Skip to main content

MABWENI KWA WANAFUNZI YAPUNGUZA VITISHO VYA UBAKAJI, YAWAPA UHAKIKA WA MAKAAZI

 





 NA MOZA SHABAN, PEMBA@@@@

SERIKALI ya awamu ya nane, imekuwa ikigeuza sekta ya elimu kwa vitendo, ikiwemo ujenzi wa dahalia.

Maana lengo hasa ni kuwapunguzia umbali wa kutembea masafa marefu wanafunzi, pale wanapokwenda na kurudi skuli.

Dahalia hizo, zimekuwa zikiwasaidia wanafunzi hao, katika kuongeza ufaulu na maarifa ya kujifunza, masomo yao na kupata utulivu, wa kujiepusha na vitisho vya udhalilishaji.

Maana alishasema mara kadhaa, Ofisa Mdhamini wa wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Pemba, Mohamed Nassor Salum kuwa, wamekuwa wakipokea kesi za vitisho vya ubakaji kwa wanafunzi.

Anasema, wapo wanafunzi hasa kuanzia kidato cha nne, wamekuwa wakiviziwa vichakani, iwe wanapokwenda ama wanaporudi masomoni.





‘’Mazingira haya ya ujenzi wa dakhalia, ni kuwahakikishia ulinzi wao, maana mingi yapo karibu mno na skuli, wanazosoma,’’anasema.

Anakiri kuwa, wahalifu wa ubakaji, walishazoea kutumia vichaka, ili kuwadhalilisha wanafunzi.

‘’Sasa wanafunzi wetu hasa wakike, wako salama baada ya serikali ya awamu ya nane, kuja na mpango wa ujenzi wa dakhalia,’’anasema.

Anakumbuka miaka 10 nyuma, suala la kupokea kesi za wanafunzi wa kike kuviziwa kwa kutaka kudhalilishwa, lilikua jambo la kwaida, ingawa kwa sasa wako salama.

Kwani anasema, serikali imekuwa ikiipa kipaumbele sekta ya elimu, kwa kuzimarisha dahalia zilizochaka na kuzijenga upya.

Hussein Ali Mwinyi ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Braza la Mapinduzi, alipokuwa akizindua dahalia ya wanawake mkoa wa kaskazini Pemba, alisema malengo ni kuiimarisha sekta ya elimu.



Na tayari serikali ilitenga shilingi bilioni 864 kwa mwaka wa fedha 2025/2026, ili kuendeleza miradi mbalimbali ya maendeleo.

Akaongeza kuwa, wanaowanyemelea wanafunzi iwe wakati wa kurudi ama kwenda masomoni, sasa watabakia peke yao vichakani, maana kasi ya ujenzi wa dakhalia inaendelea,

Kumbe sehemu moja wapo ya uumarishaji wa miundombinu ya elimu, ikiwemo ujenzi wa dahalia ni makakati wa sehemu ya mageuzi ya elimu.

‘’Serikali tayari imetenga kiasi hicho cha fedha, lengo likiwa ni uimarishwaji wa miundombinu ya elimu ikiwemo huo ujenzi wa dakhalia,’’anafafanua.

Dk. Mwinyi anasema kwa mwaka ujao wa fedha bajeti ya elimu, anatamani ifikie shilingi trilioni 1, ili kuimarisha sekta hiyo.

‘’Serikali imekuwa ikiimarisha miundombinu ya elimu, hivyo ni vyema kuyatunza na yaonekane katika uhaliasia wake, ili yaweze kutumiwa na wingine,’’ anafafanua.

Kwani kuna baadhi ya maeneo, wanafunzi hukosa fursa za kujisomea, wanapokwa majumbani, kwa sababu mbalimbali, hasa wanafunzi wa kike.



Kumbe anasema, uwepo wa dahalia hizo zitaongeza fursa na kuimarisha ufaulu wa wanafunzi hao, na kuwa salama na wadhalilishaji.

Tena akakazia kuwa, serikali itaendelea na utaratibu wa ujenzi wa dahalia, kila wilaya ili kuongeza idadi ya wanafunzi wanaonufaika kwa kufikia 10,00 ifikapo mwaka 2030.

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Khamis Abdalla Said, anasema dakhalia la wanafunzi hao wa wanawake skulini hapo, lilikuwa limechakaa na kuhatarisha sualama wa wanafunzi hao.

Changamoto nyingine, ilikuwa ni uchakavu na uhaba wa vyoo pamoja na hayo, halikuwa na uwezo wa kuchukuwa wanafunzi wengi.

Akasema kuwa, ingawa kutokana juhudi anazozichukua Dk. Mwinyi ndio maana akamua kuwajengea wanafunzi hao jengo hilo la kisasa.

Katibu Mkuu huyo akafafanua kuwa, sio dakhalia hiyo pekee, lakini zipo nyingine katika skuli za Kiwani, Maziwa Ng’ombe, Bubwini Misufini, Donde, Lumumba, Mikindani, Hasnuu Makame na Paje Mtule.

Katibu Mkuu huyo wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Khamis Abdalla Said, anasema dahalia hiyo, ina vyumba 12, vyoo 31 na ina uwezo wa kuchukuwa wanafunzi 288 wastani wa wanafunzi 24 kwa kila chumba.

Inasehemu maalum na ya kisasa ya kufulia, uwanja pamoja chumba cha muangalizi wa wanawake ‘matron’.

WADAU WA ELIMU

Tatu Abdalla Msellem wa Ole, anasema kumalizika kwa dakhalia kadhaa mkoa wa kaskazini Pemba, ikiwemo ya Chwaka Tumbe, ni kuwakinga wanafunzi na udhalilishaji.

‘’Unajua wanafunzi wa kike, wapo waliokuwa wakikatisha masomo, kwa hofu ya kuvuuka vichaka na kwenda skuli, ingawa kwa sasa dakhalia ni mkombozi,’’anasema.

Hija Hamad Ali, anasema dakhalia ni eneo salama kwa wanafunzi hasa wa kike, kwa kule kupata muda wa kujisomea zaidi.

Asia Hakim Makame kutoka TAMWA Zanzibar, anasema, dakhali zikisimamiwa vyema, wanafunzi wa kike, watakuwa salama na udhalilishaji.



Anasema, kuzurura zura ovyo, hasa wanapokwenda kwenye masomo ya zaida, huwa chanzo cha wao kudhalilishwa.

Anasema, serikali imefanya jambo jema na kubwa, kawajengea dakhalia za kisasa wanafunzi, wakiwemo wanawake.

WANAFUNZI WA KIKE

Mwanafunzi Asha Hamad wa skuli ya sekondari ya Chwaka Tumbe, anasema aliamua kuomba uhamisho hapo, ili kupata utulivu.

Mwanafunzi anasoma Utaani kidato cha tatu, anasema kwa sasa, wanaishi kwenye mazingira salama, hasa kwa wale waliokuwa wakiwanyemelea kwa ubakaji.

‘’Kwa sasa tuko salama, sio kawaida kuikuta skuli haina dakhali, hili ni jambo jema, maana wadhalilishaji walikuwa wanatunyemelea vichakini,’’anasema.

Aisha Hamad Mjaka, anasema ijapokua wanaishi kwenye jengo ambalo sio dakhalia rasmi, la skuli ya Maziwa Ng’ombe, ingawa utulivu umepakatikana.

Mkuu wa mkoa wa kuskazini Pemba Mgeni Khatib Yahya, anasema hayo ni mafanikio makubwa ya mageuzi ya sekta ya elimu, wakati huu wa uongozi wa Dk. Mwinyi na imeleta faraja kwa wanafunzi.

Maana mwaka 2021 kulikuwa na ufaulu wa asilimia 91. kutokana na uboreshaji wa sekta ya elimu, na kiwango hicho kimeongezeka na kufikia asilimia 100 tangu kuingia madarakani.  

Mzazi wa mwanafunzi Raudhat Abrahman Ali anasema hakika ni faraja, kujengwa kwa dakhalia katika skuli mbalimbali.



Anasema hofu yao juu ya watoto wao hasa wa kike, kwa sasa imepungua, maana wako katika mikono salama saa 24.

Hamida Haji Mzale wa Konde, anasema sasa ni wanafunzi wenyewe, kuhakikisha wanasoma kwa bidii, na kutimiza ndoto zao.

Afisa Maendeleo ya jamii wilaya ya Wete Salma Saleh Hamad, anashauri kuwa, ili wanafunzi waepukane na ukatili na udhalilishaji, dakhalia ni eneo salama.

TAKWIMU ZA MAKOSA

Miaka mitatu, Zanzibar iliripoti matukio 4,991 ya udhalilishaji yakiwemo 2,416 yaliohusisha ubakaji, takwimu kutoka Ofisi ya Mtakwimu wa serikali Zanzibar, imebainisha.

 

Ikafafanua kuwa, kati ya matukio hayo, wilaya ya Wete iliripotia matukio 261, ambapo mwaka 2023 yalikuwa 93.

Mwaka uliofauta, yaliripotiwa matukio 77 na mwaka 2025 yaliripotiwa 91, huku wilaya ya Micheweni kwa kipindi cha miaka mitatu, ilikusanya matukio 142.

Aidha, wilaya ya Wete kwa mwezi Machi pekee mwaka huu, kumesharipotiwa matukio 103 ya ukatili na udhalilishaji wa kijinsia.



Ambapo waathirika walikuwa 103, watoto wakiwa 84, sawa na asilimia 81.6, wakifuatiwa na wanawake 17, sawa na asilimia 16.5 na wanaume wawili sawa na asilimia 1.9.

MIONGOZO

Sheria ya Mtoto nambari 6 ya mwaka 2011, kuanzia kifungu cha 12 (1), kinatamka wazi kuwa, wazazi na mtu mwingine yeyote anayewajibika kisheria, atakuwa na wajibu wa kuhakikisha haki za ikiwemo ya ulinzi na majanha mbalimbali kama ya udhalilushaji, analindwa.

Kifungu cha kidogo cha 12 (2) (a), kinasisitiza kuwa, kila mzazi au mtu anayewajibika kisheria kwa mtoto, atakuwa na wajibu kuhakikisha maslahi bora ya mtoto ndiyo jambo lake la msingi wakati wote.

 

Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, kifungu 12 kinafafanua usawa wa mbele na kile cha 15 cha haki wa faragha na usalama wake.

Sheria ya Adhabu nambari 6 ya mwaka 2018 kuanzia kifungu chake cha 108 na 109, kimebainisha pindi mahkama ikimtia hatiani kwa kosa la ubakaji, adhabu yake ni kifungo kisichopungua miaka 30 ama cha maisha.

Hutuba ya makadirio ya mapato wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ya mwaka 2025/2026 ilisoma na aliyekuwa waziri Riziki Pembe Juma anasema, wizara inatekeleza mradi wa kupambana na vitendo vya udhalilishaji, unaotekelezwa kwa ushirikiano na shirika la kimataifa la UN- WOMEN. 

Kupitia mradi huo wizara imeandaa na kuzindua mpango kazi wa pili wa kitaifa wa kupambana na vitendo hivyo, wa mwaka 2025/2030 na kuandaa sera ya maendeleo ya jamii.

 

NINI ATHARI

Mwanajuma Hija Hamad, anasema ni kuwatishia ndoto zao wanafunzi, pindi wakiishi na majeraha ua kudhalilishwa akilini mwao.

Mwanafunzi Khadija Haji Makame, anasema kwanza ni kukatisha masomo na kujiongezea mzigo wa maisha hapo baadae.

Daktari Mafunda Mohamed Khamis, anasema hata kupoteza uhai, wakati mwingine huwa rahisi mtoto au msichana akifanyiwa udhalilishaji

KIPI KIFANYIKE

Mkuu wa wilaya ya Wete Abdalla Rashid, anasema ni elimu zaidi kwa wanafunzi, ili kujitoa kwenye vishawishi.

Sheikh Mohamed Issa Haji wa Wete, anasema jingine ni kuwepo kwa adhabu kali kwa wanaowadhalilisha wanafunzi.

Msaidizi wa sheria wilaya ya Wete Said Rashid Hassan, anasema elimu ya stadi za maisha, ni vyema ikowepo kila wakati kwa wanafunzi.

Kaimu Mratibu wa TAMWA-Pemba Amina Ahmed Mohamed, anasema moja ni waandishi wa habari, kuongeza elimu hasa kupitia mitandao ya kijamii.

 

MWISHO.

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...