Skip to main content

UJENZI UWANJA WA NDEGE WA KIMATAIFA PEMBA, BARABARA CHAKE CHAKE -MKOANI NJIA SAHIHI KUKUZA UCHUMI

 



NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@

ILE dhamira ya Dk. Hussein Ali Mwinyi kuifungua Pemba kiuchumi kupitia uwanja wa ndege wa kimataifa, sasa imefana.

Kwani uzinduzi wa ujenzi wa uwanja huo na barabara ya Chake Chake- Mkoani, umezinduliwa rasmi Septemba25, mwaka huu, katika uwanja wa ndege uliopo Furaha Pemba.

Ni furaha kubwa kwa wananchi wa kisiwa cha Pemba, kuona kwamba kitu ambacho wamekisubiri kwa muda mrefu, sasa kinakwenda kufungua uchumi wao.

Maana serikali ya awamu ya nane, imedhamiria kufanya mageuzi ya makubwa katika sekta ya usafiri wa anga Zanzibar, kwa lengo la kuimarisha miundombinu ya utoaji wa huduma katika uwanja wa ndege wa Pemba.

 


Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Hemed Suleiman Abdulla amezindua ujenzi huo kwa niaba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, jemedari wa uchumi.

 

Makamu huyo anasema, ujenzi wa miradi hiyo ni utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020/2025 ambapo malengo ya serikali, ni kuhakikisha kuwa, Pemba inakuwa na uwanja wa ndege wa kimataifa.

 

‘’Serikali imedhamiria kufanya mageuzi makubwa, katika sekta ya anga na dhamira hiyo ilianza kwa vitendo mwaka 2023 kwa kutiliana saini na Serikali ya Hispania, lengo ni kuleta maendeleo ya kiuchumi kwa wananchi,’’ anafafanua.

 

Lengo ni kuwa na uwanja wa ndege wa kimataifa, kwa ajili ya kukuza utalii, uwekezaji na biashara ambazo zitachangia kwa kiasi kikubwa, kukuza uchumi wa mtu mmoja mmoja na taifa.

 

Hemed anafahamisha kuwa, serikali imejipanga, katika kuhakikisha barabara zote za Zanzibar zinajengwa kwa kiwango cha lami, na kuwa katika hali nzuri kwa kuhakikisha zinafanyiwa matengenezo pale inapohitajika.

 

‘’Miradi hiyo itakapokamilika itapelekea kuimarika kwa huduma za usafiri wa anga na kuifungua Pemba kiuchumi, kwa kuongezeka shughuli za kibiashara, kuimarika kwa sekta ya utalii itakayochangia kuongezeka kwa pato la taifa.

 

Makamo huyo amemtaka Mkandarasi wa ujenzi wa uwanja huo kampuni ya PROPAV INFRASTRUCTURES na mshauri elekezi Dar Alhandasah Consultant, kujenga uwanja huo ka kiwango kinachokubalika kimataifa.

 

Anakumbusha, maendeleo yoyote yanahitaji kuwepo kwa amani, umoja na mshikamano, hivyo amewaasa wazanzibari kuendelea kuidumisha amani iliyopo nchini.

 


Dk. Khalid Salum Mohamed yeye ni waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi anasema, Dk. Hussein Mwinyi amedhamiria kuifungua Pemba kiuchumi, kwa kujengwa miradi mikubwa ya maendeleo.

 

Hapa akatolea mfano kuwa, ujenzi wa uwanja wa ndege Pemba na barabara ya Mkoani -Chake Chake, yenye urefu wa kilomita 43.5.

 

Wizara ya Ujenzi inaendelea na ukarabati wa bandari ya Mkoani, ambayo itakuwa na uwezo wa kupokea meli kubwa, kutoka nje, jambo  litachochea ukuwaji wa uchumi kisiwani Pemba.

 

Akisoma taarifa ya kitaalamu Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Mawasiano na Uchukuzi Dk. Habiba Hassan Omar anasema, 

Serikali imekuwa ikichukua juhudi kubwa, kuimarisha huduma za usafiri wa anga na nchi kavu.

 

Akitaja kuwa lengo ni lile lile la kukuza uchumi wa nchi na kuwandolea usumbufu wananchi na wageni wanaofika Zanzibar.

 

Dk. Habiba anasema, utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa uwanja wa ndege wa Pemba. umeanza rasmi Novemba 2024 na unatarajiwa kuchukua muda wa miezi 36, mpaka kumalizika kwake.

 

Waziri wa Fedha na Mipango Zanzibar Dk. Saada Mkuya anaeleza katika miradi ya kimkakati aliyodhamiria Dk. Mwinyi ni uwanja wa ndege wa kimataifa kisiwani Pemba.

 

‘’Fursa hizi ndizo zinzoongeza uchumi wa nchi na watu binafsi, hivyo ni faraja kwetu, kuona maeneleo yanazidi kupanuka kisiwani Pemba,’’ anaeleza.

 






Mkandarasi wa ujenzi wa Uwanja huo ni Kampuni ya PROPAV INFRASTRUCTURES kutoka nchini Hispania na Msimamizi wa ujenzi ni Kampuni ya DAR AL HANDASAH CONSULTANTS kutoka Lebanon, ambapo ujenzi huo unatarajiwa kugharimu jumla ya EURO milioni 170. 

 

Ujenzi wa Uwanja huo utahusisha jengo jipya la abiria, lenye uwezo wa kuhudumia abiria wasiopungua 300,000 kwa mwaka, ikiwemo abiria wa ndani (Domestic) na abiria wa kimataifa (International) pamoja na ujenzi wa njia ya kuruka na kutua ndege (Runway), yenye urefu wa mita 2.510 na upana wa mita 45 utakaokuwa na uwezo wa kutua ndege zote za aina ya Code 4C.

 

Kwa upande wa utekelezaji wa mradi wa barabara ya Mkoani – Chake Chake yenye urefu wa kilomita 43.5, inayojengwa na Kampuni ya PROPAV INFRASTRUCTURES ya Hispania, ikisimamiwa na kampuni ya DAR AL HANDASAH CONSULTANTS, ambayo inatarajiwa kuchukua muda wa miezi 36, hadi kumalizika kwake.

 

Ujenzi wa barabara ya Mkoani- Chake Chake utagharimu zaidi ya EURO milioni 93, itakayohusisha njia za watembea kwa miguu, taa za barabarani, (streetlights) pamoja na alama za usalama wa barabarani.

 

Aambapo itakapokamilika itawarahisishia wananchi kuzifikia huduma mbali mbali za kijamii na kiuchumi kwa urahisi.

 

Mkurugenzi wa Kampuni ya PROPAV INFRASTRUCTURES Cristiano Becker anasema, wanatambua kuwa, uwanja wa ndege ni mlango mkuu na daraja la kuiuganisha Pemba na dunia.

 

Hivyo ameahidi kuwa wataujenga uwanja huo kwa viwango na ubora unaokubalika kimataifa, ili mfano kwa maeneo mingine.

 


Mkurugenzi huyo anasema, serikali imeiamini kampuni ya PROPAV INFRASTRUCTURES na kuipa mkataba wa kuujenga uwanja huo, hivyo itajenga uwanja wa ndege wenye hadhi na sifa zote.

 

Akizungumzia ujenzi wa barabara ya Mkoani- Chake Chake Christiano anafafanua kuwa, ahadi yake ni kujenga barabara hiyo kwa uaminifu mkubwa, na yenye viwango vinavyoendana na mustakbali wa Pemba.

 

Anaeleza, ujenzi wa mradi wa uwanja wa ndege wa Pemba, pamoja na barabara ya Mkoani- Chake Chake utatoa ajira zaidi ya 1,000 kwa wakaazi wa Pemba, wananchi kutoa fursa ya kufanya biashara ndogo ndogo, pamoja na mafunzo ya ujuzi kwa vijana watakaopata fursa ya kufanya kazi na kampuni yake.

 

Kwa upande wao wananchi walifurahi sana kuona uzinduzi huo na kusema, sasa unaenda kuifungua Pemba kiuchumi kwa vitendo.

 

Wanasema, Dk. Mwinyi amekuwa akifanya juhudi mbali mbali kuhakikisha wananchi wa Pemba wanaimarika kiuchumi na ndio maana amekuwa akiwaletea mambo mengi ya kimaendeleo, hivyo anahitaji pongezi.

 

Asha Hassan Juma, mwenye uleavu wa Wawi, anasema furaha zao ni kuona miundombinu kwa ajili yao imezingatiwa katika ujenzi huo.

 

Ali Haji Kombo wa Madungu, ansema sasa anaionba Pemba iko karibu kukuza pato na uchumi wake, maama milango ya bandari, barabara na uwaja wa ndege umeshapanuliwa kimataifa.

 

                                                    MWISHO.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...