Skip to main content

UGONJWA WA ‘RED EYES’ WAKWAMISHA KESI DAWA ZA KULEVYA PEMBA

 

 NA MARYAM NASSOR, PEMBA@@@@   

 KESI ya kupatikana na dawa zinazoaminika kuwa ni za kulevya, iliyopo mahakama kuu Zanzibar, kanda ya Pemba, imeshindwa kuendelea, baada ya shahidi nambari moja, ambae ni Mkemia kushindwa kufika  mahakamani hapo, kwa  udhuru wa  ugonjwa wa ‘RED EYES’.

 Awali, ilidaiwa mahakamani hapo kuwa, mtuhumiwa katika shauri hilo, Omar Khatibu Juma, alikutwa na misokoto 700 yanayosadikiwa kuwa ni dawa za kulevya  aina ya bangi, yenye uzito wa gramu 2836.75, eneo la Machomane wilaya ya Chake chake.

Mara baada ya kufika mahakamani hapo, mtuhumiwa akiwakilishwa na wakili wake Zahran Mohamed Yussuf aliambiwa  na upande wa mashtaka ulioongozwa na Mwendesha mashtaka kutoka Afisi ya Mkurugenzi wa mashtaka, Mohamed  Ali Juma, kuwa walikuwa wanategemea kupokea mashahid watatu.

 

Alidai kuwa, kesi hiyo ipo kwa ajili ya kusikilizwa,  na wamepokea mashahidi wawili, kati ya watatu waliyoitwa, ingawa shahidi nambari moja ambae ni Mkemia, hajafika mahakamani hapo kutokana na kusumbuliwa na ugonjwa wa macho mekundu.

Aliendelea kudai kuwa, kutokana na aina ya kesi hiyo wanahitaji mtiririko mzuri wa mashahidi, hivyo hawawezi kusikiliza shahidi wengine kabla ya kuanza na Mkemia.

‘’Mheshimiwa leo (jana) kesi ipo kwa ajili ya kusikilizwa, ingawa shahidi nambari moja hajafika mahakamani, hivyo tunaomba utupangie tarehe nyingine, kwa ajili ya kusikiliza mashahidi,’’alidai.

Mara baada ya kuusikiliza upande wa mashtaka, Jaji wa mahakama kuu Pemba, Ibrahim Mzee Ibrahim, aliuliza upande wa utetezi kuwa wanasemaje kuhusu ombi la upande wa mashtaka.

Nao, upande wa utetezi ulikuwa ukiongozwa na mawakili Zahran Mohamed Yussuf na Massoud Juma walidai kuwa, hawakubaliani na ombi hilo kutokana na kuwa, mteja wao ameshakaa ndani muda mrefu na kuomna kusikilizwa kwa mashahidi waliofika mahakamani.

“Mheshimiwa Jaji, kama ikikupendeza, basi tunaomba usikilize hao mashahidi wawili waliofika, kutokana na kuwa mteja wangu yuko ndani mudaa mrefu,”alidai.

Alidai kuwa, shauri hilo tokea lifunguliwe mahakamani hapo, linafika miezi sita na mtuhumiwa yuko ndani, kama ikiwezekana basi wasikilizwe hao mashahidi waliyofika na isiwe vyenginevyo.

Nae Jaji wa mahakama hiyo, alimuliza wakili wa upande wa utetezi kuwa mteja wake, ana shutumiwa na makosa mangapi, kwa sababu kama kosa ni kukutwa na bangi basi shahidi nambari moja ni Mkemia.

Aidha alisema, Mkemia ndie atakae thibitisha kuwa kile alichokiona ni bangi au laa na hapo, ushahidi utakaofuata utakuwa unasaidia.

“Hatuwezi kusikiliza shahidi wengine kabla ya Mkemia, kwa sababu ndie atakae thibitisha hizi tuhuma ni za kweli au laa,”alisema.

Nao upande wa utetezi kisha, ulikubaliana na hoja za Jaji huyo, na kisha kesi hiyo kughairishwa hadi Machi 7 mwaka huu, ili kuendelea na ushahidi.



Ilidaiwa mahakamani hapo kuwa, Julai 28, jana majira ya saa 4:00 za usiku eneo la Mkoroshoni, katika wilaya ya Chake chake, bila ya halali  alipatikana na misokoto 700, ya dawa zinazodhaniwa kuwa ni za kulevya aina ya bhangi, yenye uzito wa gramu 2836.75.

Hilo ni kosa kinyume na kifungu cha 21 (1) (d) cha sheria za Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana  na dawa za kulevya Zanzibar, sheria namba 8 ya mwaka 2021 sheria za Zanzibar.

                                         MWISHO

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...