Skip to main content

MAMA MARIAM MWINYI: 'WAZAZI ZINGATIENI MALEZI NA MAKUZI BORA KWA WATOTO'

 


IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA 

MKE wa Rais wa Zanzibar, Msarifu na Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa Taasisi ya Zanzibar Maisha Bora Foundation (ZMBF), Mama Mariam Mwinyi amesema ana imani kuwa malezi na makuzi bora ya awali ya mtoto ni msingi imara wa kujenga taifa lenye raia wenye afya, elimu, nidhamu na maendeleo endelevu.

Mama Mariam Mwinyi ameyasema hayo Agosti 13, mwaka 2025, wakati alipozindua Kampeni ya Malezi na Makuzi ya Awali ya Mtoto wa Zanzibar (ECD) katika viwanja vya Kisonge, Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja.

Amesema kuwa, ni vyema kwa jamii kuhakikisha inawapatia watoto malezi na makuzi bora ya awali, ili kuwajengea mustkbali wa maisha bora ya baadae.


Mama Mariam Mwinyi ameeleza kuwa, ZMBF imekuwa mstari wa mbele kusaidia maendeleo ya makuzi ya mtoto, hususan katika programu za lishe pamoja na huduma za afya ya mama na mtoto, ambapo kupitia jitihada hizo, imeweza kuwafikia wanufaika zaidi ya 50,000 katika Shehia 67 na vijiji 644 vya Unguja na Pemba.

Alisema kuwa, kupitia kampeni ya Afya Bora Maisha Bora, kambi za matibabu bure zilizoendeshwa na ZMBF zimewafikia wananchi 21,000 na huduma hizo zimejumuisha elimu ya lishe, elimu ya malezi na makuzi, matibabu kwa watoto wenye utapiamlo, utoaji wa chanjo, pamoja na huduma za afya ya mama na mtoto.

Aisha amefahamisha kuwa, uzinduzi wa kampeni hiyo haipaswi kuwa tukio la siku moja, bali iwe ni harakati ya muda mrefu na endelevu ili kuhakikisha kila mtoto wa Zanzibar, kuanzia hatua ya mama katika ujauzito hadi umri wa miaka minane, anapata haki zake za msingi ikiwemo afya bora, lishe sahihi, ulinzi, malezi na mazingira salama ya ukuaji kwa ajili ya kufikia utimilifu wake.

Kwa upande mwingine, Mama Mariam Mwinyi ametoa wito maalum kwa sekta binafsi na mashirika ya maendeleo kuendeleza ushirikiano na Serikali katika uwekezaji wa malezi na makuzi ya awali ya mtoto.
Kwa upande wake Waziri wa Afya Zanzibar Nassor Ahmed Mazrui alisema, siku ya uzinduzi huo ni ya kihistoria kwa Zanzibar kwani inaanza hatua mpya ya kuhakikisha watoto wanapata mwanzo bora maishani.         

Alisema kuwa, utafiti wa kisayansi na uzoefu wa kitaifa na kimataifa vinaonesha bayana kuwa, miaka ya mwanzo ya maisha ya mtoto ndio msingi wa afya, akili na utu wa mtu mzima wa baadae, hivyo jamii ikiimarisha vizuri itapata kizazi chenye afya njema, ubunifu na maadili mema.

Waziri huyo alisema, Wizara imedhamiria kasi ya utekelezaji wa mikakati ya kupambana na changamoto za lishe na malezi chanya, kuimarisha huduma za afya ya mama na mtoto, kupanua huduma za uchunguzi na ufuatiliaji wa afya ya watoto, kuweka mazingira rafiki ya watoto kupata huduma na kucheza katika vituo na hospitali.




Nae Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Zanzibar Riziki Pembe Juma alieleza, Wizara ina jukumu la kuhakikisha watoto wote wanakuwa katika ustawi mzuri wa maisha yao yote, hivyo watashirikiana na taasisi zote zinazotoa huduma kwa mtoto, ili kufikia lengo.

‘’Kama tunavyofahamu ili mtoto akue vizuri pamoja na muelekeo sahihi katika makuzi yake, basi anahitaji kupatiwa vitu vyake vyote muhimu ili aweze kukua timilifu ambavyo ni afya bora, lishe nzuri, ulinzi na usalama, uchechemuzi wa awali na kujifunza kwake pamoja na malezi yenye mwitiko chanya kutoka kwa wazazi na jamii,’’ alisema Waziri huyo.

Alieleza kuwa, wamekuwa wakisimamia vyema Sheria ya mtoto ikiwemo nambari 6 ya mwaka 2011, sera na miongozo iliyopo, ili kuhakikisha sekta zote zinatekeleza utoaji wa huduma bora kwa watoto, ili kuwakuza katika muelekeo sahihi wa makuzi yao.

Mwakilishi kutoka Shirika la kuhudumia Watoto UNICEF Laxmi Bhawany alifafanua kuwa, uwekezaji wa mapema kwa watoto wadogo haswa katika siku 1,000 za mwanzo ikijumuisha miezi tisa ya ujauzito hadi kufikia miaka miwili ya kwanza, ni muhimu sana kwani asilimia 80 ya ukuaji wa mwili na ubongo unakamilika.

Alisema sayansi inaonesha kuwa, nyakati za awali za mtoto sio muhimu kwa maisha ya mtu binafsi pekee, bali huchangia katika mustakbali wa jamii, hivyo uwekezaji katika ukuaji wa watoto wachanga unaleta manufaa ya kudumu ambayo ni matokeo bora ya elimu, familia zenye afya na uchumi imara.

‘’Wakati wa mabadiliko ni sasa na yanaanza na sisi, kwa pamoja sisi ni chachu ya mabadiliko haya muhimu, tunaweza kubadilisha maisha,’’ alifafanua.

Ikisomwa risala katika kampeni ya uzinduzi huo, imeelezwa kuwa, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar inatambua kuwa, miaka ya awali ya mtoto ni kuanzia kuzaliwa hadi umri wa kuanza skuli, kwani ndio msingi wa maendeleo yake yote ya baadae.

Alisema kuwa, Wizara imekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha kila mtoto anapata huduma bora za malezi na makuzi kupitia programu za elimu ya maandalizi katika skuli za Serikali na binafsi.

 

‘Afya ya mtoto ni afya ya taifa. Lishe bora ni kinga bora. Malezi bora ni msingi wa amani na maendeleo’.

                                         MWISHO.




Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...