Skip to main content

MRADI WA ‘PAMOJA’ WABISHA HODI PEMBA, WAANZIA WILAYA YA CHAKECHAKE KWA MAJARIBIO, WANANCHI WAUFURAHIA

 
NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

TAKWIMU kutoka Mtakwimu Mkuu wa serikali Zanzibar, zinaendelea kutishia usalama wa wanawake na watoto wa Unguja na Pemba.

Maana, kwa miaka mkitatu iliyopita, imekusanya matukio 4,991 ya ukatili na udhalilishaji, ambao wengi wa waathirika ni wanawake na watoto.

Ijapokuwa, namba inaonesha kupungua kila mwaka kwa miaka hiyo, lakini kwa juhudi za serikali, washirika wake wa maendeleo, taasisi binafsi na mtu mmoja mmoja, bado maumivu yapo.

Maana mwaka 2023, ilikusanya matukio 1,954 ingawa mwaka uliofuata, yalishuka na kuripotiwa matukio1,8 09, na mwaka jana, yakashuka tena na kuripotiwa matukio 1,228.

Utaona kuwa, mwaka 2023, matukio 1,954, yalioripotiwa, ingawa mwaka 2024 kulikuwa na mapungufu ya matukio 145, maana yalikuwa 1,809 na mwaka 2025, kukiripotiwa pungufu ya 581 kati ya yale yaliokusanywa 1,228.



Hapo sasa, ndio maana kwa Zanzibar nzima, ukiyakusanya matukio hayo kwa kipindi kuanzia mwezi Januari 2023 hadi Disemba 2025, utabaini matukio 4,991 ya ukatili na udhalilishaji yameripotiwa.

Kwa wilaya nne za Pemba, kwa kipindi hicho wilaya ya Chakechake, imekuwa ikishika nafasi ya kwanza kila mwaka, ukiwemo mwaka 2023 iliyorpoti matukio 108.

Wakati wilaya ya Mkoani ikikusanya matukio 54, Wete matukio 93 na wilaya ya Micheweni iliyoko mkoa wa kaskazini Pemba, ikiripoti matukio 43.

Mwaka 2024, wilaya ya Chakechake ilioongoza tena, kwa kuwa na matukio 113, ikifuatiwa na Wete matukio 73, Mkoani 52 na Micheweni ikishika nafasi ya mwisho kwa Pemba, kwa matukio 46.

Takwimu zikazidi kuonesha wilaya ya Chakechake kuwa, ndio inayoongoza kwa zile wilaya nne za Pemba, kwa kusanya matukio 93, kwa mwaka 2025.

Wilaya ya Wete kama kawaida, ilishika nafasi ya pili, kwa matukio 91, Micheweni nafasi ya tatu kwa matukio 54 na Mkoani ikiwa na matukio 52.

Kwa ujumla takwimu hizo, zinatoa sura ya kuwa, kwa kipindi cha mwaka 2023 hadi 2025, wilaya ya Chakechek imekusanya matukio mingi zaidi, kuliko wilaya nyingine kwa Pemba, kwa 314, wastani wa matukio 104 kwa mwaka na manane kwa mwezi.

Wilaya inayoshika nafasi ya pili na Wete, kwa matukio 261, wastani wa matukio 87 kwa mwaka, na saba kwa mwezi.

Wilaya ya Mkoani matukio 158, wastani wa matukio 52 kwa mwaka, na manne kwa mwezi na wilaya ya Micheweni ni ya mwisho kwa kuripoti matukio 143, wastani wa matukio 47 kwa mwaka na matatu kwezi.

MRADI WA ‘PAMOJA’ NA UTAFANYA NINI CHAKECHAKE



Kwa mujibu wa Mtaalamu wa Masuala la Jinsia, kupitia Mradi wa ‘pamoja’ wa kukuza usawa wa kijinsia Tanzania, Nyezuma Simai Issa, anasema Mradi huo, ni wa aina yake, na utapunguza wimbi la ukatili na udhalilishaji, pindi utakapomalizika.

Kauli hii, aliitoa hivi karibuni, ukumbi wa Samail Gombani Chakechake Pemba, wakati akielezea muhutasiri ya utekelezaji wa mradi huo, kwa Kamati teule ya wilaya ya Chakechake, ya utekelezaji wa mradi.



Anasema, jambo jipya ambalo limo ndani ya mradi huo, ni ujenzi wa vituo vinane, vya makuzi na malezi ya awali ya mtoto, ambapo kila wilaya kitajengwa kimoja.

Kumbe, lengo la kituo hicho ni kuwapa nafasi wazazi na walezi, kujiendeleza kiuchumi, wakiwa na uhakika wa malezi, kwa watoto wao.

‘’Kupitia mradi huu wa miaka mitano, jambo kubwa ambalo limo pamoja na mingine mazuri, tutajenga vituo vinane, kwa wilaya zote nane ikiwemo Chakchake, zilizopotiwa na mradi,’’anafafanua.

Jambo jingine, ni kuona kila wilaya mradi unalikarabati jengo moja chakavu, na kwa ajili ya matumizi kama, hayo ya awali.

‘’Mradi huu, pamoja na kuanza kwa ujenzi wa vituo hivyo vinane, lakini pia unapanga kukarabati majengo mingine machakavu kwa wilaya zote, ili nayo yatowe huduma za makuzi na malezi ya awali ya watoto ikiwa yapo,’’anaeleza.



Zuri zaidi, ijapokuwa Mkoa wa Mjini Magharibi, haumo kwenye mradi, lakini mradi utajenga kituo cha kitaifa cha msaada wa kisaikolojia.

Maana wapo ambao, aidha baada ya kudhalilishwa ama kufanyiwa ukatili, watazungurukwa na msongo wa mawazo, hivyo kituo hicho kitakuwa na wataalamu wa kazi hiyo.

Akizungumza kwenye mkutano huo, Mtaalamu wa masuala ya kijamii, kupitia Mradi huo, Ali Wadi Makame, anasema ndani ya mradi huo, utawapa mikopo wanawake, waliojikusanya kwenye vikundi vya ushirika.

Ingawa hayo yatakuja, baada ya kuwapa mafunzo maalum, ya jinsi ya kujikwamua na umaskini na matumizi ya fedha hizo.

‘’Mradi huu, utawapa mikopo ya fedha moja kwa moja wanawakwe walioanzisha vikundi vya ushirika na ambavyo vimesajiliwa, ili sasa iwe sababu ya kukuza pato lao,’’anabainisha.

Lakini, akawageukia waanchi wa Unguja na Pemba, na hasa ambao mradi huo unatekelezwa, kujenga ushirikiano na maafisa wao, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa mradi.

Kuhusu kanuni za maadili, anasema mradi unataka wajumbe hao kuheshimiana na kujengeana nidhamu wakati wote, wanapokua kwenye shughuli zao.

‘’Ni jambo la kawaida kwa sisi watumishi, sasa kupitia mradi huu zitakuwepo na kisha zitasainiwa na wajumbe wa kamati zote,’’anaeleza.

Kwa sasa mradi huo kwa kuanzia, unatekelezwa kwa majaribio katika wilaya za Kati kwa Unguja na Chakechake kwa Pemba.



Ingawa kisha wilaya nyingine za Kusini, Kaskazini ‘A’ na ‘B’ kwa Unguja na wilaya za Mkoani, Wete na Micheweni kwa Pemba zitafuata.

WANANCHI WA CHAKECHAKE WANASEMAJE

Baadhi ya washiriki wa mkutano huo, wanasema mradi huo ni nzuri, na umekuwa na mwelekeo wa aina ya pekee, katika kupunguza wimbi la ukatili na udhalilishaji.

Katibu wa Kamati ya kupambana na udhalilishaji wilaya ya Chakechake Rashid Said Nassor, anasema bado vitendo vya udhalilishaji vinaendelea kutokea.

‘’Kwa aina ya mradi huu ulivyolenga, utaisaidia sana wilaya ya Chakechake, ambayo kwa Pemba, ndio kinara wa kukusanya matukio mingi ya udhalilishaji,’’anasema.

Salma Khamis Haji, anasema kilichobakia ni kwa jamii, ni kutoa ushirikiano na watendaji walioteuliwa kupitia mradi huo.

Hidaya Mjaka Ali, ambae ni mjumbe wa Kamati tendaji ya Jumuiya ya wanawake wenye ulemavu Zanzibar JUWAUZA, anasema wilaya ya Chakechake, inaelekea kupata mwaroubaini, wa vitendo hivyo.





 

‘’Vitendo vya ukatili na udhalilishaji wa kijinsia vipo na vina athari, ingawa watu wenye ulemavu huwa mara mbili, hivyo ujio wa mradi wa ‘pamoja’ itakuwa dawa,’’anasema.

 

Mkuu wa wilaya ya Chakechake Mgeni Khatib Yahya, anasema elimu zaidi inahitajika kwa jamii, ili isiendelee kuwa kinara wa matukio ya udhalilishaji.

 

Mkurugenzi wa Jumuia ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake ‘CHAPO’ Mohamed Hassan Abdalla, anasema wako tayari, kushirikiana kwa karibu na watekelezaji wa mradi huo.


 


Kamanda wa Polisi mkoa wa kusini Pemba, Abdalla Hussein Mussa, anasema miradi kama hiyo ni muhimu kwa jamii, ili kujua njia za kujiepusha na vitendo vya jinai.

 

Mjumbe wa baraza la watoto shehia ya Wawi wilaya ya Chakechake Mohamed Juma Othman, anasema moja ya njia ya kupunguza matukio hayo, ni kwa wakosaji kupewa adhabu kali.

 

Mradi wa kukuza usawa wa kijinsia Tanzania ‘pamoja’ umeundiwa timu kadhaa, ikiwemo za kijinsia, uwezeshaji wanawake kiuchumi na ufuatuliajia na tathmini.


 


Jingine lililomo ndani ya mradi huo wa miaka mitano, ni kuwepo kwa mtaalamu wa mazingira, ukiwa na lengo la kukuza fursa za kiuchumi, kwa wanawake na kukabiliana na vitendo vya ukatili na udhalilishaji.

 

Mradi huu ambao unafadhiliwa na Benki ya dunia, unatekelezwa, kwenye wilaya za Chake, Mkoani, Micheweni, Wete kwa Pemba, Kaskazini ‘A’ na ‘B’, Kati na Kusini kwa Unguja.

                         Mwisho

 

 


Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...