Skip to main content

TAMWA -ZANZIBAR YAWAKUMBUSHA JAMBO WANAMTANDAO PEMBA

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA:::

CHAMA cha waandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar, kimewataka wanamtandao wa kupinga matendo ya ukatili na udhalilishaji kisiwani Pemba, wasikatishwe tamaa, kwa kuibuka kwa matendo hayo kila siku, ni ishara wananchi wapeta uwelewa.

 

Hayo yameelezwa na Afisa Tathmini na ufuatiliaji kutoka TAMWA-Zanzibar Mohamed Khatib, kwenye kikao cha siku moja cha kuwasilisha ripoti ya utendaji kazi wa wanamtandao hao, kilichofanyika mjini Chake chake.

Alisema kazi kubwa imeshafanywa na inaendelea kufanywa na wanamtandao hao, na ndio maana katika siku za hivi karibuni, wanaodhalilishwa wamekuwa wakieleza.

Alieleza kuwa, ongezeko la takwimu ya matendo hayo pamoja na wanaotendewa na hata watu wao wa karibu kuripoti, ni dalili kuwa, sasa jamii imepata mwamko.

Afisa huyo aliwataka wanamtandao hao, kutokatishwa na tamaa na ongezeko la matendo hayo, ambapo hilo linatokana na matumizi sahihi ya kuifikisha elimu.

‘’Hivi sasa mtoto anadhalilishwa na baba yake, kaka yake, au mwalimu wake na kisha anathubutu kutoa taarifa hizo, ni ishara kuwa, kila mmoja elimu imemfikia,’’alieleza.

Hata hivyo, amewataka wanamtandao hao kisiwani Pemba, kuegemea zaidi sasa katika mwaka ujao, kuishawishi jamii kufika mahakamani, kutoa ushahidi.



Akizungumza kwenye ufunguzi wa kikao hicho, Mratibu wa TAMWA Zanzibar ofisi ya Pemba Fat-hya Mussa Said, aliwataka kuendelea na utoaji wa elimu kwa jamii, ili kila mmoja atimize wajibu wake.

‘’Inawezekana baba anaona kama wajibu wa kumlea mtoto ni wa mama peke yake, na yeye akishapata huduma za ndani, kama vile wajibu wake umekwisha, jambo ambalo sio sahihi,’’alieleza.

Hata hivyo Mratibu huyo wa TAMWA, amepongeza kazi kubwa inayoendelea kifanywa na wanamtandao hao, na hasa katika kuwafikia wananchi walioko vijijini.



‘’Tutangalia namna ya kuwawezesha japo kidogo, ili mwaka ujao wa 2023, muwe na uwezo wa hali na mali, kuwafikia wananchi wanaoishi katika visiwa vidogo vidogo,’alileza.

Akizungumza katika kikao hicho, kwa niaba ya wanamtandao wa wilaya ya Mkoani, Shaaban Ali alisema bado changamoto wanazopanga kuzifanyia kazi, ni rushwa mauhali.

‘’Elimu tunatoa mno katika ngazi ya jamii, vyuo vya qur-an, skuli na masokoni, lakini bado matukio mengine hayafiki mahakamanim kwa sababu ya watendewa kutawaliwa na rushwa muhali,’’alieleza.

Nae Rashid Mshamata wilaya ya Wete, alisema matukio mengine ya ubakaji, yanayowahusu watoto wenye miaka 16 na 17, ndio yanayoshindwa kuendelea, mbele ya vyombo vya sheria.

‘’Anaweza kuja mzazi kwa hasira na kutaka mtuhumiwa aliyemdhalilisha mtoto wake akamatwe hisia sasa na haraka, lakini kesi ikishafika mahakamani, huanza kukosa ushirikiano, na kisha hufutwa,’’alieleza.



Mratibu wa wanawake na watoot shehia ya Kangagani Awena Salim Kombo, alisema bado kesi zinazowahusu watoto wa viongozi, zimekuwa zikimalizwa kienyeji.

Nao mwanamtandao kutoka wilaya ya Wete Siti Faki Ali na mwenzake Haji Shoka Khamis wilaya ya Mkoani, wameitaka TAMWA kwa mwaka ujao, kuangalia zaidi elimu katika visiwa.



Akifungua kikao hicho Afisa mradi kutoka TAMW Zaina Salim Abdalla, alisema kazi iliyopo mebele ya wanamtandao hao, sasa ni kuishawishi jamii, kufika mahakamani kutoa ushahidi.

‘’Kwa ule Unguja, wananchi wameshahasika vyema, lakini kazi inakuwa kwa wasimamizi wa sheria, na hasa kufuata haki kwenye eneo la hukumu,’’alieleza.



Moja ya jukumu lake la msingi TAMWA ni kuhakikisha wanawake na watoto wanaishi bila ya kukumbwa na majanga mbali mbali ikiwemo utelekezwaji, udhalilishwaji na ukatili.

                                      Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch