Skip to main content

WATOTO WA KIKE BADO NGOMA NZITO KUSHIRIKI MCHEZO WA SOKA

 

 



HABIBA ZARALI, PEMBA@@@@ 

 

Ushiriki mdogo kwenye michezo kwa watoto wa kike, Kisiwani Pemba ni sababu moja inayopelekea wanawake kuwa nyuma katika sekta hiyo.

 

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa nyakati tofauti kisiwani humo, wananchi hao walisema bado wanawake ushiriki wao ni mdogo, katika michezo ya aina mbali mbali, hivyo jitihada zinahitajika kuhakikisha nao wanashiriki kama walivyo vijana wa kiume.

 

 

Said Ali Said wa Mkoani, alisema watoto wa kike huishia maskulini kushiriki michezo na wanapomaliza hawajiendelezi na wala hakuna mtu wala taasisi ya kuviendeleza vipaji hivyo.

 

"Wapo watoto wa kike wanakuwa wazuri tu katika michezo mbalimbali, kama mpira wa miguu, kikapu, mpira wa Pete na mengine, lakini cha kusikitisha ni kuwa baada ya kumaliza skuli hawajiendelezi tena,"alisema.

 

Massoud Ali Mohamed wa Chake Chake, alisema kutokana na changamoto ya mavazi, kunasababisha kudumaza kwa michezo kwa watoto wa kike.

 


Alifahamisha kuwa, kama hakutozingatiwa mavazi ya stara kwa watoto wa kike, kunaweza kukaendelea kuwa na mwitikio mdogo wa kushiriki watoto wa kike kwa kutoruhusiwa na wazazi wao.

 

"Mimi nahisi kuwe na sheria hasa watoto wa kike ya kuvaa vazi ka heshima ‘Islamic hijab’ wanapokuwa katika michezo ili waweze na stara,"alishauri.

 

Salma Suleiman wa Mkoani alisema, ili watoto wa kike waweze kuwa sawa na wanaume, kwenye suala la kushiriki michezo ni lazima Serikali itowe elimu, iwawezeshe kifedha na kuvaa nguo za maadili.

 

Katibu wa chama cha mpira wa miguu Wilaya ya Chake chake Jongo Juma Jongo, alisema kwa sasa ushiriki wa wanawake katika mchezo huo upo, ingawa ni mdogo.

 


Alifahamisha kuwa, mwitikio mdogo wa watoto wenyewe, jamii inavyochukulia mpira wa miguu ni uhuni kwa watoto wa kike inawafanya wasiendelee mbele kwenye michezo.

 

Akigusia kwa upande wa mavazi, Jongo alisema isiwe kikwazo kwa wanawake wani wanaruhusiwa kuvaa nguo za stara ikiwemo treki, vilemba na kuwataka wazazi wawaruhusu watoto wa kike, kushiriki michezo ili waweze kutimiza ndoto zao.

 

"Kuwazuwia watoto wa kike kutoshiriki michezo si haki kwa sababu, dunia ya sasa imebadilika na kupiga hatuwa

Kwani, kuna nafasi za kusoma nje ya nchi kupitia michezo na hatimaye kupata ajira",alisema.

 

Idara ya michezo na utamadini wizara ya elimu na mafunzo ya elimu, ilisema wizara inayo mikakati mbali mbali ya kuhakikisha wanawake wanakuwa sawa, katika ushiriki wa michezo.

 

Akiitaja mikakati hiyo ni pamoja na kuanzisha somo la sanaa na ubunifu, michipuo wa michezo pamoja na kuanzisha elimu ya juu vyuoni.

 

Kaimu mratib wa michezo wizara ya Habari, Utamadini na Michezo Khamis Hamad Juma, alisema katika kuhakikisha vijana wa kike wanashihiriki kikamilifu katika michezo inaweka miundo mbinu ya kujenga viwanja vinne vitakavyozingatia mahitaji yote kisiwani Pemba

 

Alieleza kuwa, viwanja hivyo, ambavyo kila kimoja kitakuwa na viwanja vya kuchezea michezo minne tofauti, ambapo ujenzi unaanza mwanzoni mwa mwezi wa sita mwaka huu 2024.

 

Mwalimu kutoka skuli ya Sekondari Uweleni Khamis Mohamed Ussi, alithibitisha kuwa wanafunzi wanaoshiriki katika michezo, ndio wanavofanya vizuri katika masomo yao.

 

Hivyo aliwaomba wazazi, kuwaruhusu watoto wao kushiriki katika michezo mbali mbali, ili waweze kupata fursa zinazotokea kupitia sekta ya michezo.

 

Hakuna hata sheria moja, kati ya zile 17 zinazoongoza mpira wa miguu, zinazomzuia mtoto wa kike, kushiriki mchezo, kwani kanuni ya kwanza ni uwepo wa uwanja ya pili ni mpira, idadi ya wachezaji, vifaa vya michezo, mwamuzi pamoja na shera ya 17 ya pigo la kona.

 

Mwisho 

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan