Skip to main content

MAAFISA USTAWI: ‘ONGEZENI MAARIFA KUKABILI MAJANGA NDANI YA JAMII’

 



 NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

MAAFISA ustawi wa jamii kisiwani Pemba, wamekumbushwa, kuongeza maarifa zaidi, ili kukabiliana na majanga yaliomo katika jamii, kwani wao ndio wahusika wakuu, katika kuilea jamii.

 

Walielezwa kuwa, jamii imekuwa ikiwapelekea vilio vyao mbalimbali, hivyo wasipokuwa makini kuongeza maarifa ya utatuzi wa majanga, utoaji wa ushauri nasihi na malezi ya kisayanysi, wanaweza kupoteza uaminfu wao, kwa jamaii.

 

Hayo yameelezwa leo Mei 19, 2024 na Mkurugenzi wa Mwemvuli wa asasi za kiraia Pemba ‘PACSO’ Mohamed Najim Omar, wakati akiyafungua mafunzo ya siku tano (5), kwa maafisa walioko serikalini na wale wa mtaani, kwenye mafunzo yanayoendelea, skuli ya maandalizi Madungu Chake chake.

 

Alisema, kila siku ndani ya jamii, kumekuwa kukiibuka majanga mapya, hivyo kama hawakuwa makini kuongeza maarifa, ya jinsi gani ya kuisadia jamii, wanaweza kukosa kazi kuachwa nyuma baadae.

 

‘’Kila siku huzuka majanga mapya, kwa mfano watoto kubakwa, kulawitiwa, kudhalilishwa, kufanyia ukatili kwa vipigo vya kupindukia, hivyo waongeze maarifa, ili wajue namna ya kuwasaidia,’’alieleza.

 

Alieleza kuwa, mafunzo hayo anaamini yatawasaidia mno maafisa hao, katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku, kwa lengo la kuleta mabadiliko, ndani ya jamii.

 

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa ‘PACSO’ Sifuni Ali Haji, alisema anategemea baada ya kumalizika kwa mradi wao wa upatikanaji haki wa miaka minne, kuweko na mabadiliko makubwa ndani ya jamii.

 

‘’Kwani kundi la watoto, limekuwa likikumbwa na majanga mbali mbali na kisha hukosa ushauri nasaha, na kuwapelekea wingine hata kukatisha masomo na nadoto zao nyingine,’’alieleza.

 

Aidha Katibu Mkuu huyo aliipongeza ‘UNDP’ kwa kupatikana kwa mradi huo, kwa kiasia kikubwa umekuja kuongeza, ufanisi kwa kundi la jamii na hasa watoto, katika kutokata tamaa, baada ya kufanyiwa udhalilishaji.

 

‘’Mradi unataka kuona kwanza, watoto wanaishi bila ya majanga, na kama yakitokezea, iwe maafisa ustawi wawe na uwezo na mbinu za kuwarejesha katika mfumo wa maisha, ambao walidhani umeshatoweka kwao,’’alieleza.

 



Mtoa mada kutika mafunzo hayo ya siku tano, anayetoka Jumuiya ya ‘ZASWA’ Saleh Juma Mbarouk, alisema moja ya sifa za msuluhisi au afisa usatawi, ni kujitambua kwa undani.

 

Alieleza kuwa, jingine ni kujenga uaminifu, kuwa na taarifa kadhaa, takwimu na kuisoma jamii, yake kabla ya kuanza kutoa ushauri nasaha.

 

‘’Huwezi kuwa Afisa ustawi wa jamii mzuri, ikiwa kwanza hujitambui thamani yako na jamii yako, hulifahamu kundi unalolifanyia kazi, huna taarifa sahihi na wakati mwingine hata takwimu, ‘’alieleza.

 



Wakichangia mada katika mafunzo hayo, washiriki Arafa Amour Mzee kutoka Mkoani na Ali Abdalla Juma wa Chake chake, wamesema, kazi kubwa inahitajika, ili kuwakinga watoto na majanga.

 

Walisema, wazazi na walezi, lazima wasiwe sehemu ya kuwapotosha watoto wao, kwa mfano kuwashirikisha katika mambo yasiowahusu, kwani kufanya hivyo, kunaweza kukawavunjia ndoto zao.

 




Hata hivyo, wameipongeza ‘PACSO’ na wanafadhili wao ‘UNDP’ kwa uamuzi wa kutoa mafunzo hayo, ambayo yatawajengea uwezo wa kukabiliana na mambo kadhaa, ikiwemo viashiria vya udhalilishaji katika maeneo yao.

 

Mafunzo hayo ya siku tano, ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wa upatikanaji haki, unaotekelezwa na ‘PACSO’ kwa muda wa miaka minne, na tayari kuanzia mwaka jana, shughuli kadhaa zimeshafanyika, ikiwa ni pamoja na mafunzo ya haki za binaadamu na utawala bora,  kwa watu wenye ulemavu, viongozi wa dini na waandishi wa habari.

 

                  Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan