Skip to main content

VYAMA VYA SIASA TUMIENI MIFUMO SAHIHI SERA ZIWAFIKIE WATU WENYE ULEMAVU WA UZIWI

 



NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@

 TAASISI zinazoshughulikia masuala ya uongozi wa wanawake vimeviomba vyama vya siasa kuzingatia na kuhakikisha ushiriki wa watu wenye ulemavu katika mikutano ya kampeni zinazoendelea ili kuweza kufuatilia sera zinazotolewa na wagombea wa vyama vya siasa katika nafasi za Urais, Uwakilishi, Ubunge na Udiwani kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025.

 Taasisi hizo ambazo ni pamoja na Jumuiya ya Wanawake wenye Ulemavu Zanzibar (JUWAUZA), Jumuiya ya Mazingira, Jinsia na Utetezi Pemba (PEGAO), Jumuiya ya Wanasheria Wanawake Zanzibar (ZAFELA) na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania, Zanzibar (TAMWA-ZNZ) zimesema kuwa kuna baadhi ya vyama havijazingatia mahitaji ya watu wenye ulemavu katika mikutano yao jambo ambalo linawanyima haki yao ya msingi ya kufuatilia sera za vyama na hivyo kufanya maamuzi sahihi ya kura zao. 







 Walisema kuwa kuna baadhi ya vyama vimeshuhudiwa vikiendesha mikutano ya kampeni bila ya kuandaa mazingira rafiki kwa watu wenye ulemavu hali inayopelekea kushindwa kushiriki na kufuatilia kampeni.

 “Mikutano mingi imekosekana kwa miundombinu wezeshi,  wakalimani wa lugha ya alama, maandiko makubwa kwa wenye ulemavu wa macho, na vifaa vya msaada wa kusikia, ambapo huwanyima watu wenye ulemavu fursa ya kushiriki kikamilifu katika mchakato wa kampeni," alifafanua.

Alieleza kuwa chama kimoja tu ambacho kimeweka wakalimani katika mikutano yake na ambao huonekana zaidi wakati wa mikutano inayofanywa na mgombea wa Uraisi na hivyo katika nafasi nyengine mazingira hayo bado yanakosekana isipokuwa kwa jimbo moja tu katika mkoa wa mjini magharibi ambapo kumeandaliwa wakalimali maalum kwa ajili ya kundi hilo muhimu. 

 Alifafanua kuwa ni vyema kuiga  chama hicho ili kuhakikisha  sera ya ilani ya vyama  zinawafikia kwa urahisi,  kuweka maandiko makubwa, vifaa vya msaada wa kusikia katika maeneo yote  na wakalimani wa lugha za alama ili kujenga demokradia ya kweli.

 Kwa mujibu wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) jumla ya watu wenye ulemavu wapatao 8,021 wanatarajiwa kushiriki katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 visiwani Zanzibar.

Pia Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Watu Wenye Ulemavu (CRPD, 2006) Kifungu cha 9 kuwa nchi zihakikishe kuwa watu wenye ulemavu wanaishi kwa kujitegemea na kuweka utaratibu wa kufikia huduma zote pamoja na mawasiliano na teknolojia.

 Sheria ya Watu wenye Ulemavu Zanzibar Namba 8 ya mwaka 2022, kifungu cha 29 kinaeleza umuhimu wa watu wenye ulemavu kuweza kufikia miundo mbinu mbali mbali pamoja, taarifa, mawasiliano na haki zote za kibinaadamu na za msingi. 

 Aidha kutokana na haki walizopewa watu wenye ulemavu za kushiriki kikamilifu katika kampeni za kisiasa, viongozi wa vyama vya siasa wanawajibika kuhakikisha ushiriki huo unatekelezwa bila vikwazo kwa kuweka miundombinu rafiki katika viwanja vya kampeni, kutoa taarifa zinazoweza kufikiwa kwa urahisi, na kuwezesha upatikanaji wa usafiri pamoja na vifaa vya msaada.



 Tume ya Uchaguzi na wadau wengine wanapaswa kutoa motisha kwa vyama na wagombea wanaojumuisha watu wenye ulemavu, hatua ambayo itachochea usawa na kudhihirisha mfano bora wa demokrasia jumuishi.

 Imetolewa na JUWAUZA, PEGAO, ZAFELA na TAMWA-ZNZ kwa kushirikiana na Ubalozi wa Norway nchini Tanzania ambao ni watekelezaji wa program ya kuhamasisha wanawake kushiriki katika nafasi za uongozi.



                                                   Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...