Skip to main content

KHADIJA ANWAR: MGOMBEA ANAESAKA UWAKILISHI JIMBO LA WAWI

 



IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@

KHADIJA Anwar Mohamed mwenye umri wa miaka 40 mkaazi wa Wawi Mgogoni ni mwanamke shupavu mwenye ndoto ya kuwa kiongozi tangu akiwa mdogo.

Aliamua kujiunga na chama cha CUF wakati huo ili kusudi apate nafasi ya kuwa kiongozi kwa lengo la kutatua kero za wananchi kwenye jamii iliyomzunguka.

Mwaka 2000 Khadija alianza kupata nafasi za uongozi katika chama chake, ambapo alijiona tayari anaenda kutimiza ndoto zake alizokuwa akiziwaza mara kwa mara.

Alianza kushika nafasi ya Mshikafedha wa tawi katika Jumuiya ya vijana na baada ya hapo ulifanyika uchaguzi kwenye chama na kufanikiwa tena kushika nyadhifa hiyo ya Mshikafedha lakini wa Jumuiya ya vijana kwenye jimbo.

"Kwa vile lengo langu ni kuwa kiongozi na kuwatetea wananchi maendeleo, sikufikia hapo bali niliendelea kushika nyadhifa mbali mbali ndani ya chama changu mpaka nimefikia pale ninapopataka," anaeleza Khadija.

Aliwahi kuwa Makamo Mwenyekiti mteule wa Kanda ya Pemba ambapo alikuwa anasimamia majimbo 18, hali ambayo iliendelea kumjengea ujasiri na kujiamini, huku akiamini wazi kwamba ipo siku ataingia kwenye vyombo vya maamuzi kuwatetea wananchi na kuwafikishia maendeleo.

Ilipofika mwaka 2019, wanachama wa CUF pamoja na viongozi wao walijiunga na chama cha ACT Wazalendo na baada ya kufanya uchaguzi, akabahatika kuwa Katibu wa Ngome ya Vijana Kusini Pemba na alikuwa anasimamia majimbo tisa (9).

"Baadae nikashika nafasi ya Mwenyekiti wa Ngome ya Vijana Taifa ingawa baada ya hapo kutokana na umri wangu kutoka kwenye ujana, ilinibidi nigombee nafasi nyengine ambazo zinaniruhusu," anafafanua Khadija.

Alifanikiwa kuwa Mjumbe wa Kamati Kuu ya chama Taifa, pia Naibu Waziri kivuli wa Mambo ya Ndani sambamba na Waziri kivuli wa Ulinzi.

Mama huyo alishikilia nafasi mbali mbali ndani ya chama, ndio alipoona sasa kuna haja ya kuingia kwenye vyombo vya maamuzi ili lengo lake la kuwatumikia wananchi aweze kulifikia.




"Nilijiona kuna nafasi nyingi nimeshikilia ndani ya chama changu, lakini nilisema kuwa bado lengo langu sijalifikia, hivyo lazima nipambane na ndipo nilipochukua fomu ya ubunge viti maalumu na kugombea," anasema.

Anaeleza kuwa, kura hazikutosha kwa upande wake kwa sababu kwenye majimbo wanawake wana tabia ya kusokotana sana, hivyo akatokea mshindi wa tatu, ingawa hakukata tamaa kwani kimpindi kilichofuata aligombea nafasi ya uwakilishi kwa upande wa Jimbo.

Ameshawahi kugombea nafasi hiyo mara mbili na zote kuibuka mshindi wa pili, ambapo mwaka huu kwa mara ya tatu amefanikiwa kuchaguliwa kugombea nafasi hiyo.

"Nilisema ni mwiko kukata tamaa, nikagombea tena uwakilishi mwaka huu wa 2025 na nashkuru sana wajumbe walinichagua kwa kura 82 huku wa pili yangu akiibuka na kura 52," anaeleza.

Alikuwa mwanamke pekee kati ya wagombea watano waliokuwa wakitafuta nafasi hiyo, ambapo aliwashinda wanaume wanne na ndipo alipopata nafasi ya kugombea ili kuishikilia nafasi hiyo kwenye Jimbo lake.

Khadija anahadithia kuwa, ilikuwa ni ngumu kuingia jimboni kugombea kutokana na wanaume kumkwaza kwa kile wanachodai kuwa, nafasi za wanawake ni viti maalumu pekee na za majimboni ni za wanaume tu.

"Kwa kweli walinishika nisigombee lakini niliwaambia kuwa nimeshaweka nia ya kugombea na nimeamua, kwa hiyo sipindishi kauli yangu na hasa kwa vile chama chetu kinazingatia jinsia, ndipo nilipopata nguvu zaidi ya kujiamini," anaeleza.




Ingawa alikosa mara mbili lakini hakukata tamaa ambapo mara ya tatu amefanikiwa kuingia kwenye mchakato wa kugombea na sasa anaendelea kuwaomba wananchi kura za ndio, ili aweze kuwaletea maendeleo katika Jimbo lake la Wawi Wilaya ya Chake Chake.

