Skip to main content

KUMBE SIFUNI NDIE KATIBU MKUU WA MWANZO PACSO MWANAMKE

 

NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@

SIFUNI Ali Haji ni Katibu Mkuu na ni kiongozi wa mwanzo, anaefanya kazi na mtandao wa asasi za kiraia katika kisiwa cha Pemba, akiwa wa kwanza mwanamke.

Anasema mtandao huo unaojulikana kwa jina la PACSO, ni Umoja wa Jumuiya zisizo za kiserikali uliyoanzishwa mwaka 2005.

Katika safari ya uongozi wake, anaendelea kuzisimamia jumuiya na wanachama waliokuwa Pemba ikiwemo Pegao, Juwauza, na Tamwa.

Sifuni anaendelea kuvunja vikwazo vyake, katika Jumuiya hiyo kwa zaidi ya miaka sita, akilenga macho yake katika mkoa wa kusini na kaskazini mwa mji wa Pemba.

Kutokana na juhudi zake na moyo wa kujituma, amekuwa akilenga uwezo wa kusimamia maendeleo endelevu kwa jamii ya kisiwa hicho.

‘’Nafasi hii haikuja tu, baada ya juhudi zangu nilizokuwa nikizifanya katika uwanachama wangu, ndipo nilipopigiwa kura kwa asilimia zote kushika nafasi ya katibu, anafafanua.

Zaidi ya mwaka mmoja taasisi hiyo, haikuwa na mafaniko yoyote baada ya kusimamiwa na wanaume, ndipo ilipofika mwak 2006 Sifuni alipojitolea na kuisimamia.

Katika kujinyakulia nafasi ya ukatibu, ni mwanamke wa kwanza aliyejiamini, asiyekubali kukatishwa tamaa na amekuwa na jukumu kubwa la kuratibu na kuunganisha mashirika yasiyo ya kiserikali NGOs,.

Sifuni ni mwanamke anayeaminika katika kisiwa hicho, katika kujenga uwezo, kutoa mafunzo na kuongeza ujuzi kwa wanachama na asasi zilizomo kuwa na ufanisi.

 Kupitia uongozi wake, ameweza kuunganisha ushirikiano wa maendeleo kwa jamii katika kufanya mikutano, ndani yake akiwalenga wanawake, vijana na watu wenye ulemavu.

Haijawahi kutokea kutokana na mchango wake, amekuwa akikuza misingi ya utawala bora na ustawi wa wananchi wote wa Pemba.

Ni mwananmke anayesimamia utekelezaji, utamaduni na uwajibikaji, pamoja na kusaidia utoaji wa huduma za kijamii na kiuchumi.

Amekuwa akiwajibika kwa kusaidia mipango ya Serikali, kuunga mkono juhudi katika kuboresha uchumi wa wananchi, kupitia malengo ya kitaifa na Malengo ya Maendeleo Endelevu SDGs.

Ingawa hapo awali alianza kufanya kazi katika jumuiya ya kuhifadhi mazingira mwaka 1996 na alikuwa mwanamke wa kwanza akihamasisha jamii juu ya matumizi mabaya ya kasa.

Na aliweza kuihamasisha jamii, kutokana na athari za utumiaji wa kasa na utoaji wa elimu kwa wananchi, hususan kwa ukanda wa pwani.

Baada ya uhamasishaji huo, aliunda vikundi vya wajasiriamali vya mboga mboga, akiwa kiongozi na alikuwa na nafasi ya katibu kwa kuwasaidia wanawake wenzake.

‘’Katika vikundi vya wajasiriamali niliweza kufanya maendeleo mazuri, kwa kuvisimamia juu ya upandaji wa miti na mazao ya mboga mboga,’’anaelezea.

Vikundi hivyo alivionesha njia na amevihamasisha na aliwataka wanawake wasikae nyuma katika kujiinua kiuchumi.

Mbali na kupitia nafasi hizo, kumbe Sifuni alianza uongozi tangu akiwa skuli ya msingi vitongoji wilaya ya Chake chake, akisimamia wanafunzi wenzake.



