Skip to main content

HIFADHI YA MAZINGIRA KAMBINI, YASEMA WAANDISHI NGUZO YA MAFANIKIO

 



NA HAJI NASSSOR, PEMBA@@@@

 

UONGOZI wa Jumuiya ya uhifadhi wa mazingira ya kijiji cha Kambini Kichokochwe, wilaya ya Wete Pemba, umesema kuwa, ukitaka kufanikiwa katika utekelezaji wa jambo lolote, ni vyema kuwashirikisha waandishi wa habari.

 

Ulisema, kutokana na kuwa na suati pana na ya haraka, wanaweza kufanikisha kampeni yoyote, ambayo jumuia, jamii au serikali kuu imeamua kuwafikia wananchi wake.

 

Kauli hiyo imetolewa leo Mei, 19 na Katibu wa Hifadhi hiyo, Bakari Suleiman Juma, wakati akizungumza na wanachama wa jumuiya ya waandishi wa habari Pemba ‘PPC’ na wananchi wingine, kwenye kilele cha maadhimisho ya siku ya uhuru wa habari dunia, ambapo waandishi hao, waliiadhimisha kwa upandaji wa mikoko.

 




Alisema, waandishi wa habari, wamekuwa na mchango mkubwa, katika kufakikisha kila kitu, mfano zoezi la uhamasishaji upandaji miti hiyo, hivyo kwa tukio hilo, limewapa hamasa.

 

Alieleza kuwa, aanamini jamii ya Tanzania, itapata mwanga wa kuhakikisha wanapanda miti katika maeneo yaliokumbwa na mabadiliko tabia nchi, kufuatia tukio la waandishi wa habari kushirikiana nao.

 

‘’Kwa hakika uongozi wa ‘PPC’ na wadu wenu Umoja wa Vilabu vya Habari Tanzania ‘UTPC’ mmefikiria jambo jema na zuri, la kuadhimisha siku yenu, kwa upandaji miti katika eneo la bahari ya hindi, hapa Kambini Kichokochwe,’’alieleza.

 

Kwa upande wake, Mwenyikiti wa Klabu ya waandishi wa habari Pemba ‘PPC’ Bakar Mussa Juma, alisema waandishi pamoja na kazi yao ya kuandika habari, wameona ni vyema kuungana na jamii, katika zoezi hilo.

 





Alieleza kuwa, mara nyingi tukio hilo hupendelea kuadhimisha kwenye kumbi za mikutano, ingawa kwa kutambua umuhimu wa upandaji miti na faida zake, wameamua kujitoa,’’alieleza.

 

Alifahamisha kuwa, mwaka jana wanachama wa ‘PPC’ walishiriki katika zoezi la usafi, katika fukwe ya bahari ya Vuma wimbi mkoa wa kaskazini Pemba, kwa dhamira ya kuziweka safi.

 

‘’Waandishi wa habari, nao ni waathirika wa joto lenye ujazo mkubwa, na ndio maana tumehamasika kuzihama ofisi kwa muda na kulirejeshea uasili wake eneo hili la Kichokochwe kwa upandaji miti,’’alieleza.

 



Akizungumza kwenye zoezi hilo, Mwenyekiti wa taasisi ya Community Forest Pemba ‘CFP’ Kombo Seif Khamis alisema, wamefarajika, kuona wameungana na waandishi wa habari, katika zoezi hilo.

 

Alieleza kuwa, kwani suala la athari za mabadiliko tabia nchi haziwakumbi wavuvi, wakulima, wafugaji pekee, bali hata kundi la waandishi wa habari, wakati wanapotekeleza majukumu yao.

 

Wananchi wa kijiji hicho, Fatma Shaame Hamad na Asha Ali Mussa, wamesema wamepata ari na kasi ya utunzaji wa mazingira, kufuatia tukio la waandishi wa habari, kuungana nao.

 



Walisema, ijapokua wao ndio waathirika wakubwa katika eneo hilo, lakini janga likiwa la kitaifa, kila mmoja anakuwa anakumbana na changamoto.

 

Kaimu Katibu wa ‘PPC’ Mchanga Haroub Shehe, aliwakumbusha waandishi wa habari, kuendelea kuyaibua maeneo kama hayo, ili wenye mamlaka wachukue hatua.

 

‘’Kupanda miti kama hivi leo, ni zoezi moja muhimu sana, lakini tuhakikishe, tunazidi kuyaibua, ili wanaofanyakazi zao, wabuni njia mbadala la kuzuia athari zaidi,’’alifafanua.

 



Mwandishi wa habari Hassan Msellem na mwenzake Maryam Salum Habibu, wamesema ni vyema kwa uongozi wa ‘PPC’ kwa kushirikiana na wadau wao, kufanya zoezi kama hilo, kila fursa inapopatikana.

 

Katika zoezi hilio, mkiti aina ya mikoko 10,000 imepandwa kwa mfumo wa mbegu, katika eneo la bahari ya hindi, ambalo miaka 25, eneo hilo lilikuwa sehemu ya nchi kavu.

 

                       Mwisho   

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan