Skip to main content

WADAU WA HABARI ZANZIBAR WAIKUMBUSHA TENA SMZ JAMBO LAO

 


NA MWANDISHI WETU, ZANZIBAR@@@@


WADAU wa vyombo vya habari wameiomba serikali ya Mapinduzi Zanzibar kukamilisha mchakato wa marekebisho ya sheria za habari zilizotolewa maoni na wadau ili  kutoa mazingira rafiki kwa waandishi wa habari kutekeleza majukumu yao bila vikwazo.

 

Imeelezwa kwa muda mrefu licha ya wadau mbalimbali kutoa na kuwasilisha mapendekezo yao kuhusu mapungufu yaliyopo kwenye baadhi ya sheria hizo, lakini utekelezaji wake bado umekuwa wa kusuasua jambo linalopelekea mazingira magumu ya utendaji kazi wa vyombo vya habari nchini.

 

Mkurugenzi wa Chama cha Waandishi wa Habari Tanzania, Zanzibar (TAMWA ZNZ), Dkt. Mzuri Issa alieleza mchakato wa mabadiliko ya sheria za habari umekuwepo kwa miaka mingi lakini bado sheria hizo ambazo nyingi ni za muda mrefu zimekwama kurekebishwa.

 

"Sisi wengine tangu tuko waandishi chipukizi tunazungumzia kupata hizi sheria mpya za habari, tangu 2008 kwa kweli ni muda mrefu, tunahitaji kusimamia jambo hili kwa umoja wetu na hatimae tupate sheria mpya za habari Zanzibar," alieleza Dkt. Mzuri katika kongamano hilo.




 

Aliongeza wadau wa habari wamefanya mapitio ya sheria nane za habari ikiwemo Sheria ya usajili wa wakala wa habari, magazeti na vitabu namba 5 ya mwaka 1988 iliyofanyiwa marekebisho na sheria no.8 ya 1997, Sheria ya Tume ya Utangazaji Zanzibar namba 7 ya mwaka 1997  iliyorekebishwa na sheria namba 1 ya mwaka 2010 na kuwasilisha ripoti ya mapendekezo yao kwa mamlaka husika ikiwemo kukutana na Rais na waziri.

 

Aliongeza kuwa "tumewahi kuzungumza na Mhe. Rais kuhusu sheria hizi na Waziri pia, nadhani inabidi tupange kuzungumza nao tena ili tuone hili linakwendaje. Haitapendeza hata kidogo tumalize mwaka huu na bado hatujapata mabadiliko ya sheria za habari.”

 

Akigusia kuhusu uhuru wa vyombo vya habari na mabadiliko ya tabianchi, Katibu Mtendaji wa Baraza la Habari Tanzania (MCT), Ernest Sungura, alieleza vyombo vya habari vitatekeleza kwa ufanisi wajibu wao katika kulinda mazingira iwapo waandishi watakuwa huru kupata na kutoa taarifa bila hofu kisheria.

 

Alieleza, “kaulimbiu ya kimataifa mwaka huu ilijikita katika uhifadhi wa mazingira. Lakini kwakweli bila kuwa na sheria nzuri za habari hatuwezi kutekeleza hayo tunayoyataka. Waandishi wa habari tunahitaji uhuru wa kupata taarifa ili tuweze kutekeleza uandishi wa habari mahususi. Hatuwezi kuyatekeleza hayo kama sheria hazitutengenezei mazingira ya kulinda uhuru wetu.”



 

Katika hatua nyingine alivitaka vyombo vya habari kubuni mbinu mpya za kukabiliana na changamoto za kiuchumi na kufikiria namna ya kuendana na kasi ya mageuzi ya masuala ya kiteknolojia ili kulinda uhuru wao.

 

"Sahizi changamoto kubwa inayoathiri uhuru wa habari ni masuala ya kiuchumi katika vyombo vya habari. Tunaitaji kuangalia upenyo ili kuona namna gani kile kinachosababisha madhara katika vyombo vya habari kinatatuliwa," alibainisha katibu mtendaji huyo.

 

Akifafanua kuhusu maendeleo ya mchakato wa mabadiliko ya sheria za habari Zanzibar, Katibu Mtendaji Tume ya Utangazaji, Suleiman Salim alieleza tayari mapendekezo ya sheria hizo yapo ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali kwaajili ya hatua zaidi.

 

"Kwa sasa mswada wa sheria ya habari ipo kwa mwanasheria mkuu, na tunaitegemea itakwenda baraza la wawakilishi kama mswada na tunawaomba walioko kule waichangie vizuri ili iweze kupita na tupate sheria mpya," Suleiman Salim, Katibu Mtendaji Tume ya Utangazaji aliwaambia wadau.




 

Aidha Suleiman alisema tayari serikali imekamilisha mchakato wa kuandaa Sera mpya ya habari Zanzibar na kuwatoa hofu wadau wa habari juu ya uwepo wa sera hiyo kuwa itazinduliwa muda sio mrefu.

 

Akichangia mdahalo kwenye maadhimisho hayo, Salim Said ambaye ni mwandishi wa habari mkongwe alieleza uwepo wa sheria bora ni muhimu katika kuwezesha mazingira bora ya waandishi wa habari kuwajibika.



 

"Vyombo vya habari ni washirika wa maendeleo, hivyo kuwa na sera na sheria bora itawawezesha waandishi wa habari kuwa na mazingira rafiki katika  kutekeleza majukumu yao," alifahamisha, mwandishi wa habari huyo mkongwe Zanzibar.

 

Maadhimisho ya siku ya uhuru wa vyombo vya habari 2024 yameandaliwa Baraza la habari Tanzania Ofisi ya Zanzibar (MCT ZNZ), Chama cha Waandshi wa Habari Tanzania Zanzibar (TAMWA,ZNZ) Jumuiya ya Waandishi wa Habari za Maendeleo (WAHAMAZA), Klabu ya Waandishi wa Wabari Zanzibar (ZPC) na Shirika la Commonwealth Foundation yakiambatana na kaulimbiu ya  “UHURU WA VYOMBO VYA HABARI NA MAGEUZI YA SERA NA SHERIA ZA  HABARI ZANZIBAR, ambapo yamefanyika leo Mei 23, 2024 kisiwani Unguja.

 

-------MWISHO-

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan