Skip to main content

WATENDAJI 'THBUB' WAKUTANA NA WADAU MBALI MBALI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU

 




1.    01/// Kamishna wa Tume ya haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) ofisi ya Zanzibar, Khatib Mwinyichande (wa pili kulia) akizungumza kwenye kikao cha pamoja baina ya tume hiyo na Tume huru ya Taifa ya Uchaguzi INEC kilichofanyika ofisi za INEC zilizopo Wilaya ya Mjini Mkoa wa Mjini Magharibi, ikiwa ni utaratibu wa THBUB kukutana na wadau wa Uchaguzi wakiwa kwenye mwendelezo wa Uangalizi kuelekea Uchaguzi mkuu 2025 wakati wa kampeni kwa vyama mbalimbali vya siasa. Wa kwanza (kulia) ni Mratibu wa Uchaguzi Unguja (REC) Bw. Abdallah Bakar Khamis, Katibu Msaidizi THBUB Bw. Juma Msafiri Karibona (katikati), Bw. Wilfred Msagati Afisa Sheria, THBUB Unguja (wa pili kushoto) na Bitizani Kejo, Afisa Uchunguzi Mkuu kutoka THBUB Dar es Salaam.

 


2.    02/// Kamishna wa Tume ya haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) ofisi ya Zanzibar, Khatibu Mwinyichande (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na maofisa wa tume hiyo pamoja na maofisa wa Tume huru ya Taifa ya Uchaguzi INEC mara baada ya kikao cha pamoja kilichofanywa na tume mbili hizo kwenye ofisi za INEC zilizopo Wilaya ya Mjini Mkoa wa Mjini Magharibi, ikiwa ni utaratibu wa THBUB kukutana na wadau wa Uchaguzi wakiwa katika mwendelezo wa Uangalizi kuelekea Uchaguzi mkuu 2025 wakati huu wa kampeni zinazoendelea kwa vyama vya mbalimbali vya siasa.

 

3.    Timu ya maofisa wa Tume ya haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) wakiwa kwenye mwendelezo wa kukutana na wadau mbalimbali wa uchaguzi vikiwemo vyama vya siasa kuelekea uchaguzi mkuu mwezi Oktoba 2025. Pichani ni Maofisa wa THBUB (kushoto) wakiwa kwenye kikao cha pamoja na wanachama wa Chama Cha ACT Wazalendo (kulia) ofisi za ACT, Vuga Wilaya ya Mjini Mkoa wa Mjini Magharibi, hivi karibuni.

 


 

4.    Maofisa kutoka Tume ya haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB), (kulia) wakizungumza wakati wa kikao cha pamoja na Mwenyekiti wa Chama cha Wakulima Taifa (AAFP), ambae pia ni Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama hicho, Bw. Said Soud Said huko ofisi za Chama hicho Mwera, Wilaya ya Magharibi A, Mkoa wa Mjini Magharibi. THBUB inafanya mwendelezo wa kuwatembelea wadau wa uchaguzi zikiwemo Tume za Uchaguzi za ZEC na INEC, vyama vyote vya siasa wakiwemo viongozi na wadau wa vyama hivyo, THBUB inafanya zoezi maalumu la uangalizi wa uchaguzi kuelekea Uchaguzi mkuu mwezi Oktoba, 2025.





 

KUTOKA PEMBA

5.    Maofisa kutoka Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB), wakiwa kwenye picha ya pamoja baada ya mafunzo ya Haki za binadamu na misingi ya utawala bora kwa waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali kisiwani Pemba, kuelekea Uchaguzi mkuu Oktoba 2025, waliokaa katikati ni Kamishna wa (THBUB) ofisi ya Zanzibar, Khatib Mwinyichande, Afisa Mfawidhi THBUB kituo cha Pemba Bw. Suleiman Salim (kulia) na Mratibu kutoka Idara ya Habari Maelezo ofisi ya Pemba, Bi. Jamila Abdallah Salim (wa Kwanza kushoto). Mafunzo hayo yalifanyika hivi katika ofisi za THBUB zilizopo Mtaa wa Kichungwani, Wilaya ya Chachake, Mkoa wa Kusini Pemba.

 


Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...