NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, amedhamiria kwa vitendo kuleta maendeleo ya
kiuchumi kisiwani Pemba.
Na ndio maana, anachukua
juhudi mbalimbali kuhakikisha wananchi wa Pemba, wanakuwa na maisha bora
kiuchumi, kwa kuendelea kuwapelekea miradi ya kimaendeleo ya kimkakati.
Lengo ni kuona kwamba,
kila mwananchi anajiajiri na kuajiriwa kupitia fusra za kiuchumi, ambazo zinaendelea
kuletwa na Dk. Mwinyi katika kila sekta.
Hayo ni ya kujivunia
katika kisiwa hiki, kwani kinaenda kufunguka na kuleta maendeleo endelevu kwa
wananchi wake.
Moja ya miradi mikubwa ambayo
itakuza uchumi wa wananchi kisiwani Pemba, ni ujenzi wa bandari za kitaifa ambazo
zitawaingizia kipato wananchi, kwa namna moja ama nyingine na kupata maendeleo.
Katika ahadi zake Dk.
Mwinyi alizoziweka kwa wananchi kwa ajili ya kukuza kipato chao, ni ujenzi wa
Bandari ya Shumba Mjini, iliyoko wilaya ya Micheweni mkoa wa kaskazini Pemba.
Bandari hiyo ni kiungo
muhimu kati ya wananchi na wafanyabiara wa Pemba, pamoja na wale wa Mombasa
nchini Kenya, hivyo uchumi utaimarika kwa wananchi na serikali kwa ujumla.
Dk. Mwinyi anasema, moja
kati ya vitegauchumi kisiwani Pemba, ni kujenga bandari za kisasa, kama inayojengwa
Shumba Mjini, ambayo ni miongoni mwa tegemeo kubwa la kukuza uchumi.
Rais
huyo, aliahidi kuendelea kuimarisha miundombinu ya bandari ya Shumba, ili
kupunguza gharama za maisha na bei za vyakula, ambazo zimekuwa zikiwakabili
wananchi.
Serikali
ya awamu ya nane, imeimarisha bandari hiyo ambayo itakuwa ni bandari kuu kwa koa
wa askazini Pemba, kwani meli kubwa za nje zitafunga gati moja kwa moja.
Bandari
ya Shumba Mjini, itaongeza ufanisi wa upokeaji wa mizigo na bidhaa kutoka
Tanzania Bara na nje ya nchi, ikiwemo Mombasa Kenya, jambo litakalosaidia kwa
kiasi kikubwa, kupunguza gharama za chakula kisiwani humo.
Anasema,
pia bandari hiyo ni hatua muhimu ya kupunguza gharama za usafirishaji wa bidhaa
muhimu, hatua ambayo itapelekea kushuka kwa bei za vyakula na bidhaa nyingine.
“Tunatambua
changamoto kubwa ya gharama za usafirishaji wa bidhaa kutoka Unguja kuja Pemba,
ambayo inachangia kupanda kwa bei za vyakula, na bidhaa, hivyo kupitia bandari ya
Shumba itakuwa mwarubaini wa hilo,’’anasema.
Yeye
ametekeleza kwa vitendo, yale aliyowaahidi wananchi, wa kuifungua Pemba
kiuchumi, kwa sababu bandari ya Shumba, itakuwa kubwa ambayo meli za mizigo
zitaegesha hapo.
Eneo
jingine ni kwamba, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Hemed Suleiman Abdulla
hivi karibuni alipoitembelea bandari hiyo, alisema utakapokamilika mradi huo, utafungua
fursa za kiuchumi kwa wananchi wa Micheweni.
Akasema
bandari hiyo, ina umuhimu mkubwa wa kiuchumi, hivyo itajenga ustawi bora wa
maisha ya wananchi na kuingiza pato kwa serikali.
Maana
bandari hiyo itafungua uchumi wa wananchi kisiwani hapa, kwa kuzalisha ajira na
kukuza biashara, jambo ambalo litaimarisha pato la mtu mmoja mmoja na taifa kwa
ujumla.
“Bandari
hii, itakuwa na viwango vya kimataifa, hivyo moja kwa moja itakuja kunyanyua
uchumi wa wananchi wa maeneo haya ya Shumba Mjini, wilaya ya Micheweni na Pemba
kwa ujumla,” alieleza.
Akafafanua
kuwa, bandari hiyo itaongeza ajira kwa vijana wa bodaboda, kuimarika kiuchumi
kwa wajasiriamali, wanaouza vyakula, na wavuvi kwa kupata bei nzuri ya samaki.
“Wananchi
wa maeneo haya watanufaika kwa namna moja ama nyengine, mara bandari hii
itakapoanza kazi, hivyo ni hatua nzuri iliyochukuliwa na Dk. Mwinyi katika
kuimarisha kipato cha wananchi,”anaeleza.
Makamu
huyo aliuwagiza uongozi wa Shirika la Bandari Zanzibar (ZPC), kuhakikisha
miamala bandarini hapo, inafanyika kwa kutumia mifumo, ili kudhibiti upotevu wa
mapato.
“Mapato
ya serikali ni muhimu, kwa sababu ndio inayosaidia kujenga miradi mikubwa ya
kimaendeleo kama huu, na kuwanufaisha wananchi moja kwa moja,” anaeleza.
Naibu
Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Zanzibar Badria Atai Massoud anasema, bandari hiyo
itaiwezesha Zanzibar, kuwa kitovu cha biashara kwa ukanda wa Afrika Mashariki.
Jingine
akasema, itakapomalizika, itachangia kuimarika kwa utalii, kukuza uhusiano
mwema na mataifa jirani.
“Kwa
kweli Dk. Mwinyi ana maono ya mbali na ndio maana, akajenga bandari hii, ili
kuekeza na dhamira yake ya kuleta maendeleo Pemba, inakwenda kutimia si muda
mrefu,”anasema.
Naibu
huyo, anawashukuru wananchi wa Shumba Mjini, kwa kukubali kupisha ujenzi wa
bandari hiyo, na kwa ushirikiano mkubwa, wanaoendelea kuutoa katika kipindi
chote cha ujenzi.
Mshauri
Elekezi kutoka Kampuni ya Anova Consulting LTD, Mhandisi Serafina Michael
anasema, bandari hiyo inatarajiwa kutoa huduma ya usafirishaji wa abiria na
mizigo, na itahudumia takribani abiria 1,500 kwa wakati mmoja.
Maana
kwa awamu ya kwanza ujenzi wa bandari hiyo, utajumuisha jengo la abiria, gati,
diko kwa ajili ya wavuvi, msikiti, ambapo hadi kukamilika kwake litagharimu
shilingi bilioni 11.6.
WANANCHI
Hussein
Rashid Hussein, anaishukuru serikali ya Zanzibar, kwa kuendelea kujenga miradi
mbalimbali ya maendeleo, ambayo inakwenda kustawisha maisha yao na kuwakwamua
na umasikini.
“Tumeona
maendeleo makubwa yaliyofanywa na yanayoendelea kufanywa na Dk. Mwinyi, hivyo tunajivunia,
kwani badari hii itaongeza ajira kwa vijana wetu,” anaeleza.
Mwananchi
Shaame Ali anasema, kuwepo kwa bandari hiyo, kutawasaidia kupata usafiri wa
uhakika na usalama, hivyo watajiamini katika safari zao.
“Kwa
sasa hatotumia tena bandari bubu kama ilivyokuwa zamani, kwa sababu bandari
itakuwa nay a uhakika na usalama kwetu,’’anasema.
Asha
Shoka mkaazi wa Micheweni anasema, bandari hiyo pia itawanufaisha
wafanyabiashara, kwani mizigo yao, itakuwa salama na itakuja moja kwa moja
kwenye bandari hiyo.
“Bei
zikiwa nafuu, biashara itauzika haraka na kwenda kuchukua mzigo mwingine, hivyo
kipato chetu kitaongezeka kwa muda mfupi, na maendeleo yatapatikana,” anasema.
Mwananchi
Bijuma Haji anasema, kupitia bandari hiyo, serikali itapata mapato ambayo yatawasaidia
kujengewa miradi mikubwa na kimkakati, ambayo inawanufaisha moja kwa moja.
Bandari
ya Shumba Mjini iliyopo wilaya ya Micheweni, ni miaongoni mwa vipaombele vya
Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi, kupitia bajeti yake mwaka wa fedha 2025/2026.
Bajeti
hiyo iliyoeleza kuwa, itaimarisha miundombinu ya bandari, ikiwemo kuanza kwa
ujenzi wa bandari hiyo.
Hayo
yalifahamaika, kwenye hotuba ya makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka 2026/2027
kwa bandari ya Mangapwani, Ujenzi wa bandari ya abiria na mizigo Maruhubi,
ujenzi wa bandari ya shumba Mjini, uimarishaji wa bandari ya Mkoani na ujenzi
wa bandari kavu Maruhubi.
MWISHO.
Comments
Post a Comment