Skip to main content

MITAZAMO INAVYOCHANGIA WANAWAKE KUTOGOMBEA UONGOZI.

 



   NA AMRAT KOMBO, ZANZIBAR @@@@

Wapo wanawake ambao wanao uwezo mkubwa wa kuwa viongozi, lakini baadhi ya mitazamo katika jamii inawarudisha nyuma na kuamua kukaa pembeni.

Kwa bahati mbaya mitazamo hii,  inahusishwa na maelekezo ya dini kutokana na tafsiri potofu inayotolewa na badhi ya watu juu ya maelekezo ya dini na kuonekana kwa kiasi fulani.

 Hata utekelezaji wa mikataba ya kikanda na kimataifa juu ya haki na nafasi za wanawake, ikiwa pamoja na katika uongozi, ambayo nchi yetu imeiridhia inatekelezwa kwa kuchechemea au kufumbiwa macho kwa visingizio mbali mbali.

Miongoni mwa mikataba inayohimiza kulindwa kwa haki za wanawake ni tamko la kimataifa kuhusu haki za binadamu la 1948 ambao umelenga kutokomeza aina zote za kuwabagua  wanawake.

Kifungu cha pili cha Mkataba wa Afrika juu ya haki za binadamu,inajumuisha kanuni yakutobagua kwa misingi ya rangi, kabila ,jinsia ,lugha,dini,siasa au maoni mengine yoyote.

Zanzibar inayo idadi kubwa ya waumini wa dini ya Kiislamu (zaidi ya asilimia 95),ambao mwenendo wa maisha yao unaongozwa na melekezo ya dini yao na kila kukicha viongozi wake wa dini ya Kiislamu huikanusha mitazamo ya watu wanaokataa mwanamke kuwa kiongozi.

Miongoni mwa maelezo yanayotolewa kuonyesha dini ya Kislamu haikatazi mwanamke kuongoza ni nafasi walizopewa wanawake kuogoza katika enzi za mitume,ikiwa pamoja na wakati wa vita.

Mwanazuoni maarufu wa masuala ya dini ya Kiislamu, Profesa Issa Haji Zidi wa Zanzibar, amekuwa akisisitiza mara kwa mara kwamba dini ya kiislamu haijakataza kuwepo kwa kiongozi mwanamke, isipokuwa mwanamke anatakiwa kufuata,sheria na taratibu na Kiiislamu juu ya mwanamke awe na mwenendo gani wa kimaisha ndani na nje ya nyumba yake.

Alisema  katika enzi za Mtume Muhammad (S .A.W ) mwanamke alikuwa kiongozi katika vita na mambo mengine na kote aliweza kuifanya kazi hio kwa uweledi na uadilifu.

Mchungaji wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Shukuru Malonda, alisema mwanamke ana nafasi mbalimbali  za uwongozi, ikiwemo  ndani ya kanisa na kijamii.

Alitoa mfano wa viongozi wa kike waliongoza na kuwasimamia watu katika dini ya Kikirsto na kutaja kwamba miongoni mwao  Esta, ambae alikuwa Malkia na Debora (  kiongozi na hakimu wa wana wa Israeli) alikuwa nabii.

Anasema katika kanisa hilo wamewapatia nafasi sawa wanawake na wanaume ya kuongoza kanisa, ikiwemo nafasi ya wachungaji na nafasi ya wainjilist.

"Katika kanisa letu, tumewachaguwa wanawake wawili na wanaume wanne ambao ni wachungaji, pamoja na wainjilist 12 ikiwa wanawake watano na wanaume saba, wote kazi yao moja ya kuongoza kanisa,"alisema.

Licha ya serikali kusimamia maendeleo ya wanawake, lakini taasisi zisizoza kiserikali  wanaume na wanawake wanapata nafasi sawa za uongozi na hapana tatizo lolote.

Mratibu wa kuinua wanawake katika uongozi  katika Chama cha Waandishi wa Habari Wanwawe (TAMWA ZANZIBAR), Maryam Ame,alisema  haielewi dini inayokataza mwanamke kuwa kiongozi,ispokuwa jambo muhimu ni kuwa na uwezo na kuimudu nafasi hio.

"Tunatoa elimu kwa wanawake ambao wanahitaji kuwa viongozi ili wajitambue na kutatua changamoto zinazowakabili, vikiwemo vikwazo vya kusingizia dini," aleieleza.




Mapka hivi karibuni wanawake 172, wamepatiwa mafunzo ya uongozi Unguja na Pemba na kuwashauri wanaotaka kuingia kwenye uongozi wasiwe na hofu kwani katiba inawahakikishia haki hio ambayo inasisitizwa katika mkataba mbali mbali ambayo nchi yetu meiridhia.

Pamoja na hamasa  za serikali, asasi za kiraia na viongozi wa dini, lakini mwanasiasa Hamisa Mmnanga alisema bado ipo haja ya wakati wa uchaguzi  kuwepo na utaratibu bora utaowapa nafasi waliokuwa  mahodari, shupavu na jasiri kuwania nafasi hizo.

Diwani wa zamani wa Bububu, Amina Ali Mohamed, alisema mitazamo ya kidini inayoshadidiwa na baadhi ya watu imesababisha kuwepo mizozo na mara nyengine wanawake kudharauliana.

"Baadhi ya wananchi bado wapo nyuma katika kuhakikisha mwanamke anapewa nafasi ya uongozi, iwe wa kijamii, kiuchumi au siasa," aliongeza.

Aliwataka wanamke wenye nia ya kuoongoza kutosisikiliza maneno ya watu wenye mitazamo isiokuwa na tija na badala yake waendelee kufanya kazi kwa bidi ili kuwahakikishia wananchi kuwa mwanamke anaweza kuongoza.

 Faki Ali ambae ni mkaazi wa meline nne,alisema  ni kweli baadhi ya watu wanawakwamisha wanawake wasitake kuwa viongozi kutokana na kuwepo na mtazamo hasi ya kidini.

 Zaliha salum ambae ni kijana aliewahi kutaka kuingia katika siasa lakini hofu ya dini yake imemsababishia kuachana na  nafkra hizo. 

Diwani  wa Jitimai  Mwanakwerekwe Unguja,  Asha Hassan alisema ameingia katika nafasi za uwongozi kwasababu anaamini dini yake ya Kiislamu inaruhusu mwanamke kuongoza, ijapokuwa baadhi ya masheikh wanarudisha nyuma maendeleo ya wanawake.

Aliwataka wanawake wenziwe kutokata tama na waendele kutekeleza ibada ya Mungu,huku wakiwa wanaendelea kupambana katika harakati za kuwa kiongozi.

Kwa ujumla yapo mabadiliko Zanzibar juu ya nafasi ya mwanamke katika uongizi, lakini bado panahitajika elimu na juhudi ili mwanamke wa Visiwani ajione hanyimwi haki ya kuongoza na anashirikiana na wanaume katika kuiletea jamii maenedeleo yenye maisha mazuri, raha na furaha.

  MWISHO

Comments