Skip to main content

MAAFISA USTAWI: ‘ONGEZENI MAARIFA KUKABILI MAJANGA NDANI YA JAMII’

 



 NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

MAAFISA ustawi wa jamii kisiwani Pemba, wamekumbushwa, kuongeza maarifa zaidi, ili kukabiliana na majanga yaliomo katika jamii, kwani wao ndio wahusika wakuu, katika kuilea jamii.

 

Walielezwa kuwa, jamii imekuwa ikiwapelekea vilio vyao mbalimbali, hivyo wasipokuwa makini kuongeza maarifa ya utatuzi wa majanga, utoaji wa ushauri nasihi na malezi ya kisayanysi, wanaweza kupoteza uaminfu wao, kwa jamaii.

 

Hayo yameelezwa leo Mei 19, 2024 na Mkurugenzi wa Mwemvuli wa asasi za kiraia Pemba ‘PACSO’ Mohamed Najim Omar, wakati akiyafungua mafunzo ya siku tano (5), kwa maafisa walioko serikalini na wale wa mtaani, kwenye mafunzo yanayoendelea, skuli ya maandalizi Madungu Chake chake.

 

Alisema, kila siku ndani ya jamii, kumekuwa kukiibuka majanga mapya, hivyo kama hawakuwa makini kuongeza maarifa, ya jinsi gani ya kuisadia jamii, wanaweza kukosa kazi kuachwa nyuma baadae.

 

‘’Kila siku huzuka majanga mapya, kwa mfano watoto kubakwa, kulawitiwa, kudhalilishwa, kufanyia ukatili kwa vipigo vya kupindukia, hivyo waongeze maarifa, ili wajue namna ya kuwasaidia,’’alieleza.

 

Alieleza kuwa, mafunzo hayo anaamini yatawasaidia mno maafisa hao, katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku, kwa lengo la kuleta mabadiliko, ndani ya jamii.

 

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa ‘PACSO’ Sifuni Ali Haji, alisema anategemea baada ya kumalizika kwa mradi wao wa upatikanaji haki wa miaka minne, kuweko na mabadiliko makubwa ndani ya jamii.

 

‘’Kwani kundi la watoto, limekuwa likikumbwa na majanga mbali mbali na kisha hukosa ushauri nasaha, na kuwapelekea wingine hata kukatisha masomo na nadoto zao nyingine,’’alieleza.

 

Aidha Katibu Mkuu huyo aliipongeza ‘UNDP’ kwa kupatikana kwa mradi huo, kwa kiasia kikubwa umekuja kuongeza, ufanisi kwa kundi la jamii na hasa watoto, katika kutokata tamaa, baada ya kufanyiwa udhalilishaji.

 

‘’Mradi unataka kuona kwanza, watoto wanaishi bila ya majanga, na kama yakitokezea, iwe maafisa ustawi wawe na uwezo na mbinu za kuwarejesha katika mfumo wa maisha, ambao walidhani umeshatoweka kwao,’’alieleza.

 



Mtoa mada kutika mafunzo hayo ya siku tano, anayetoka Jumuiya ya ‘ZASWA’ Saleh Juma Mbarouk, alisema moja ya sifa za msuluhisi au afisa usatawi, ni kujitambua kwa undani.

 

Alieleza kuwa, jingine ni kujenga uaminifu, kuwa na taarifa kadhaa, takwimu na kuisoma jamii, yake kabla ya kuanza kutoa ushauri nasaha.

 

‘’Huwezi kuwa Afisa ustawi wa jamii mzuri, ikiwa kwanza hujitambui thamani yako na jamii yako, hulifahamu kundi unalolifanyia kazi, huna taarifa sahihi na wakati mwingine hata takwimu, ‘’alieleza.

 



Wakichangia mada katika mafunzo hayo, washiriki Arafa Amour Mzee kutoka Mkoani na Ali Abdalla Juma wa Chake chake, wamesema, kazi kubwa inahitajika, ili kuwakinga watoto na majanga.

 

Walisema, wazazi na walezi, lazima wasiwe sehemu ya kuwapotosha watoto wao, kwa mfano kuwashirikisha katika mambo yasiowahusu, kwani kufanya hivyo, kunaweza kukawavunjia ndoto zao.

 




Hata hivyo, wameipongeza ‘PACSO’ na wanafadhili wao ‘UNDP’ kwa uamuzi wa kutoa mafunzo hayo, ambayo yatawajengea uwezo wa kukabiliana na mambo kadhaa, ikiwemo viashiria vya udhalilishaji katika maeneo yao.

 

Mafunzo hayo ya siku tano, ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wa upatikanaji haki, unaotekelezwa na ‘PACSO’ kwa muda wa miaka minne, na tayari kuanzia mwaka jana, shughuli kadhaa zimeshafanyika, ikiwa ni pamoja na mafunzo ya haki za binaadamu na utawala bora,  kwa watu wenye ulemavu, viongozi wa dini na waandishi wa habari.

 

                  Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...