Skip to main content

IDARA YA KATIBA NA MSAADA WA KISHERIA KUWAPA ELIMU YA KISHERIA WANANCHI WAWI LEO HII

 


 

NANA HAJI NASSOR, PEMBA

WANANCHI wa shehia ya Wawi wilaya ya Chake chake, wametakiwa kuitumia fursa ya kuhudhuria mkutano maalum wa elimu ya kisheria, ulioandaliwa na Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria, unaotarajiwa kufanyika asubuhi hii shehiani humo.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Mkuu wa Divisheni ya Idara hiyo Pemba Bakari Omar Ali, alisema mkutano huo, ni maalum kwa ajili ya wananchi hao, ili kuwapa elimu na msaada wa kisheria bila ya malipo.

Alisema, mkutano huo ambao utafanyika eneo la Kwa gerei Wawi, ni sehemu ya utendaji wa kazi wa kawaida wa Idara hiyo, katika kuhakikisha jamii inapata muelekeo wa kutambua haki na wajibu wao kisheria.

Alieleza kuwa, zipo njia kadhaa za wananchi kujua haki zao za kisheria, moja wapo ni kuwapelekea wataalam wa sheria ndani ya shehia, na kuelezea changamoto zao.


‘’Mkutano huu ambao unatarajiwa kufanyika asubuhi hii shehia ya Wawi ni maalum, ili kuona wanapata uwelewa, lakini pia kuuliza na kutoa changamoto zao za kisheria,’’alifafanua.

Mkuu huyo wa Divisheni ya Idara ya Katiba na Msaada wa kisheria, alisema watalamu kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu, watendaji wa Tume ya Haki za Binaadamu na Utawala Bora pamoja na wasaidizi wa sheria wa Chake chake watakuwepo.

‘’Wataalamu hawa watahakikisha kila mwananchi atakaefika kwenye mkutano wa leo, na akiwa anajambo lolote la kisheria atauliza na kupata jawabu papo hapo,’’alisema.

Katika hatua nyingine, aliwahimiza wananchi hao, kuitumia fursa hiyo, kwani kinyume chake wakiwafuata baadhi ya wanasheria watahitaji fedha nyingi, ili kusikiliza na kuchambua changamoto zao.

Mapema sheha wa Wawi Khamis Mohamed Khamis, alisema matayarisho yote kwa ajili ya mkutano huo mkubwa wa wazi, yamekamilika.

Alisema, baada ya kupokea taarifa hiyo kutoka Idara ya Katiba na Msaada wa kisheria Zanzibar, alishakutana na kamati yake, na wameshatoa taarifa kwa wananchi.

‘’Niliwatumia wajumbe wangu kutoa taarifa kwa wananchi wa makundi kadhaa kama ya watu wenye ulemavu, watumishi wa umma, wakulima, waalimu wa vyuo vya qur-an na wanamichezo,’’alifafanua.

Mkurugenzi wa Jumuiya ya Wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake ‘CHAPO’ Mohamed Hassan Abdalla, alisema hiyo ni heshima kubwa kwa Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria kuwapa fursa ya kuandaa mkutano huo.

Msaidizi wa sheria shehia ya Wawi, Fatma Hilali Salim, aliwakumbusha wananchi wa shehia hiyo, kufika kwa wingi kwenye mkutano huo, ili kupata ufafanuzi wa changamoto zao za kisheria.

Mjumbe wa sheha Nassor Rashid Said na Katiba wa sheha Sham Haroub Said, waliipongeza Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria, kwa uamuzi wake wa kuandaa mkutano huo.

Mikutano kama hiyo, inatarajiwa kufanyika katika shehia za wilaya ya Mkoani, Wete na Micheweni.

                       Mwisho   

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...