Skip to main content

KAMATI KUFANIKISHA TAMASHA LA 31 UTAMADUNI WA MZANZIBARI ZAZINDULIWA PEMBA

 



NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@

KAIMU Ofisa Mdhamini Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Pemba, Sharifa Hamad Shapandu, amezitaka kamati za kufanikisha tamasha la 31 la utamaduni wa mzanzibari, kuhakikisha zinafanyakazi kwa kushirikiana, ili kufanikisha tamasha hilo.

 

Ameyasema hayo August 18, 2026, ofisini kwake Gombani Chakechake Pemba, mara baada ya kuzizindua kamati hizo tano, kuelekea uzinduzi wa tamasha hilo mwishoni mwa mwezi ujao, kisiwani humo.

 

Alisema kuwa, kuwepo kwa kamati hizo anataka iwe ni njia rahisi ya kufanikiwa kwa tamasha hilo, ambalo kwa awamu hii, linatarajiwa kuwa la aina yake.

Alieleza kuwa, njia ya kuzigawa kwa kamati hizo, ni namna ya kuwa na na urahisi wa ufuatuliaji, ingawa isiwe chanzo cha kukosa kushirikiana.

 

‘’Najua kuwa zipo kamati tano, zinawajumbe wenye uwezo na maarifa yasiofanana, lakini hili sasa muwe na ushirikiano kwa pamoja, ili kulifanikisha hili,’’alifafanua.

 

Aidha Kaimu Ofisa Mdhamini huyo, amewataka wananchi kushiriki kikamilifu katika tamasha hilo, tangu kuanza kwa uzinduzi wake wilaya ya Micheweni, ili kujionea mambo mbalimbali ikiwemo, utamaduni wa kizanzibar, michezo, maigizo na ngoma za asili.

"Wananchi wote nawaomba mushiriki kikamilifu, katika tamasha hili la utamaduni wa mzanzibari, ikiwa ni njia moja wapo ya kujionea utamaduni wetu na wingine kujikumbusha,’’alieleza.

 

Mapema Mkuu wa Divisheni na Utamaduni Pemba Hamad Ali Haji, alisema tamasha hilo litakuwa la aina yake kwa mwaka huu, kwa kuvishirikisha zaidi ya vikundi 10 vya ngoma asili, kutoka Unguja na Pemba.

 

Alisema, tangu kuanzishwa kwa tamasha hilo, kwa mwaka huu, ambalo ni 31, kwa wanachi watakaojitokeza wataniufaika na mambo makubwa, ikiwemo resi za ngalawa, Punda, msewe wa zamani na sasa, taarab asilia na mbio za baiskeli.

 

‘’Kwa mwaka huu wizara yetu ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, chini Waziri Riziki Pembe Juma Khamis na Katibu Mkuu Matar, tamasha hili, litakuwa la kuvutia na si la kukosa,’’alisisitiza.

 


Katika hatua nyingine, alisema tamasha hilo kwa kuanzia, litazinduliwa Septemba 19 hadi 23 mwaka huu kisiwani Pemba, wilaya ya Micheweni na mgeni rasmi akitarajiwa kuwa, Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar Hemed Suleiman Abdulla.

 

Alifafanua kuwa, kwenye uzinduzi wa tamasha hilo, utafuatiwa na matembezi ya wajasiriamali, wasanii wa ngoma za asili, utenzi na shamra shamra nyingine za kulipamba.

 

Siku ya pili, tamasha litahamia wilaya ya Wete, litanogeshwa na maulidi ya home, nasheed, dufu na maigizo yanayohusiana na tamaduni wa kiislam na kizanzibari.

 


‘’Wananchi wa wilaya ya Wete, wanakaribishwa siku hiyo, ukumbi wa zamani wa baraza la Wawakilishi, ambapo hakutakuwa na kiingilio,’’alisema.

Aidha Mkuu huyo wa Divisheni ya Utamaduni Pemba, alisema Septemba 21, kutakuwa na mashindano ya ngalawa, yatakayoambatana na sarakasi na ngoma za asili Mkoani, na siku inayofuata ni mchezo Ng'ombe uwanja Pujini.

 

 ‘’Niwaarifu wananchi wa Pemba, tamasha hili litahitimishwa Septemba 23, kwa usiku wa sanaa, pamoja na wajasriliamali, wakionesha shughuli mbalimbali, zikipambwa na kwa taarabu, uwanja wa Gombani, kabla ya kilele Septemba 25 Unguja,’’alieleza.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa kamati ya Habari na Burudani Adam Ramadhani Kombo, ameipongeza wizara, kwa kuendeleza tamasha hilo na kuahidi kamati yake, itafanyakazi kwa karibu na wizara, ili kufanikisha shughuli hiyo.

 

Aidha aliwataka wajumbe wa kamati hiyo, kuhakikisha, kazi na majukumu waliyopewa wanayafanya kwa ufanisi, ili kuhakikisha wananchi wote wanapata taarifa.

 


Hili ni tamasha la 31, la utamaduni wa mzanzibari, kufanyika Unguja na Pemba, ambapo kwa mwaka huu, uzinduzi wake unatarajiwa kufanyika Micheweni Septemba 19 mwaka huu.

 

                           MWISHO.

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...