Skip to main content

NAIBU WAZIRI AELEZA HATUA ZA SERIKALI KUIMARISHA USTAWI WA MTOTO

 


NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@

SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imesema inaendelea kuchukua hatua mbalimbali za kuimarisha ustawi na ulinzi wa watoto nchini.

Hayo yameelezwa na Naibu Waziri wa wizara hiyo Zawadi Amour Nassor, wakati akifungua kongamano la maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika, leo tarehe 16 Juni 2026 katika ukumbi wa ZSSF Tibirinzi Chake chake Pemba.

Alisema hatua hizo ni pamoja na kuimarisha mifumo ya ulinzi wa mtoto,  kuendeleza kampeni za kupinga ukatili dhidi ya watoto, kuimarisha huduma za afya na lishe, kuhamasisha malezi chanya pamoja na kuendeleza ushiriki wa watoto katika masuala yanayowahusu.

"Serikali inaendelea kuchukua hatua mbali mbali za kuimarisha ustawi na ulinzi wa watoto, ikiwa ni pamoja na kuimarisha mifumo ya ulinzi wa mtoto, kuendeleza kampeni za kupinga ukatili dhidi ya watoto, kuimarisha huduma za afya na kuhamasisha malezi chanya" alisema.

Alieleza hatua hizo kwa pamoja zinalenga  kuimarisha ustawi wa mtoto na jamii kwa ujumla, jambo litakalo jenga taifa bora na lenye nguvu hapo baadae.

Alisema kaulimbiu ya maadhimisho ya mwaka huu inayosema “Linda Mtoto wa Afrika: Mpe Afya Bora na Maisha Bila ya Udhalilishaji”, inajumuisha upatikanaji wa  afya ya mwili, afya ya akili, lishe bora, malezi yenye upendo, elimu bora, mazingira salama na fursa za kushiriki katika masuala yanayomhusu, ambavyo kwa pamoja ni chachu ya ustawi wao.

"Kaulimbiu hii inatukumbusha kuwa mtoto mwenye afya bora na anayeishi katika mazingira salama yasiyo na aina yoyote ya udhalilishaji ana nafasi kubwa ya kukua, kujifunza, kufanikiwa na kuchangia maendeleo ya taifa pamoja na familia kwa ujumla", alisema.



Naibu Waziri huyo alendelea kueleza kua wizara  kwa kushirikiana na wadau wa watoto imeona ni vyema kuwa na kaulimbiu inayoakisi masuala ya Afya na upatikanaji wa huduma za Maji safi na salama, ili kuikumbusha jamii wajibu wake juu ya hili.

Aidha alisisitiza kua,  maisha bila udhalilishaji yanamaanisha ulinzi wa mtoto dhidi ya ukatili wa kimwili, kihisia, kingono, kutelekezwa, unyanyasaji mtandaoni, ajira za watoto na mila au desturi zinazoweza kuathiri ustawi wake.

Alieleza pamoja na mafanikio yaliyopo, kuna changamoto mbali mbali ikiwemo ukatili na udhalilishaji wa watoto, baadhi ya watoto kukosa malezi stahiki, afya ya akili na matumizi yasiyo salama ya teknolojia na mitandao ya kijamii, ambapo zinazohitaji juhudi za pamoja katika kuzitatua.

Aidha alitoa mapendekezo kwa wadau wa kulinda haki za watoto kuendelea kufanya uchambuzi wa changamoto zinazochochea vitendo vya Ukatili na udhalilishaji wa Watoto na kuandaa mikakati ya pamoja ya utatuzi wa hayo.

Pia aliendelea kutoa wito kwa wadau wanaotetea haki za watoto kuweka masuala ya watoto katika vipaumbele vya maendeleo ya taifa kwa kuhakikisha sera, mipango na bajeti zinazingatia mahitaji ya watoto katika sekta zote, na kuimarisha sheria zinazolinda haki za watoto na mipango ya udhibiti wa haki hizo.



Kwa upande wake Mkurugenzi maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii,  Jinsia Wazee na Watoto Siti Abbas Ali  alisema, katika kuhakikisha ustawi wa watoto, kwa mara ya kwanza wizara imeweka bajeti ya mabaraza ya watoto, ili isaidie kuendesha shughuli zao kwa ufanisi zaidi.

Akiwasilisha mada ya wajibu wa Jamii, wazazi na skuli katika upatikanaji wa maji safi na salama kwa mtoto mkufunzi Fihim Abdalla Mohamed kutoka wizara ya Afya alisema, ni kulinda vyanzo vya maji pamoja na kuimarisha usafi na usalama wa maji hayo majumbani.

Akizungumza kwa niaba ya watoto walioshiriki maadhimisho hayo Mwenyekiti wa watoto bodi ya ushauri taifaKhamis Abdallah Mbarouk ameipongeza wizara na asasi nyengine za Kiraia kwa kuandaa maadhimisho hayo, huku akiisihi jamii iendelee kumtunza mtoto kwa ustawi wake na maendeleo ya sasa na baadae.


Kila mwaka tarehe 16 Juni, nchi za Afrika huadhimisha Siku ya Mtoto wa Afrika
.

Siku hii ilianzishwa na Baraza la Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika mwaka 1991 kwa lengo la kuwakumbuka watoto waliopoteza maisha katika maandamano ya Soweto nchini Afrika Kusini tarehe 16 Juni 1976.

Tukio lililotokea wakalipokua wakipinga mfumo wa ubaguzi wa rangi uliowanyima haki yao ya kupata elimu bora na yenye usawa.

Kwa mwaka 2026 maadhimisho hayo yamefanyika Kisiwani Pemba, ambapo watoto wa makundi mbali mbali,  wakiwemo wenye ulemavu, wanafunzi na kutoka mabaraza ya watoto walishiriki.

"Kwa pamoja, tunaweza kujenga Zanzibar na Afrika ambayo kila mtoto atakuwa salama, mwenye afya njema, mwenye furaha na mwenye uwezo wa kutimiza ndoto zake."



                                                       MWISHO

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...