Skip to main content

WAZIRI SULEIMAN ASHAJIISHA UTOAJI MAONI SERA MAMBO YA NJE




WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais Ikulu Zanzibar Ali Suleiman Ameir amewataka wananchi na wadau mbali mbali kutumia fursa ya kutoa maoni kwenye rasimu ya sera mpya ya mambo ya nje, ili kujenga sera madhubuti ambayo ni dira ya maendeleo itakayowanufaisha kijamii, kisiasa na kiuchumi.


Akizungumza katika kongamano la kukusanya maoni kuhusu marekebisho ya sera hiyo ya mwaka 2001 alisema, Serikali imeelelekeza kushirikishwa wadau ili kuwezesha kupata sera madhubuti itakayoboresha.

Alisema kuwa, ni muhimu kwa wadau kuunda sera madhubuti ambayo italiwezesha Taifa hili kunufaika ipasavyo na kukuza ushirikiano baina ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na mataifa mengine duniani.

"Tayari tumeshafanya makongamano haya katika mikoa mengine na sasa tunaendelea, haya yanalenga kupata sera yenye tija ambayo itakidhi matarajio ya wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania," alisema.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk alisema kuwa, kupitia kongamano hilo, wataelewa masuala muhimu katika sera ya mambo ya nje, ikiwemo dhana ya uchumi wa buluu ambayo ni miongoni mwa mbinu za kukuza uchumi katika nchi.

Aidha alieleza kuwa, sera hiyo itatoka fursa kwa wakulima wa mwani na karafu kupanua wigo katika masoko duniani, kwa lengo la kupata tija zaidi ya bidhaa zao.

Nae Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Said Shaib Mussa alisema, sera hiyo iliundwa mwaka 2001 na kuanzia kutumika mwaka 2004 ikiwa na lengo na kuimarisha ujirani mwema, ushirikiano wa kiuchumi, ushirikiano na nchi zinazoendelea,  pamoja na umoja wa nchi za afrika.

Alisema kuwa, matarajio yao katika sera hiyo ni kuimarisha uchumi wa buluu, uratibu wa mikataba na kulinda mila zetu za kiafrika, hivyo kuna haja ya kutoa maoni kwenye rasimu ya sera hiyo ili kuimarisha zaidi.

Akiwasilisha mada Kaimu Mkurugenzi Idara ya Diaspora Jastin Kisoka alifahamisha kuwa, msingi wa sera hiyo ni kulinda uhuru, kukuza ushirikiano wa kiuchumi na washirika wa maendeleo, kuanzisha, kuendeleza na kulinda maslahi ya kijamii, kiuchumi na kisiasa pamoja na kujenga uchumi endelevu.

Akielezea baadhi ya mafanikio alisema kuwa, ni kuimarisha ujirani mwema na ushirikiano wa uwili, ushirikiano wa kikanda na usuluhishi wa migogoro.

"Pia kuna baadhi ya changamoto ambazo zimetufanya tuje hapa kukusanya maoni yenu na kuziboresha, ikiwa ni pamoja na kutotumia ipasavyo lugha yetu, ukosefu wa miongozo ya kisera na kutokuwepo kwa ulinzi na usalama," alieleza.

Katibu Mkuu Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvivi Zanzibar Dk. Abdul Suleiman Jumbe  akiwasilisha dhana ya uchumi wa buluu alisema, rasimu hiyo imezingatia maeneo muhimu ya rasilimali za uchumi wa buluu ambazo wanaamini wataimarisha zaidi na kukuza uchumi wa wananchi na nchi kwa ujumla.

Waziri Mstaafu wa SMZ Mohamed Aboud Mohamed alisema, ni wajibu wa washiriki hao kutoa maoni ya kujenga ambayo yatakuwa na maslahi kwa Taifa lao, kwa ajili ya vizazi vya sasa na vijavyo.

Mkuu wa Mkoa Kusini Pemba Matar Zahor Massoud alisema, aliwasisitiza wananchi kutoa maoni mbali mbali kuhusu sera hivyo kwa maslahi yao na Taifa.

Kwa upande wao washiriki wa mkutano huo waliomba, ulinzi na usalama uimarishwe mbali mbali ikiwemo mipakani kwani kuna madawa ya kulevya yanaingizwa siku hadi siku, ambayo yanawaathiri vijana wengi ambao ndio Taifa la leo.

Mshiriki kutoka Baraza la vijana Micheweni alisema kuwa, ni vyema sera hiyo ikazungumzia namna bora ya kutatua changamoto za kimaadili, kwani imekuwa ni kikwazo kikubwa katika nchi ya Tanzania.

Kongamano hilo la siku moja limefanyika katika viwanja vya kufurahishia watoto Tibirinzi Chake Chake Pemba.

                 MWISHO.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch