura ya 9 imeeleza  bayana kwamba kuanzishwa kwa madawati ya jinsia na watoto katika vituo vya kulelea watoto.

“Hivyo kila mmoja wetu anaona wazi jinsi wanavyofanya kazi katika madawati hayo, hivyo niwaombe wananchi kutoa mashirikiano katika kupiga vita ukatili wa Kijinsia”, alieleza.

Alifahamisha kuwa kumekuwa na shida katika suala zima la ukatili na udhalilishaji wa kijinsia kwa wanawake na watoto ni jambo  ambalo lipo miongoni mwa familia, wanawake wapo wengine wanapigwa mpaka unashangaa kutokana na kipigo kama vile anapigwa nguruwe.

“Lakini wapo wengine pia wanawanyanyasa watoto wao, kwakuwaacha watoto na kujilea mwenyewe jambo ambalo linapelekea mtoto huyo kushinda mitaani, barabarani, kitu kinachopelekea  sura mbaya nchini,” alifahamisha Mwenyekiti Mery.

Aidha aliwataka  wanawake na walezi kwa ujumla kurudi kwa Mungu wao kwa kuswali na kuomba dua, ili kuweza kulea watoto wao kwa misingi mizuri na yenye maadili kwa maendeleo.

“Tanzaznia tumeingiliwa na matatizo makubwa ya ubakaji, ya ulawiti, tumeingiliwa na mataifa kutoka nje hadi wengine wameanzisha skuli kwa masuala hayo hata Wizara ya Elimu imegundua hilo, hivyo tuswali ili tuondokane na mambo maovu,” alisema.



Wakati akimkaribisha Mwenyekiti wa UWT Taifa katika hafla hiyo Makamu Mwenyekiti wa  UWT Zainab Khamis Shomari(MNEC), alisema kuwa lengo la kuchaguliwa kuwa viongozi kwenye Jumuia ni kuimarisha Jumuia, Kiuchumi Kisiasa na Kimaendeleo.

“Hivyo nafasi mliotupatia tutaiheshimu tutailinda kwa kadri ya uwezo wetu hivyo tunaomba mashirikiano yenu ili tuweze kufikia malengo, na kutekeleza majuku yale ambayo katiba ama kanuni ya UWT inavyowaongoza,” alisema.

Alieleza kuwa kutokana na dhamana walizopatiwa ndani ya Jumuia watafanya kazi bega kwa bega  na  viongozi wenzao pamoja na wananchama katika kuhakikisha wanaiweka ccm madarakani pale ifikapo 2025.

“Sisi akinamama tupo wengi kwa mujibu idadi ya Sensa ya mwaka huu na ndio wapiga kura wakubwa na wengi, hivyo ifikapo 2025 tuone kwamba asilimia hiyo imekwenda kwa mwanamke mwenzetu katika kumchagua kuwa Rais,” alieleza.

Hivyo aliwataka akinamama wa Jimbo la Chake Chake kuhakikisha wanachangamkia fursa mbali mbali zinazotolewa na Serikali katika kujikita zaidi kwenye masuala mbali mbali ya kimaendeleo kwa maslahi ya taifa.

Kwa upande wake Naibu Waziri Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Anna Athanas Paul alieleza mwaka huu wameweza kupokea jumla ya kesi 1360  za ukatili wa Kijinsia.

“Hivyo  kutokana na idadi hii kwa mwaka huu tunahitaji mashirikiano kutoka kwa jamii ili kupinga vitendo hivyo,” alifahamisha Naibu Waziri huyo.

Nae Katibu Mkuu wa UWT Philis M.Nyimbi(MNEC), alifahamisha kuwa mkusanyiko wa wanawake katika kuadhimisha siku ya wanawake duniani ni kuthamini mchango uliotolewa na wanawake wenzao katika kupinga ukatili na unyanyasaji wa kijinsia duniani.

Mapema Naibu Katibu Mkuu Zanzibar  Tunu Juma Kombo alisema kuwa lengo la siku ya wanawake duniani ni kufikia kwenye malengo yakimaendeleo.

Hata hivyo aliwataka  wanawake wenzake siku hiyo sikusherehekea tu pekee, pia ipo haja kutoa mashirikiano yakuhakikisha wanapambana kupiga vita vitendo vyote vya ukatili wa kijinsia kwa wanawake na watoto, ili kufikia malengo.

                                         MWISHO.

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch