Skip to main content

MBINU ZA DK. MWINYI UIMARISHAJI BANDARI YA MKOANI PEMBA, MATUNDA YAONEKANA KWA MACHO SASA

 


 NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@

UNAPOZUNGUMZIA juhudi za serikali, katika kuiletea Pemba maendeleo ya kiuchumi, huwezi kuacha uimarishaji miundombinu ya bandari ya Mkoani Pemba.

Bandari ambayo ni sehemu muhimu katika uchumi wa watu wa kusini Pemba na kisiwa kizima kwa ujumla.

Kutokana na umuhimu wa bandari hiyo, serikali imekuwa ikiimarisha kwa kuifanya kuwa ya kisasa zaidi, ili kutoa huduma bora kwa wananchi.

Kwani kumekuwa na maboresho makubwa, yanayo husisha gati ya kisasa, ujenzi wa jengo la abiria, njia ya kupitia abiria na kuongezwa kwa eneo la bandari kavu, kwa kuwekwa eneo maalumu la kutunzia makontena ya mizigo.

Mkurugenzi wa Shirika la Bandari Pemba Abdalla Salim Abdalla, anasema bandani ya Mkoani ni ya pili kwa ukubwa visiwani humo, ikipokea meli kubwa za mizigo kutoka nchi mbalimbali na kukuza uchumi wa kisiwa hicho.

Anasema, maboresho hayo yanalenga kuziwezesha meli za kisasa za mwendokasi, kuegesha kwa urahisi na usalama na kurahisisha safari za boti baina Unguja, Pemba na Tanga.

Kwakuona umuhimu wa Bandari hii, serikali imewekeza kiasi cha Dola za Marekani milioni1, kwa maboresho ya gati pekee.

Ambapo kumbe lengo ni kuziwezesha meli za kisasa za mwendokasim kuegesha kwa urahisi na usalama, ili kurahisisha safari za boti baina miji ya Unguja, Pemba na Tanga.


Ikafahamika kuwa, gati hiyo yenye urefu wa mita 300 na upana wa mita 25
0, kwa sasa imekuwa ikipokea wastani wa  meli 80 na majahazi 15 kwa mwezi.

Tena kati ya hizo, zimo meli za abiria, za makontena pamoja na mizigo kutoka miji ya Mombasa na Uturuki na majahazi kutoka mkoa wa Tanga.

Maana kabla maboresho hayo, uingiaji wa meli na majahazi ulikuwa mdogo, kwani kwa mwezi hazikufika hata meli 30.

Hii inathibitisha kwamba, maboresho hayo ni mapinduzi makubwa ya sekta ya bandari, ambayo ni miongo ni mwa sekta muhimu inayo waunganisha raia kutoka sehemu moja kwenda nyengine.

Kwani wizara ya Ujenzi Mawasiliano na Uchukuzi, imesema kwa kipindi cha Julai 2025 hadi Machi 2026, mamlaka imehudumia abiria 2,108,239.

Amba hao ni wale wanao safiri kupitia bandari za Unguja na Pemba, kati ya hao 86, 442 kwa Pemba pekee.



Hii inaonyesha umuhimu wa sekta ya bandari  katika kurahisisha safari za wananchi wa Unguja na Pemba na maeneo mengine.

Ali Abudu Mzee ni Mwenyekiti bodi ya Shirika la bandari, anafahamisha maboresho hayo ya gati hiyo, pia yalienda sambamba na maboresho ya njia ya kupitia abiria, yenye urefu wa mita 150 na upana wa mita 2.5.

Kwani njia hiyo iliowekwa mabati juu na uzio pembeni, inalenga kuongeza usalama wa abiria, wakati wanapokwenda kupanda meli ama boti kwa safari zao mbalimbali.

Wananchi wanaotumia bandari hiyo kusafiria wanaeleza, kabla ya ukarabati huo, walitembea urefu huo wa mita 150, katika mazingira magumu  ambayo jua na mvua viliishia mwilini mwao.

“Kabla maboresho haya, tulikuwa tukipata shida sana, kwani tulitembea masafa katika mazingira yasio rafiki, jua na mvua vilikuwa lazima kwetu,’’anasema Omar Haji Makame.

Aisha Hassan Hassnuu anasema maboresho mengine yaliofanywa bandarini hapo, ni ya utanuzi wa njia ya kupitishia vitendea kazi, sasa umewapa usalama zaidi.

Mwananchi Asha Salim Mohamed anasema bei za bidhaa kama mchele, sabuni na vyengine zinapungua.

“Kabla maboresho ya bandari ambapo Kontena za mizigo zilishushiwa Unguja bei za bidhaa zilikuwa juu, wafanyabiashara walililia sana usafiri lakini kwa miaka miwili hii ni nafuu sana kwetu” anaeleza.

 


Nae Mwanajuma Hija Said, anaamini kuwa hayo yaliofanywa na Dk. Mwinyi yanalenga kuimarisha usalama wao, na utoaji huduma bora.

Kwani kwasasa bandari ya Mkoani ni sehemu muhimu ya kuiunganisha Pemba na sehemu nyengine, hasa katika uwanja wa kiuchumi.

Aidha maboresho mengine yaliofanyika ni yale ya utanuzi wa eneo la bandari kavu, inaosimamiwa na kampuni ya Fumba Ports, inayojumuisha ghala la kuhifadhia kontena.

Eneo hili lenye ukubwa wa mita za mraba 420, limezungushiwa uzio wenye mfumo wa usalama wa umeme, na lina uwezo wa kuhifadhi makontena 580 kwa wakati mmoja.

Kazi hii iliyofanywa na serikali ya awamu ya nane, lengo ni kurahisisha shughuli za upakiaji na upakuaji wa makontena ya mizigo, yanayo kuja au kupelekwa nje ya nchi.

Oktavian Mbela Kilei ni Msimamizi mkuu wa shughuli za bandari kavu, kutoka kampuni ya Fumba Ports anasema, hadi Mei 2026 makontena 930 za mizigo, imepokelewa, na kontena 793 zimesafirishwa, kati ya hizo 38 ni zilizojaa mizigo.

“Toka kuzinduliwa rasmi sehemu hii ya kuhifadhia makontena mwaka 2024 hadi Mei 2026 tumeshasafirisha, makontena 793 za mizigo na kontena 930 zimepokelewa kutoka nchi mbalimbali”, anaeleza.

Kumbe eneo hilo, ni kwa ajili ya meli kupakuwa mizigo, kufanyiwa upekuzi, kupakiwa pamoja na uwekaji wa makontena.

Tena akasema michakato yote hayo huhusisha taasisi mbalimbali za serikali ikiwemo Taasisi ya Viwango Zanzibar ‘ZBS’, Wakala wa Chakula, Dawa na Vipodozi Zanzibar ‘ZFDA’ na nyenginezo.

Akafafanua kuwa, chakujivunia ni upakuaji mizigo hufanywa ndani ya siku mbili hadi saba, tofauti na zamani ikichukuwa zaidi ya siku 30 mpaka kukabidhiwa kwa wenyewe.

Msimamizi huyo kutoka Fumba Ports anaeleza, makontena hayo mara nyingi huja na bidhaa kama sabuni, Mchele, Mafuta, Nondo na Misumari.

Anafafanua kwa upande wa upakiaji kontena hizo hupakia bidhaa kama karafuu, mafuta ya karafuu, mwani, kombe na chaza.

Anaeleza malengo ni kuongeza uwelewa kwa wafanyabiashara wa nchi mbali mbali, ili waweze kuitumia zaidi bandari hiyo.

Anamatumaini kwamba, jambo hilo litawezesha kuongeza idadi ya makontena yanayoingia na kutoka, kwani lengo ni kufikia tani 10,000 kwa mwaka.

Mfanyabiasha Suleiman Mohamed Said anaeleza kabla ya maboresho hayo, walipata usumbufu mkubwa, wanaposafirisha bidhaa zao, kwani walisubiri muda mrefu.

“Zamani tulikuwa tukiagiza mizigo inachukuwa siku hadi 30 kuupata, wakati mwengine bidhaa zinaharibika, ingawa sasa siku mbili, kontena zinapakuliwa kwa kuchelewa siku saba, ni faida kwetu,’’anaeleza.

Stadi Seif Haji ndie Msimamizi kitengo cha Marine bandari ya Mkoani Pemba anasema, kabla kuwepo kwa mradi wa ’contena Yard’ kisiwani Pemba, mizigo ilipakiwa katika meli za abiria.

Akizitaja kama vile za Azam sealink na Ikram sealine, kupelekwa Unguja kwa ajili ya kufanyiwa upakiaji na kusafirishwa.

“Kwa sasa huduma za usafirishaji zimeimarika Pemba, michakato ya upakiaji na usafirishaji hufanyika hapa bandari ya Mkoani na bidhaa kusafirishwa moja kwa moja, katika nchi ilio kusudiwa sio kama zamani”, anafafanua.

Mbali na manufaa ya kiuchumi, sasa bandari ya Mkoani, imesaidia kutoa ajira kwa wazawa, kwa asilimia 75 ya wafanyakazi katika eneo hilo ni wa Pemba wenyewe.



Hii inaonyesha kufanikiwa kwa lengo la serikali ya kuhakikisha vijana wanapata fursa za ajira zilizopo katika maeneo yao.

Mitandao ya kijamii, inaripoti kuwa, tafiti zinaonyesha nchi zinazoendelea, zinatazama bandari kama chanzo muhimu cha kipato na maendeleo ya nchi.

Wakati bandari kubwa ulimwenguni zinapakia na kupakuwa hadi tani milion 744 za shehena kwa mwaka.

Ilifahamika kuwa, kwa Zanzibar kwenye hutuba ya bajeti ya wizara ya Ujenzi na Uchukuzi Zanzibar ya 2026/2027, imebainisha kuwa, shehena za mizigo mchanganyiko 802,584 ziliingia nchini kwa kipindi cha Julai mwaka 2024 hadi Machi jana.

Huku ikifahamika kuwa, shehena 1,452, 665 zikiingia Zanzibar kwa kipindi cha Julai 2025 hadi Machi 2026, sawa na ongezeko la asilimia 81.

Aidha makontena 65,476 yalioingia Zanzibar kwa kipindi cha Julai 2024 hadi Machi 2025, huku makontena 73,450 kwa kipindi cha Julai 2025 hadi Machi 2026, ikiwa ni ongezeko la asilimia12.2.

Vile vile hutuba hiyo inaeleza utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa bandari ya Mkoani umefikia asilimia 73 ya kazi zote, zilizopangwa na hadi kufikia Machi  2026 na zaidi ya shilingi bilioni 3.094 zimetumika.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi ndie aliezindua meli ya kwanza ya makontena, bandarini hapo na kuwataka wafanyabiashara, kutumia fursa hiyo.

Septemba 2024 meli ya Lamu Shipping Limited, ilishuhudiwa na wazanzibari ikishusha kwa mara ya kwanza makontena kwenye Bandari ya Mkoani.

Mbali ya maboresho ya bandari ya Mkoani, pia Pemba kuna ujenzi wa bandari ya mizigo ya Wesha na bandari ya abiria ya Shumba mjini, itakayo waunganisha wananchi wa kisiwani humo na nchi jirani ya Kenya.

                            MWISHO.

 

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...