Wakati anasoma skuli hiyo, alikuwa kiongozi wa darasa na alipenda sana, kujishughulisha na kuuchanganyika na wanafunzi wenzake.

Alipopewa shughuli, alikuwa akizitekeleza na kuzisimamia vizuri na walimkubali juu ya utendaji wake.

Mwaka 1990 aliajiriwa kuwa mtumishi wa umma, huku akijihusisha na asasi na jumuiya, akiendeleza vikundi vya wajasiriamali bila muingiliano wa ajira na uongozi wake.

Kutokana na uwezo alionao juu ya uongzo wake, haikuathiri majukumu aliyokuwa akiyafanya hata akiwa nyumbani kwake.

Ingawa aliwahi kugombania nafasi ya uwakilishi katika jimbo la Ole, mwaka 2020 ila hakubahatika na alionesha uthubutu.

Nafasi hiyo ilimpa matumaini na aliweza kuchuana na mwanamme ila hakuonesha kushindwa baada ya kupata kura moja.

Kutokana na harakati Sifuni anatamani kuwa kiongozi, maana sifa za mwananmke kiongozi ni kusikiliza ushauri na maoni na wala siyo kutetereka wala kuburuzwa.

Kwa sasa Sifuni ni Katibu wa umoja wa jumuiya zisizo za kiserikali Pemba na anajivunia kuwa yeye ni mwanamke wa mwanzo katika jumuiya hiyo.

Mafanikio makubwa ameyapata katika uongozi wake kupitia asasi hiyo, ameweza kuingiza fedha zisizopungua zaidi ya shilingi milioni 700 kwa wastani wa miradi 10 kwa sasa.

WATU WA KARIBU

Mkrugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Asasi za Kirai PACSO Mohamed Najim anasema, Sifuni amekuwa kiongozi mzuri, na mwenye ushirikiano na jamii anaependa kujitoa na kujitolea kwa kufanikisha harakati za maendeleo.

‘’Amekuwa na mawasiliano mbalimbali ndani na nje ya nchi ili kuhakikisha jamii, inanufaika katika kupata maendeleo kupitia asasi hii ya kiraia,’’anafafanua.

Suleiman Hamad Salim ni mume wa Sifuni anasema, amekuwa na ushirikiano mkubwa na wanajamii wa kisiwa cha Pemba, katika kuhamasisha maendeleo na utatuzi wa changamoto zinazowakumba.



Kaimu Mratibu wa chama cha waandishi wa habari wanawake TAMWA- Pemba Amina Ahmed anasema, amekuwa akimjua kwa kuzijengea uwezo jumuiya hiyo na wanachama, katika kufikia malengo yao ya kikatiba.

Amekuwa kiongozi mzuri, katika kuimarisha uwezo wa kiutendaji na amekuwa mstari wa mbele katika utetezi wa haki za jamii.

Ali Abdalla Bakari ni mwanajamii wa Chake chake anasema, amekuwa akimjua Sifuni, kwa ucheshi na ni mchapakazi mwenye moyo wa kujituma na kuwa tayari katika majukumu yake.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya uhifadhi na utunzaji wa mazingira Vitongojo VECA Ali Abdalla Juma anasema, kiongozi huyo ni mwenye uzalendo na moyo wa kujitolea.

Fatma Suleiman Hamadi ni mtoto wa Sifuni anasema, hata yeye amerithi uongozi kutoka kwa mama yake kwani amepata mafunzo kupitia asasi hiyo huku akiwa kiiongozi kwenye jumuiya yake.

Sifuni ni mzaliwa wa shehia ya Vitongoji wilaya ya Chake chake mwaka 1968 na ni mama mwenye familia ya watoto sita aliyesoma skuli ya Vitongoji tangu elimu ya msingi hadi sekondari.

Mwaka 2022 Sifuni alistaafu utumishi wa umma na amejikita katika asasi hiyo, kuwa kiongozi mwenye busara na matumaini ya watu wa Pemba.

 Wanaharakati na kiongozi wa dini wanalipi

Afisa Program wa chama cha waandishi wa habari wanawake Zanzibar TAMWA Khairat Ali anasema, amewajengea uwezo waandishi wa habari katika kuandika habari zinazozingatia haki za wanawake katika uongozi, demokrasia na zinazochangia maendeleo ya jamii.

‘’Tupo hapa kuwafundisha masuala ya takwimu kwa sababu tunataka kuona jitihada zenu katika kushughulikia masuala ya wanawake na uongozi zimefika wapi, zinaleta mafanikio kwa kiwango gani na jamii imezipokea kwa namna gani,’’anafafanua.

Sophia Ngalapi ni mkuu wa mawasiliano chama cha waandishi wa habari wanawake Zanzibar TAMWA anasema, ni vyema waandishi wa habari kuwaibua wanawake ambao wana uwezo wa kuongoza kwenye jamii ili kusaidia kuchapuza maendeleo.



Anasema kuwa wapo viongozi wanawake, wanawajibika ipasavyo katika majukumu yao na kuibadilisha jamii kwa kutatua changamoto zilizopo ili kufikisha maendeleo kwa haraka.

Mratibu kutoka Ofisi ya Mufti Shehe Said Ahmed Mohamed anasema, katika dini ya kiislamu nimeweka wazi nafasi ya mwanamke katika uongozi, kwani amekuwa mtu bora katika kusimamia na uislamu hauna shaka.

Yohana Ali Mfundo ambae ni Mchungaji kutoka Kanisa la Mkusanyiko wa Mungu Tanzania (TAG) lililopo Ngerengere Chake chake anasema, dini yao haijabagua mwanamke asiwe kiongozi, isipokuwa aendeshe kwa kufuata taratibu na sheria zinavyoelekeza.

MIKATABA

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lililotolewa na azimio Oktoba 31 mwaka 2000, limesema kuongezeka ushiriki wa wanawake katika ngazi za maamuzi, inazidisha semokrasia ya nchi, uchumi, amani na utulivu.

Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, kifungu cha 21(1) kinaeleza kila Mzanzibar anayo haki na uhuru wa kushiriki kikamilifu, katika kufikia uamuzi juu ya mambo yanayomuhusu mwanamke.

Mkataba wa Kikanda wa Nchi za Kusini mwa Afrika, uliotiwa saini mwaka 2008, kupitia Ibara ya nambari 13 kinaeleza kuwekwa mikakati madhubuti ya kuwawezesha wanawake.

Taarifa ya wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Waze na Watoto Zanzibar ya mwaka 2024/2025 imebainisha kuwa, tafiti zinaonesha kuwa nchi zinazozingatia usawa wa kijinsia zimeweza kuimarika kiuchumi kwa  kasi kuliko nchi  ambazo hazizingatii.

Mkataba wa Kimataifa wa Kutokomeza aina zote za Ubaguzi dhidi ya Wanawake mwaka 1979 katika kifungu cha 5.2.1 umefafanua kuwa, kuondosha ubaguzi dhidi wanawake na kuhakikisha kuwa wanafaidika na haki sawa za kiuchumi kijamii, kisiasa na kiraia.

 Mkataba wa Wanawake Barani Afrika wa mwaka 2003 na umepitishwa na wakuu na Serikali za Afrika huko Maputo, katika kifungu 5.2.2 unalinda haki za wanawake juu ya aina yoyote ya ubaguzi.

Sera ya Maendeleo ya Wanawake na jinsia ya mwaka 2000 ya Taifa katika kifungu cha 5.2.3 kinaeleza kuwa inatoa mwelekeo, mikakati na shughuli mbali mbali za uongozi na maendeleo inazingatia usawa wa kijinsia.

Na katika Malengo ya Maendeleo Endelelevu lililoanza mwaka 2015 mpaka 2030 kuhusu lengo 16 limezungumzia kujaza jamii zenye amani na zilizojumuishi kwa maendeleo endelevu na kuwezesha upatikanaji wa haki kwa wote.

    MWISHO.

 

 

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...