Skip to main content

HAYA HAPA MAGUMU YA UDHALISHAJI WANAYOPITIA WANAWAKE WAJASIRIAMALI

 



NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@

UKATILI na udhalilishaji dhidi ya wanawake na wasichana unasalia kuwa kitendo cha ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu duniani kote.

Ambapo kila mwaka makadirio ya wanawake milioni 316 sawa na asilimia 11 ya wanawake wenye umri wa miaka 15 hadi 45, hukutana na vitendo hivyo duniani kote, kwa mujibu wa mitandao ya kijamii.

Udhalilishaji huo unaweza kua wa kimwili, kingono au kihisia.

Takwimu za mwaka 2024 za Shirika la Afya Duniani (WHO), zinaonyesha mwanamke mmoja, kati ya watatu amewahi kufanyiwa ukatili huo katika kipindi cha maisha yake.

Kwa mujibu wa takwimu za ukatili na udhalilishaji wa kijinsia Zanzibar, zilizotolewa na ofisi ya Mtakwimu mkuu wa serikali,  mwaka 2024 kulikuwa na 1,809 ya ukatili na udhalilishaji wameripotiwa.

Takwimu hizi zinaonyesha waathirika wengi walikua watoto ambao ni asilimia 84.3 ikifuatiwa na wanawake ambao ni asilimia 11.7.

Aidha utafiti uliofanywa na shirika lisilo la kiserikali, linaloendeleza usawa wa ukuaji wa kiuchumi na kijinsia katika sekta isiyo rasmi (EFG),Tanzania 2017, unaonyesha wanawake wanakumbana na viwango vya juu vya ukatili na udhalilishaji katika harakati zao za kiuchumi.

Hasa katika sekta zisizo rasmi ikiwemo masokoni.

Hili linaonyesha namna wanawake wanaofanyakazi katika sekta hizo wanavyo andamwa na changamoto mbalimbali.

Changamoto ambazo kwa namna moja ama nyengine, zinarejesha nyuma ustawi wao na taifa.

Kwani ripoti ya ofisi ya taifa ya takwimu (NBS) ya mwaka 2017, kuhusu hali halisi ya wanaume na wanawake wanaofanya kazi inaonyesha, idadi ya wanawake wanaofanya kazi katika sekta zisizo rasmi, ni asilimia 51, huku walio katika mashirika na serikali  ni asilimia 18 hadi 28.

Utafiti wa (EFG) pia unaonyesha hadi asilimia 96 ya wanawake, hukumbana na ukatili, unyanyasaji na udhalilishaji, katika maeneo ya kazi ikiwemo sokoni.

Ukatili huo unaweza kua wa kiuchumi, kimwili na kisaikolojia, ambao mara nyingi hufanywa na wasimamizi wa masoko na wateja.

Yote hayo hutokea kwa uwiano unaoshabihiana, katika maeneo mbalimbali,   ingawa hutofautiana, kulingana na shughuli au biashara mtu anayofanya na eneo husika.

SIMULIZI ZA WANAWAKE SOKONI

Mmoja ya wanawake waliowahi kukumbana na udhalilishaji katika soko la mjini Wete, Tahiya Said Abeid, anaefanyabiashara ya viungo, anasema, haikua rahisi kwake kuingia sokoni hapo.

Baada ya mkulima wa magimbi aliemuuzia bidhaa hiyo, kuvamia sehemu yake ya biashara na kumchukulia tungule zake, pale yeye aliposhindwa kumaliza kurudisha fedha walizokubaliana.

“Kwa vile sina mtaji wa kutosha kuna siku nilichukua magimbi kwa mkulima, ili niyauze kwa shilingi 230, 000, nikamlipa shilingi 200,000 na fedha iliyobakia, tukakubaliana avumilie kwa siku mbili, aliporudi nikawa sijaipata, hapo akavamia sehemu yangu ya biashara na kuchukua bidhaa zangu,’’alilalamika.



Maryam Mohamed Mgeni, mfanyabiasha soko la Kifumbikai Wete anasema, aliwahi kutolewa maneno machafu na yakuumiza, baada ya kuchelewa kurejesha chenji ya mteja.

Anaeleza alipokea maneno mabaya, makali, yenye kuumiza na kukatisha tamaa na kusababisha kutokwa na machozi, mbele za wenzake.

‘’Kwa udhalilishaji nilioupata siku hiyo, nililazimika kufunga biashara na kurudi nyumbani mapema, baada ya kujisikia vibaya,’’anasimulia.

Wengi wa wanawake waliozungumza na mwandishi wa habari hizi, walilalamikia hali ngumu ya uchumi, ndio inayosababisha wao kukutana na changamoto za ukatili na udhalilishaji.

Mfanyabiashara Fatma Said Ali wa soko la Mjini Wete anasema, uwepo wa masharti mengi ya upatikanaji mikopo, mwenendo mrefu wa ufuatiliaji mikopo, hiyo  na watu kukataa kuwapa dhamana ya mikopo wajasiriamali wanawake, walioko masokoni ni ukatili wa kihisia kwao.

“Ukiachia kukatishwa tamaa kwa maneno, wakati mwingine kushikwa bila ridhaa, pia hii tabia ya watu kukataa kutupa dhamana tukiomba mikopo, na pingamizi nyenginezo kwetu,’’anaeleza.

Fatma na wafanyabiashara wengine wanawake sokoni hapo wanasema, wameshawahi kuunda kikundi kwa ajili ya kuomba mikopo, ili wajiinue kiuchumi, ikashindikana kutokana na kuwepo kwa mchakato mrefu wa upatikanaji wake.

Salum Muumini, (si jina la kerasmi) anaeleza amewahi kushuhudia mwanamke aliekua mfanyabiashara wa soko la Kifumbikai Wete, miaka miwili iliopita kushikwa shikwa  bila  ya ridhaa yake.

‘’Hasa hawa chukuaji na watoaji mizigo ndani ya soko, huwa wanawadhalilisha wajasiriamali wanawake, maana huwashika na kupinga vikali,’’anasema.

Omar Haji Kassi, anasema aliwahi kushuhudia kitendo hicho kisicho cha kiungwana, kwa mwanamke aliyekuwa akiuza samakini nae kushikwa na kulazimika kwenda Polisi.

‘’Sikujua ile kesi iliishia vipi, lakini yule mwanamke hapa amehama na sikia kwa sasa yuko Unguja Fungu refu kwa biashara ya kuanika dagaa,’’anaelezea.

Ifahamike vitendo hivyo ni kinyume na matakwa ya sheria za nchi, mikataba ya kikanda na kimataifa inayosisitiza usalama wa mwanamke popote alipo.

Mfano mkataba wa kimataifa wa mwaka 1976 wa kupambana na aina zote za ukatili dhidi ya wanawake (CEDAW), katika mapendekezo namba 19 na 35, unahimiza serikali kuwalinda wanawake, dhidi ya ukatili wa kijinsia.

Ibara ya13 ya itifaki ya haki za binaadamu wanawake barani Afrika Protocol to the African Charter on Human and Peoples Rights of Women in African’ wa mwaka 2003 ulioanza kutumika rasmi 2005, inasisitiza nchi wanachama kuhakikisha ulinzi na hifadhi kwa wanawake wanaofanyakazi katika sekta zisizo rasmi.

Ifahamike kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake ni jukumu la kila mtu, ndio maana Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA–Zanzibar, imekuwa ikipinga kwa vitendo vitendo hivyo.

 Hao yenyewe imekuja na mradi wa “Tunaweza pamoja” unaolenga kupinga vitendo vya ukatili kwa wanawake na wasichana.

Afisa Programu wa mradi huo Asya Hakim Makame, ametilia mkazo umuhimu wa kuripoti na kupambana na vitendo hivyo, hasa katika maeneo yasiorasmi, kama vile sokoni.

Anasema lengo la mradi huom ni kuwajengea uwezo waandishi wa habari kuripoti  matukio hayo hasa katika maeneo yasio rasmi.

‘’Ndio maana sehemu ya mradi huu, tumeshawajengea uwezo waandishi wa habari 40, kwa Unguja na Pemba, ili kuhakikisha wanakuwa weledi kuchimbua matendo hayo.

SERIKALI

Mkuu wa mkoa wa kaskazini Pemba, Mgeni Khatibu Yahya anasema, wanawake waungane kujilinda na vitendo hivyo, kwa kuviripoti katika mamlaka husika.

Kwa upande wa wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto vipaumbele vyake kwenye bajeti ya 2026/2027, imedhamiria kupambana na ukatili na udhalilishaji, dhidi ya wanawake na watoto.

Akiwasilisha bajeti hiyo waziri wa wizara hiyo Anna Athanas Paul, anasema, wizara itawawezesha wanawake kiuchumi, ili wajitegemee lengo likiwa ni kupunguza ukatili na udhalilishaji dhidi yao.


“Wizara inafanya juhudi za ufuatiliaji wa majukwaa na vikundi vya wanawake kupitia mradi wa ‘PAMOJA’ na ‘Dk. Mwinyi Boosting fund’ ambao unakusudia kutoa mikopo ya masharti nafuu, kwa walengwa,” anaeleza.

 Aidha Rais wa Zanzibar na Dk.Hussein Ali Mwinyi, katika hutuba zake mbalimbali amekua akisisitiza kua, ukatili na udhalilishaji ni janga la kidunia, linalohitaji nguvu ya pamoja kulishinda.

Ndipo serikali ya awamu ya nane, ikaanzisha mahakama maalumu za kushughulikia kesi za udhalilishaji, ili watuhumiwa wa kesi hizo, wachukuliwe hatua.

NINI ATHARI YAKE

Mfanyabiashara wa soko la Wete Haji Juma Makame, anasema kwanza ni kudumaza uchumi wa wanawake, walioamua kujitegemea.

Mayasa Hassan Kombo wa Mtemani Wete, anasema ni kuendelea mfumo dume katika maisha ya wanawake ya kujikuza kiuchumi.

Kaimu Mratibu TAMWA Pemba Amina Ahmed anasema, ni kudhoofisha ndoto za wanawake kwenye kukuza pato lao.

Shiekh Said Ahmad Mohamed, anasema ni kuendeleza udhalilishaji wa kiuchumi kwa wanawake, katika maeneo yasio maarufu.

ZIPI NJIA KUDHIBITI HILI

Mfanyabiashara wa soko la mjini Wete Tahiya Said Abeid anasema, ni serikali na wadau wingine wa maendeleo, kuwawezesha wanawake waofanyabiashara masokoni, kwa mitaji yenye masharti nafuu.

Hamad Omar, ambae nae ni mfanyabiashara soko la Kifumbikai Wete, anasema ni elimu kwa wanaume hasa waliopo masokoni, kuhusu dhana ya udhalilishaji.

‘’Tulishazoea kuwa udhalilishaji ni ulawiti, ubakaji, lakini hata kuangushiwa bidhaa chini, matusi, kuwashika shika wanawake ni hatari kwao,’’anashauri.

 Sadri Mussa Said Msimamizi wa masoko na mazingira wilaya ya Wete anashauri, ni vizuri wafanyabiashara wanawake waliopo sokoni wawatumie viongozi wao wa masoko, kuripoti vitendo wanavyofanyiwa.

Mratibu wa wanawake na watoto shehia ya Kisiwani Wete, anapendekeza, serikali na washirika wa maendeleo, kuwekeza katika harakati za kuwasaidia wanawake, kiuchumi na taaluma.

Afisa Maendeleo ya jamii wilaya ya Wete Salma Saleh Hamad, anashauri kuwa ili wanawake waepukane na ukatili na udhalilishaji sokoni, ni lazima waripoti vitendo hivyo badala ya kuvifumbia macho.

MWISHO

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...