Skip to main content

NCHIMBI AONA MBALI MIAKA 5 IJAYO CCM IKIRUDI MADARAKANI






MGOMBEA MWENZA wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi CCM Dk. Emanuel John Nchimbi amesema, katika miaka mitano inayokuja wamedhamiria kuongeza kasi ya zoezi la utafiti wa rasilimali za bahari, ili wananchi wapate maisha bora, kwani uchumi wa buluu umeleta mafanikio makubwa katika nchi.

Dk. Nchimbi ameyasema hayo wakati wa mkutano wa mkuu wa kampeni uliyofanyika katika viwanja vya Kinyasini Jimbo la Gando Wete Mkoa wa Kaskazini Pemba.

Amesema,  wanayo imani na matumaini makubwa kwamba ndani ya bahari kwa upande wa Pemba kuna rasilimali nyingi ambazo zitawasaidia wananchi kuwa na maisha bora, hivyo ilani ya CCM ya mwaka 2025/2023 imeweka wazi suala la kuongeza kasi ya zoezi la utafiti, ili kuimarisha zaidi uchumi wa wananchi.

"Pia tutaimarisha ufungaji wa samaki, vizimba vya samaki na ukulima wa zao la mwani ili kuinua kipato cha wananchi na kuwaletea manufaa katika familia zao," alisema Dk. Nchimbi.

Dk. Nchimbi alisema kuwa, anaamini kwamba chama kitapata ushindi wa kishindo, kwani wanajivunia mambo makubwa yaliyofanywa na marais kipindi kilichopita ambayo yamesababisha kuinua uchumi wa Zanzibar kwa asilimia 7.5.

"Kwa kweli uchumi umekuwa sana visiwani Zanzibar na hii ni kutokana na mashirikiano makubwa ya wananchi na wanachama wa chama cha Mapinduzi CCM, tunaona fahari kubwa kwa kazi zinazofanywa na marais wetu hawa," alisema.

Aidha alifafanua kuwa, ilani imeweka wazi suala la kuimarisha kilimo cha uzalishaji, kilimo cha umwagiliaji maji na kusema kuwa katika kufanikisha hilo ilani imeweka mkazo kwenye upatikanaji wa pembejeo, mikopo nafuu na masoko ya bidhaa, ili kuhakikisha kila siku kunakuwa na uhakika wa chakula.

Alieleza kuwa, wataendeleza amani na usalama sambamba na kulinda Muungano wa Tanzania, kwani unaendeleza umoja, undugu na kuondoa ubaguzi baina yao.

Vile vile alifafanua kuwa, wamedhamiria kujenga makumbusho ya historia ya Mapinduzi ili ifahamike na vizazi vyote vya sasa na vijavyo, kwa sababu Mapinduzi ndio yaliyomkomboa mzazibari, ndio yaliyowafanya wazanzibari wawe sawa, yameleta umoja, hivyo wanajivunia sana.

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk. Mohamed Said Mohamed (Dimwa) alisema, ikiwa watamchagua Dk. Samia basi wajue kwamba atakuwa na msaidizi mzuri ambae ni kiongozi mwenye hofu ya Mungu na yuko tayari kuwatumikia wananchi.

Alisema kuwa, maendeleo mengi yamefanywa na Serikali za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Serikali ya Zanzibar kwa kujenga majengo ya kisasa ya kutolea huduma pamoja na kuwawezesha wananchi wenye kipato cha chini kupitia mradi wa TASAF, jambo ambalo limewakomboa na maisha duni.



Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Mohamed Aboud Mohamed alieleza kuwa, Dk. Nchimbi ni mwadilifu, mwenye imani, anaependa watu na anajua mahitaji ya watu, hivyo atakuwa mshauri mzuri wa Dk. Samia.

"Dk. Mwinyi amefanya kazi ya kuwaunganisha wananchi, hivyo hakuna ubaguzi wa kidini, kijinsia, umoja na mshikamano umetawala visiwani hapa, lililobaki twendae tukapige kura ifikapo Oktoba 29 mwaka huu na tuwachague viongozi wetu," alisema Mjumbe huyo.

Mbunge mstaafu wa Arusha Sesilia Pereso aliwaomba wananchi kumchagua mama Samia pamoja na viongozi wengine wa CCM ili waongoze tena awamu ya pili kwa ajili ya kuwaletea maendeleo katika nchi.

Alisema, chama kimewaletea mama hodari, shupavu na ana sifa zote za kuongoza awamu nyengine, hivyo kila mmoja anapaswa kuweka kura ya ndio kwake ili awaletee wananchi maendeleo.

"Kazi alizozifanya mama Samia katika miaka minne iliyopita ni uthibitisho tosha kwamba ana uwezo wa kuongoza, kwa pamoja tuwapigie kura viongozi wa CCM ili watuletee maendeleo," alisema Mbunge huyo mstaafu.




Mbunge wa Jimbo la Gando Salum Mussa Omar na mwakilishi wa Jimbo hilo Maryam Thani Juma wamewataka vijana kutodanganywa na wasiopenda maendeleo bali wawachague viongozi wa CCM ili maendeleo zaidi yawafikie.

Walisema, kila kona yanaonekana maendeleo yaliyofanywa na chama cha Mapinduzi CCM, hiyo ni heshima kubwa kwa wananchi, hivyo ni vyema wakalipa fadhila kwa kuwapigia kura za nduo viongozi wa CCM.

"Nawahakikishia marais wetu watashinda kwa kishindo kwa sababu wananchi wameniambia kuwa kwa maendeleo wanayoyaona hakuna sababu ya kuikosesha kura CCM," alisema mgombea ubunge wa Gando.

                         MWISHO.



Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...