Skip to main content

WASICHANA NA ELIMU YA JUU, VIGINGI NA MASHIMO YA KUWAKATISHA TAMAA YAZIDI

 

NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@

RIPOTI ya Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto ‘UNICEF’, lile la masuala ya wanawake, UN-Women na shirika la Plan International, inaonesha idadi ya wasichana wanaoandikishwa skuli, kwa sasa ni kubwa kuliko wakati wowote.

Ripoti hiyo iliotolewa mwaka 2020, inaeleza idadi ya wasichana watoro skulini tangu mwaka 1995 imepungua na sasa wasichana wana fursa ya kusoma skuli za sekondari, kuliko wavulana.

HALI ILIVYO NCHINI

Mitandao inaripoti, kiwango cha wanafunzi wanaojiunga na elimu ya sekondari nchini Tanzania ina uwiano nzuri, ambapo wasichana hufikia karibu nusu ya wanafunzi wanaosajiliwa.

Hata hivyo, kutoka elimu ya msingi hadi sekondari kwa ujumla asilimia 56 ni ya wasichana, huku asilimia 34 pekee ndio wanaomaliza elimu ya sekondari.

Huku mitandao ikiripoti, hata Zanzibar kunauwiano mzuri wa wasichana wanao jiunga na masomo ya sekondari, kati yao na wavulana.

Idadi ya wanaomaliza na kufaulu ni pungufu ikilinganishwa na wavulana, kwa kila mwaka.

Wakati dunia ikishuhudia ongezeko la idadi ya wasichana wengi skulini wanaoingia sekondari, inashuhudia idadi ndogo ya wasichana wanaomaliza kwa mafanikio.

Hii inaonyesha uwepo wa vikwazo mbalimbali vinavyowakabili wasichana, katika safari yao ya utafutaji wa elimu hasa sekondari, ambavyo ni sababu ya kutofikia malengo yao.

Kwa mujibu wa ripoti za UNESCO na UNICEF wasichana ni miongoni mwa waathiriwa wa unyanyasaji, ukatili wa kingono, kimwili na kisaikolojia wanapokuwa maskulini au maeneo ya karibu.

Huku aina hizi za udhalilishaji zikiathiri zaidi ya watoto na vijana millioni 200 ulimwenguni kote (wasichana na wavulana).

 SASA CHANGAMOTO NI ZIPI

Khansaa Ali Makame ni mwanafunzi wa kidato cha pili skuli ya sekondari ya Mitiulaya anasema, moja ni kutembea umbali mrefu, katika kuzifikia skuli hasa za sekondari.

Anaeleza hili, husababisha kukutana na vishawishi vingi wanapokuwa njiani, ambavyo maranyingi, hupelekea udhalilishaji.

“Moja ya changamoto ni kutembea umbali mrefu tunapokwenda skuli, hili baadhi ya watu huchukulia kama fursa ya kufanyiwa vitendo vya udhalilishaji kwa kutushawishi kwa ahadi za ‘lift,’’ anaeleza.

Anasema mwisho wake husababisha ubakwaji au mimba za umri mdogo na kupelekea kukatisha masomo na kuzima ndoto zao.

Khadija Said Mattar mwanafunzi wa kidato cha tatu skuli ya sekondari Chasasa Wete, anaoba lugha chafu na za kukatisha tamaam kutoka kwa watu mbalimbali, ni changamoto nyingine kwao.

Tena hata wakiwa kwenye gari, mara nyingi watu huzungumza nao kwa lugha tofauti na abiria wingine, huku lugha hizo zikionyesha kutokuthamini utu na heshima yao.

“Wasichana tunachangamoto nyingi katika juhudi zetu za utafutaji elimu, binafsi nimewahi kutolewa maneno makali na yenye kuumiza na watu tofauti kwa zaidi ya mara moja,’’ananikumbusha.

Mwanafunzi Bilha Khamis Suleiman wa kidato cha nne skuli ya sekondari Mitiulaya, anaeleza changamoto nyengine ni wazazi kuwatwisha wasichana majukumu ya nyumba.

Ansema imeshazoeleka msichana anapofika sekondari wazazi wengi hubadili muelekeo, badala ya kumuandaa aelimike, huanza kuwaandaa kuwa mamama wa nyumbani.



Mundhir Maalim Omar mwanafunzi wa kidato cha tano skuli ya sekondari Chasasa Wete Pemba, anasema amewahi kushuhudia mwanafunzi mwenzake, tena msichana akifanyiwa udhalilishaji kwa kuitwa jina kwa aina ya maumbile yake.

Anasema alimshuhudia msichana huyo akipoteza furaha na kujiamini kwake kwa siku kadhaa kila anapo kuwa darasani.

WAALIMU WANASEMAJE

Khadija Bakari Sharifu, Msaidizi Mwalimu Mkuu skuli ya Sekondari Mitiulaya anasema, changamoto za kifamilia, kama utelekezwaji ni miongoni mwa changamoto inayowakabili wasichana wa sekondari kutofikia ndoto zao.

Anaeleza kuwa, hii huwakumba baadhi ya wanafunzi  wanaotelekezwa na kulelewa na watu wengine au mzazi mmoja.

Mwalimu Salum Ali Yussuf, anaeleza bado wapo wazazi na walezi, ambao huona ni hasara kubwa kuwasomesha watoto wa kike, kwa sababu wanahofia kupoteza gharama zao, jambo ambalo sio sahihi.

“Baadhi ya wazazi au walezi wanaamini watoto wao wa kike hawana haki ya kupata elimu ya juu, hivyo huamua kuwaozesha mapema, na hii ndio changamoto kubwa kwa wasichana,’’ anaeleza.

USTAWI WA JAMII   

Salma Saleh Hamad Afisa ustawi wa Jamii Wilaya ya Wete, anikiri kuwa wasichana ni watu wanaopitia changamoto kadhaa, ikiwemo za udhalilishaji.

Kumbe wakiwa sekondari, vishawishi huwa vingi kwao na kupelekea udhalilishaji wa aina mbalimbali ikiwemo, kubakwa na kupata mimba wasizozitarajia.

Anaongeza wasichana hasa wa sekondari wanapaswa kuangaliwa kwa karibu na familia zao ili kupunguza hili.

Anasikitishwa na wazazi na walezi wanao kubali suluhu za kifamilia na sio kisheria, pale watoto wao wanapopewa ujauzito au udhalilishai mwingine.

Safia Salim Said, yeye ni Mratibu wanawake na watoto shehia ya Kisiwani wilaya ya Wete,  anasema wasichana hasa wakishafika sekondari, hubebeshwa majukumu ya familia na kupoteza mwelekeo wa elimu ya juu.

Anasema hali hii kwa kiasi kikubwa, hupelekea wasichana kushindwa kufanya vizuri katika masomo na wengi wao hubakia nyumbani na kisha kuolewa.

MIKAKATI YA KUKABILIANA NA HILI

Mwanakhamis Hafidh Juma wa Kizimbani Wete Pemba, anasema wamekuwa wakiwasaidia wasichana jinsi ya kukabiliana na changamoto hizo, ikiwemo ya vishawishi.



Msaidizi Mwalimu Mkuu skuli ya sekondari Mitiulaya, Khadija Bakar Sharif anasema, wanaweka mahusiano mazuri, baina yao na wanafunzim ili kubaini changamoto wanazopitia.

Afisa ustawi wa Jamii wilayani humo, Salma Saleh Hamad, anasema ustawi wa jamii kwa kushirikiana na wadau wingine, wamekuwa wakiwaelimisha wasichana hao.

Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania Zanzibar -TAMWA Zan kupitia Afisa Programu wa kupambana na ukatili  na  unyanyasaji, Asiya Hakim, ametahadharisha juu ya changamoto zinazo wakumba wasichana hasa wakiwa sekondari katika kutafuta kwao elimu.

Anasema katika kupunguza athari hizo, TAMWA imewajengea uwezo waandishi wa habari, kuripoti  matukio ya udhalilishaji, hasa kwenye sehemu ambazo hazipewi kipaumbele ikiwemo, skuli na vyuoni.

Hili linatekelezwa kupitia Mradi wa ‘Tunaweza Pamoja’ unaotekelezwa na UN- Women kwa kushirikiana na TAMWA Zanzibar, hasa kwa wilaya za Wete na Micheweni kwa Pemba.

 SERIKALI KUU INAFANYA NINI

Ofisa Mdhamini wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Pemba Mohamed Nassor Salim, anasema katika kutatua changamoto za wasichana, wizara inajenga skuli katika maeneo ya karibu.

 “Tunajenga skuli kwenye maeneo ya karibu, ili wanafunzi wasitembee umbali wa zaidi ya kilomita tatu au tano, ili wasipite katika maeneo hatarishi,’’anafafanua.

Anafahamisha kuwa, wizara inatoa mafunzo ya stadi za maisha kwa wanafunzi, kuanzia darasa la sita, ili wanapofika sekondari, wawe wamejitambua na kujielewa.

Kumbe hilo, humuwezesha mwanafunzi kujua mabadiliko yake ya kimwili na kumjenga kuyaelewa, ili kukabiliana na changamoto zitokanazo na mabadiliko hayo.

Mkuu wa mkoa wa kaskazini Pemba, Mgeni Khatibu Yahya anasema, serikali ya mkoa kupitia idara ya ustawi, imekua ikiwasaidia wanafunzi wenye mazingira magumu, ili kuhakikisha wanaepukana na changamoto zinazowakabili.  

Eeneo jingine, Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Anna Athanas Paul inasema, vipaumbele vyao kwa mwaka 2026/2027 ni pamoja na kukuza utekelezaji wa mpango wa pili wa kitaifa, wa kupambana na ukatili na udhalilishaji.

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeridhia uwepo wa sheria, kanuni na mikataba ya kikanda na kimataifa inayotetea haki za wanawake na wasichana.

Miongoni mwao ni mkataba wa umoja wa mataifa wa kupambana na ukatili dhidi ya wanawake wa mwaka 1993.

TAKWIMU

Takwimu za mwaka 2024 za Shirika la Afya Duniani (WHO), zinaonyesha mwanamke mmoja, kati ya watatu, wamewahi kufanyiwa ukatili, katika kipindi cha maisha yake.

Kwa mujibu wa takwimu za ukatili na udhalilishaji wa kijinsia Zanzibar, zilizotolewa na Ofisi ya Mtakwimu mkuu wa serikali,  mwaka 2024 kulikuwa na 1,809 ya ukatili na udhalilishaji wameripotiwa.

Takwimu hizi zinaonyesha waathirika wengi walikua watoto ambao ni asilimia 84.3 ikifuatiwa na wanawake ambao ni asilimia 11.7.

Aidha utafiti uliofanywa na shirika lisilo la kiserikali, linaloendeleza usawa wa ukuaji wa kiuchumi na kijinsia katika sekta isiyo rasmi (EFG), Tanzania 2017, unaonyesha wanawake wanakumbana na viwango vya juu vya ukatili na udhalilishaji katika harakati zao za kiuchumi.

                                      MWISHO.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...