Mgombea huyo wa uwakilishi kupitia chama cha ACT Wazalendo anasema, hakupambana cha changamoto sana katika kugombea, kwani tayari alikuwa ameshajiamini, hivyo hakuna mtu aliemsikiliza kwa kumvunja moyo.

"Unajua changamoto zinakuja kutokana na udhaifu wetu wanawake, kwa sababu mtu akikuona dhaifu anakutumia kukuharibia lakini ikiwa umejiamini na umesimama imara, hakuna changamoto yeyote inayoweza kukuopelekesha," anafafanua.

Changamoto nyengine alizokumbana nazo ni kupigiwa, kudhalilishwa na kutolewa maneno ya kashfa, kwani katika jamii kuna watu wa vyama tofauti, hivyo kila mmoja anajiona yeye yuko sahihi kuliko mwenzake.

Anawataka wananchi wa Jimbo hilo wategemee mazuri endapo watamchagua na kuingia kwenye chombo cha maamuzi, kwani ni lengo lake kuwatumikia na kutatua changamoto zinazowakabili.

Anasema, wananchi wa Jimbo hilo wanatambua utendaji wake wa kazi na kusimamia ipasavyo majukumu yake, hivyo anaamini kuwa watamchagua ili aweze kwenda kuwatetea.

Mgombea huyo anasema, alipochaguliwa na wajumbe alifurahi sana kwani aliona wamemuamini na ndio maana wakamchagua kwenda kuwatetea na kuwaletea maendeleo wananchi.

"Lakini furaha ile inakatika ghafla pale unapoona kuwa kuchaguliwa kule ni kubeba dhima hapa Duniani na Akhera, hivyo akili yako yote unaipeleka kutumikia wananchi ipasavyo na sio kufurahia kwa kuwa umepitishwa kugombea nafasi hiyo," anasema.

Anaeleza kuwa, na utakapokumbuka kwamba umebeba dhima katika hilo, basi utafanya kazi kwa kuwa na hofu ya Mungu pamoja na kuwa na uadilifu, jambo ambalo utatekeleza vizuri majukumu yote waliyokutwisha wananchi wa Jimbo lako.

Khadija anasema, atapofanikiwa kuwa mwakilishi wa Jimbo hilo atajitahidi kuifikisha Wawi pale wanapoitaka wananchi kwa kuwa ya kimaendeleo zaidi.

"Kuna mwenzangu mwanamke ambae yupo Jimbo jengine, alinitaka ushuari kuhusu kugombea Jimbo au viti maalumu? nikamwambia tujitupe kwenye Jimbo, ingawa hakuwa na tamaa ya kupata lakini na yeye alifanikiwa na tayari yupo kwenye mchakato wa kugombea," anaeleza.

Anasema, wanawake wanaweza kugombea na kuleta mabadiliko makubwa endapo watafanikiwa, ingawa bado kuna baadhi yao wana hofu na ndio maana wanakimbilia viti maalumu.

Mama huo anasema, atakapochaguliwa kuwa mwakilishi, atafanya kazi zake za kuwatumikia wananchi na pia atafanya majukumu ya nyumbani bila kuathiri upande wowote.

"Majukumu ya nyumbani lazima niyafanye kama mke, mama na familia na majukumu ya kazi nitayafanya kadiri yatakavyokuwepo, nitajitahidi sitoathiri upande wowote," anaeleza.

Anaeleza kuwa, mume wake anamuunga mkono katika harakati zote za kisiasa, hivyo anapata nguvu zaidi ya kutokata tamaa.

Aliwataka wananchi wazidi kuwa na imani nae na wamchague kwa ajili ya kuongoza kwenye Jimbo hilo, ili kuwafikishia maendeleo zaidi.

Mume wa Khadija, Omar Ali Shehe anasema,  anashirikiana na mke wake katika kuhakikasha anapata ushindi .

Anasema, mke wake ana uwezo mzuri wa kuongoza, ni jasiri na ana uthibutu, hivyo atakapopata nafasi ya kuongoza Jimbo, anaamini atawatimikia vyema wananchi wake.

Anasema kuwa, anamuunga mkono katika kila hatua kwani anamuamini na anajua lengo lake, hivyo anampa mashirikiano makubwa na ndio maana anafanikiwa hatua kwa hatua.

Katibu wa Habari, Mawasiliano na Uenezi katika Jimbo la Wawi Yussuf Maulid Issa anasema, Khadija ni mwanamke mpambanaji, asieyumba, asieogopa misukosuko na anaejali maslahi ya Jimbo lake.

Anamuelezea kuwa, Khadija amekuwa akisaidia mambo mbali mbali katika Jimbo lake bila kujali vyama, hivyo atapofanikiwa kushika nafasi ya uwakilishi, anaamini atatatua kero zilizomo kwenye Jimbo lake.

"Ameshawahi kuandaa kombe la kumuenzi Maalim Seif Sharif Hamad na kuzishirikisha timu zote za Jimbo na timu iliyopata ushindi ilikabidhiwa zawadi yake," anahadithia.

Mgombea huyo ameolewa na ana watoto na anapewa mashirikiano mazuri na familia yake katika harakati za kugombea nafasi za uongozi.

                            MWISHO 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...