Skip to main content

LAILA: MWANAMKE SHUPAVU ANAYEANDIKA HISTORIA YA UONGOZI VISIWANI

NA AMRAT KOMBO, ZANZIBAR

Kila binadamu ana malengo maishani, lakini kuyatekeleza kunahitaji mipango thabiti na ujasiri wa kipekee. Kwa Laila Rajab Khamis, maarufu kama Laila, ujasiri huo umekuwa silaha kubwa iliyomfikisha kwenye nyanja za siasa na kumuwezesha kuwa miongoni mwa wanawake wachache wanaopigania nafasi za juu za uongozi Zanzibar.

 Laila alizaliwa mwaka 1968 Kengeja, Pemba, akiwa mtoto wa tatu kati ya watoto kumi wa familia ya Mzee Rajab. Elimu yake ya awali ilifika darasa la kumi katika Skuli  ya Uwelene. kabla ya kuingia kwenye siasa alikuwa mfanya biashara wa nguo mwaka 2000.

Hata hivyo, ndoto yake haikuishia kwenye biashara pekee, bali kuandika historia ya uongozi kama mwanamke jasiri. Safari yake ya kisiasa ilianza rasmi mwaka 2008 alipojiunga na chama cha NCCR-Mageuzi na kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Jimbo la Rahaleo. 



Hatua hiyo ilimfungulia mlango kushika nyadhifa mbalimbali ikiwemo Mjumbe wa Halmashauri Kuu, Mjumbe wa Kamati Kuu, Mlezi wa chama na hatimaye Makamu Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi Zanzibar.
“Lengo langu kubwa ni kuwatetea wanawake na watoto katika masuala ya kijamii. Nimeona Rais Samia, mwanamke mwenzangu, ameweza kuiongoza Tanzania ,kwanini yeye asishiriki? Familia yake imesimama bega kwa bega naye licha ya tofauti za vyama. 

“Mimi na mume wangu kila mmoja ana chama chake, lakini hajawahi kunidharau. Hunitia moyo na kunijenga zaidi. Hata mama yangu ameridhia hatua zangu na ananiombea kila siku,” anabainisha kwa furaha. 
Laila amejijengea uwezo kupitia mafunzo ya uongozi na siasa kutoka taasisi mbalimbali za kimataifa. “Nafarijika kuwa katika chama ambacho kimewapa wanawake nafasi kubwa. Viongozi wanawake tupo sita, wanaume watatu. Hii imenitia nguvu zaidi,” anaongeza kwa kujiamini.

Mbali na siasa, Laila amekuwa mstari wa mbele kusaidia wajasiriamali wa ushonaji na vijana wa michezo. Hata hivyo, anakiri changamoto kubwa ni dhihaka kutoka kwa baadhi ya wananchi. 



“Wengine hunikejeli kwa kugombea nafasi hii, lakini sijakata tamaa. Nitaendelea kupambana kwa sababu najua wapo wanaoniunga mkono,” anasisitiza. Matarajio yake sasa ni kushika nafasi ya urais na kutumia sera zake kuleta mabadiliko. “Nimejipanga kuwasaidia wanawake, vijana na watoto kwenye masuala ya kijamii na kiuchumi. 
Vijana wanakabiliwa na tatizo kubwa la ajira, nami nimeweka mkazo mkubwa katika hilo,” anasema. Hata hivyo, Laila anakiri iwapo hatashinda hatakata tamaa, bali ataendelea kushiriki kwenye kinyang’anyiro kingine na kushirikiana na washindi kuhakikisha maendeleo ya Wazanzibari yanapatikana.

WANAOMFAHAMU LAILA 
Mtumwa Ame Khamis, mkazi wa Fuoni, anaeleza: “Laila ni mwanamke aliyebeba ujasiri wa kugombea nafasi ya urais bila woga. Amejibika na hakuogopa kuingia kwenye kinyang’anyiro hiki na kuandika historia ya Zanzibar.” 
Sheha wa Jimbo la Fuoni, Juma Mussa  Juma, naye anaeleza: “Ninampongeza Laila kwa kujiamini na kujitoa kwake. 
Hii itachochea wanawake wengine kuingia kwenye siasa na kugombea nafasi za uongozi. Laila ni mwanamke mchapakazi na hodari, na naamini anaweza kuleta maendeleo Zanzibar. Hata hivyo, Sheha huyu aliongeza kuwa kwa majukumu yake hana takwimu za wagombea wa uchaguzi, wawe wanawake au wanaume, kwa kuwa si jukumu la Sheha kujiweka mbele katika mchakato huo. 

Pia, wagombea wenyewe hawana utaratibu wa kwenda kujitambulisha kwake, jambo linalomfanya abaki kando na masuala ya ushindani wa kisiasa.

Kwa upande wa chama chake, viongozi wameeleza kuwa kuibuka kwa mgombea mwanamke katika kinyang’anyiro cha urais ni hamasa kubwa kwa wanawake wengine. Wamefafanua changamoto kubwa kwa wanawake ni ukosefu wa elimu ya uongozi na hofu ya kujiamini, jambo linalozuia wengi kuingia kwenye siasa.
 
Naibu Katibu Mkuu wa NCCR-Mageuzi, Ameir Mshindani Ameir, anaona ni muhimu serikali kurejesha ruzuku kwa wagombea kama ilivyokuwa mwaka 1995 ili kusaidia kampeni. “Katika kipindi hiki cha kampeni, ruzuku ingesaidia wagombea kupata nguvu ya kuendelea na harakati zao. Bila rasilimali za kifedha, mgombea anakosa nguvu ya kushindana kikamilifu,” anabainisha.

Licha ya changamoto zote, Laila ameapa kutokata tamaa. Ndoto yake kuu ni kushika nafasi ya juu ya uongozi na kuwa sehemu ya historia ya wanawake waliopigania maendeleo ya Zanzibar. Ujasiri wake, kujitolea na kujiamini kwake ni mfano wa kuigwa kwa kizazi cha wanawake wanaotaka kuandika historia zao za kisiasa.

 Kwa kumbukumbu, katika uchaguzi wa mwaka 2020, wagombea wa nafasi ya uwakilishi walikuwa 251, ambapo wanawake walikuwa 61 na wanaume 190. Kwa upande wa madiwani walijitokeza wagombea 350, wanawake 74 na wanaume 276. Kwa mwaka 2025, Tume ya Uchaguzi Zanzibar bado haijatoa takwimu rasmi zinazoonesha jumla ya wagombea wa nafasi za uwakilishi, ubunge pamoja na udiwani.

Kwa sasa, jina la Laila Rajab Khamis limechukuliwa kama alama ya mabadiliko, uthubutu na uwekaji wa historia ya mwanamke katika siasa za Zanzibar. Changamoto zinaweza kujitokeza, lakini dhamira yake ya kupigania nafasi ya urais na kuwatetea wanawake, vijana na watoto inaendelea kumpa nguvu ya kusonga mbele.
          MWISHO

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...