Skip to main content

MITAZAMO INAVYOCHANGIA WANAWAKE KUTOGOMBEA UONGOZI.

 



   NA AMRAT KOMBO, ZANZIBAR @@@@

Wapo wanawake ambao wanao uwezo mkubwa wa kuwa viongozi, lakini baadhi ya mitazamo katika jamii inawarudisha nyuma na kuamua kukaa pembeni.

Kwa bahati mbaya mitazamo hii,  inahusishwa na maelekezo ya dini kutokana na tafsiri potofu inayotolewa na badhi ya watu juu ya maelekezo ya dini na kuonekana kwa kiasi fulani.

 Hata utekelezaji wa mikataba ya kikanda na kimataifa juu ya haki na nafasi za wanawake, ikiwa pamoja na katika uongozi, ambayo nchi yetu imeiridhia inatekelezwa kwa kuchechemea au kufumbiwa macho kwa visingizio mbali mbali.

Miongoni mwa mikataba inayohimiza kulindwa kwa haki za wanawake ni tamko la kimataifa kuhusu haki za binadamu la 1948 ambao umelenga kutokomeza aina zote za kuwabagua  wanawake.

Kifungu cha pili cha Mkataba wa Afrika juu ya haki za binadamu,inajumuisha kanuni yakutobagua kwa misingi ya rangi, kabila ,jinsia ,lugha,dini,siasa au maoni mengine yoyote.

Zanzibar inayo idadi kubwa ya waumini wa dini ya Kiislamu (zaidi ya asilimia 95),ambao mwenendo wa maisha yao unaongozwa na melekezo ya dini yao na kila kukicha viongozi wake wa dini ya Kiislamu huikanusha mitazamo ya watu wanaokataa mwanamke kuwa kiongozi.

Miongoni mwa maelezo yanayotolewa kuonyesha dini ya Kislamu haikatazi mwanamke kuongoza ni nafasi walizopewa wanawake kuogoza katika enzi za mitume,ikiwa pamoja na wakati wa vita.

Mwanazuoni maarufu wa masuala ya dini ya Kiislamu, Profesa Issa Haji Zidi wa Zanzibar, amekuwa akisisitiza mara kwa mara kwamba dini ya kiislamu haijakataza kuwepo kwa kiongozi mwanamke, isipokuwa mwanamke anatakiwa kufuata,sheria na taratibu na Kiiislamu juu ya mwanamke awe na mwenendo gani wa kimaisha ndani na nje ya nyumba yake.

Alisema  katika enzi za Mtume Muhammad (S .A.W ) mwanamke alikuwa kiongozi katika vita na mambo mengine na kote aliweza kuifanya kazi hio kwa uweledi na uadilifu.

Mchungaji wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Shukuru Malonda, alisema mwanamke ana nafasi mbalimbali  za uwongozi, ikiwemo  ndani ya kanisa na kijamii.

Alitoa mfano wa viongozi wa kike waliongoza na kuwasimamia watu katika dini ya Kikirsto na kutaja kwamba miongoni mwao  Esta, ambae alikuwa Malkia na Debora (  kiongozi na hakimu wa wana wa Israeli) alikuwa nabii.

Anasema katika kanisa hilo wamewapatia nafasi sawa wanawake na wanaume ya kuongoza kanisa, ikiwemo nafasi ya wachungaji na nafasi ya wainjilist.

"Katika kanisa letu, tumewachaguwa wanawake wawili na wanaume wanne ambao ni wachungaji, pamoja na wainjilist 12 ikiwa wanawake watano na wanaume saba, wote kazi yao moja ya kuongoza kanisa,"alisema.

Licha ya serikali kusimamia maendeleo ya wanawake, lakini taasisi zisizoza kiserikali  wanaume na wanawake wanapata nafasi sawa za uongozi na hapana tatizo lolote.

Mratibu wa kuinua wanawake katika uongozi  katika Chama cha Waandishi wa Habari Wanwawe (TAMWA ZANZIBAR), Maryam Ame,alisema  haielewi dini inayokataza mwanamke kuwa kiongozi,ispokuwa jambo muhimu ni kuwa na uwezo na kuimudu nafasi hio.

"Tunatoa elimu kwa wanawake ambao wanahitaji kuwa viongozi ili wajitambue na kutatua changamoto zinazowakabili, vikiwemo vikwazo vya kusingizia dini," aleieleza.




Mapka hivi karibuni wanawake 172, wamepatiwa mafunzo ya uongozi Unguja na Pemba na kuwashauri wanaotaka kuingia kwenye uongozi wasiwe na hofu kwani katiba inawahakikishia haki hio ambayo inasisitizwa katika mkataba mbali mbali ambayo nchi yetu meiridhia.

Pamoja na hamasa  za serikali, asasi za kiraia na viongozi wa dini, lakini mwanasiasa Hamisa Mmnanga alisema bado ipo haja ya wakati wa uchaguzi  kuwepo na utaratibu bora utaowapa nafasi waliokuwa  mahodari, shupavu na jasiri kuwania nafasi hizo.

Diwani wa zamani wa Bububu, Amina Ali Mohamed, alisema mitazamo ya kidini inayoshadidiwa na baadhi ya watu imesababisha kuwepo mizozo na mara nyengine wanawake kudharauliana.

"Baadhi ya wananchi bado wapo nyuma katika kuhakikisha mwanamke anapewa nafasi ya uongozi, iwe wa kijamii, kiuchumi au siasa," aliongeza.

Aliwataka wanamke wenye nia ya kuoongoza kutosisikiliza maneno ya watu wenye mitazamo isiokuwa na tija na badala yake waendelee kufanya kazi kwa bidi ili kuwahakikishia wananchi kuwa mwanamke anaweza kuongoza.

 Faki Ali ambae ni mkaazi wa meline nne,alisema  ni kweli baadhi ya watu wanawakwamisha wanawake wasitake kuwa viongozi kutokana na kuwepo na mtazamo hasi ya kidini.

 Zaliha salum ambae ni kijana aliewahi kutaka kuingia katika siasa lakini hofu ya dini yake imemsababishia kuachana na  nafkra hizo. 

Diwani  wa Jitimai  Mwanakwerekwe Unguja,  Asha Hassan alisema ameingia katika nafasi za uwongozi kwasababu anaamini dini yake ya Kiislamu inaruhusu mwanamke kuongoza, ijapokuwa baadhi ya masheikh wanarudisha nyuma maendeleo ya wanawake.

Aliwataka wanawake wenziwe kutokata tama na waendele kutekeleza ibada ya Mungu,huku wakiwa wanaendelea kupambana katika harakati za kuwa kiongozi.

Kwa ujumla yapo mabadiliko Zanzibar juu ya nafasi ya mwanamke katika uongizi, lakini bado panahitajika elimu na juhudi ili mwanamke wa Visiwani ajione hanyimwi haki ya kuongoza na anashirikiana na wanaume katika kuiletea jamii maenedeleo yenye maisha mazuri, raha na furaha.

  MWISHO

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch