Skip to main content

SHEHA SHUNGI: ‘CHIMBENI MASHIMO SALAMA KUHIFADHIA MAJI TAKA’

 

NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

UONGOZI wa shehia ya Shungi wilaya ya Chake chake Pemba, umewataka wananchi, ambao bado hawajachimba mashimbo ya kuhifadhi maji taka, kufanya hivyo haraka, ili kuzuia uwezekano wa kukumbwa na magonjwa ya mripuko.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi shehiani hapo, Sheha wa shehia hiyo Hamad Ramadhan Soud, alisema shehia haitomvumilia mwananchi yeyote, anetiririshaji maja taka, kwani athari yake inaweza kuenea kwa shehia nzima.

Alisema, kila mwananchi ahakikishe amechimba shimo maalum na kisha kulifunika vyema, ili kuhifadhi maji anayotumia kutoka nyumbani mwake, badala ya kuyaacha yasambae.

Alieleza kuwa, maji yanayotumiwa hata kwa kukoshea vyombo au kukogea chooni, ndio chanzo cha magonjwa kama matumbo ya kuharisha damu, kipindu pindu na minyoo.

Sheha huyo alieleza kuwa, amekuwa akitoa elimu hiyo kila muda kwa wananci wake, ili kuona wanajikinga na magonjwa mbali ambayo yanaweza kusababishwa na maji taka.

‘’Niwatake wananchi wangu, haraka sana wale ambao hawajachimba mashimo ya kuhifadhi maji taka, kama vile yanayotiririka kutoka chooni, kufulia au hata ya kukoshea vyombo, wachimbe ili kuzuia maradhi,’’alifafanua.

Katika hatua nyingine, Sheha huyo amewataka wananchi, kuendelea kumpa taarifa pindi wakibaini kuwepo kwa mwenzao, anayetiririshaji taka, ili hatua za kinidhamu zichukuliwe.

Wakati huo huo, amewaahidi wananachi kuendelea kuwasiliana na wataalamu wa afya, ili kufika shehiani humo na kuwapa elimu juu ya namna bora ya kuyahifadhi maji taka.

 Mwananchi Asma Said Abdalla wa Chanjamjawiri, alisema lazima elimu iongezwe kwa wale wachache wanaoendelea kudharua, juu ya suala la uchimbaji mashimo ya kuhifadhi maji taka.

Kwa upande wake, Mbarouk Idrissa Omar wa Misooni shehiani humo, alisema hata suala la faini liweze kufanyakazi ikiwa, kuna mwananchi anashindwa kutekeleza agizo hilo.

Nao Asha Suleiman Hamad na Amina Suleiman Juma wa kijiji hicho, walisema wengi wao wameitikia wito wa uchimbaji mashimo, ingawa ni yale yanayojaa haraka.

‘’Kama kuna mfadhili, ni vyema akajitokeza, ili tumshawishi kutuchimba shimo moja kubwa, kwa kila baada ya nyumba tano hadi saba, ili kudhibiti maji hayo,’’walifafanua.



Mtaalamu wa magonjwa ya binaadamu kutoka Manispaa ya Chake chake Abubakar Khatib Bakar, alisema Manispaa hufanya mara kwa mara msako wa nyumba hadi nyumba, ili kuwabaini wananchi wanotiririsha maji taka.

Alisema, kwa sasa wamo kwenye mpango kabambe wa kuhakikisha ndani ya miaka 10 ijayo, hakuna magonjwa ya mripuko, na sasa wameshatimiza miaka mitano, bila ya ugonjwa huo.

‘’Manispaa ya Chake chake imejipanga, ili kuona ndani miaka 10 hakuna mgonjwa ya mripuko, na ndio maana tukimgundua kwa mara ya kwanza, anapigwa faini ya shilingi 20,000 lakini mara ya pili anafikishwa mahkamani, na faini isiyopungua shilingi 250,000,’’alifafanua.

Hata hivyo, amewakumbusha wananchi wanaonzisha ujenzi wa nyumba, kuhakikisha wanafanya kila namna, ili kudhibiti maji taka, ambayo athari yake pia ni kusababisha ugonjwa wa ngozi.

Shehia ya Shungi iliyopo wilaya ya Chake chake Jimbo la Chonga, inao wananchi 3,884 ambapo inaundwa na vijiji vya Missoni, Shungi, Kiziwani, Chanjamjawiri, inayomiundombinu ya elimu, afya na barabara.

                 Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch